Hapana,
Nipo kizota, ni mapumziko. JK amesisitiza kuhusu uungwana, kuhusu kejeli zenu na jinsi anavyoyachukulia. Jk amelaani Mtandao kuwapa wapiga kura orodha nzima ya NEC (wakupigiwa kura) kutoka kila kundi, amewaita wazi wazi Watoa Rushwa, na kasisitiza wapiga kura wawachague hata wale wasio na uwezo wa kwenda mikoani kutoa rushwa.
JK ameelezea maendeleo mbali mbali, ameongelea tatizo na Mbolea na namna serikali inavyolikabili, kwa kujenga kiwanda kwa ajili ya Minjingu Phosphate(sic)
JK ameongelea kuunganisha nchi kwa barabara, ya lami, ametaja ya Lindi na Singida zimeanza.
JK ameongelea kuundwa/kujengwa kwa reli ya kuunganisha TZ mpka BUrundi na Rwanda. Na kusema ya sasa (reli) njia ni ya mwaka 1910, hata mabehewa na Injini ukitaka kuagiza inabidi utengenezewe special kwa ajili yako, only TZ UG and Kenya are using this old tech.
JK ameongelea madini, ameelezea kuhusu mikataba, akasema wanaojadili hawana uwezo wa kuhujumu kwa kuwa sheria zote zimo. Amesisitiza loss carry forward ya 15% ndio tatizo na analishughulikia. Pia amesema madini inaingiza 1.9% ya pato la taifa. Ameelezea vizuri, kasoro ni moja why mikataba ni siri ndio hakusema
JK amesema kuhusu umeme Kilwa (soon kukamilika, Lindi na Mtwara kutumia umeme wa Gesi ya Mnazi mmoja.
Jk ameongelea namna falsafa yake ya maisha bora kwa kila mtz inavyofanya kazi.
JK ameongelea mafunzo kwa askari wetu na kuwajengea nyumba maafisa wake. Amesisitizia mafunzo kwa askari wakati wa amani.
JK ameongelea tatizo la Umeme kwa ujumla na kusema ni 10% tu ya watanzania wote wanapata umeme, wanaifanyia kazi hilo.
JK amesema mazungumzo ya muafaka yata resume soon, yalisimama kwa ajili ya kampeni ya CCM.
JK ameongelea mambo ya michezo na kusema wanaifanyia kazi.
JK ameongelea umasikini na jinsi alivyoifanyia kazi, jinsi alivyozungumza na CEOs katika CEO's roundtable, akaongela kuwa kama uchumi ukipanda kwa asilimia 10 kila mwaka basi pato la mtanzania inaweza kufikia kiasi fulani (nimesahahu) ikifika mwaka 2025, kiwango ambacho ni kidogo pia, amesema analifanyia kazi.
JK ameongelea UFISADI, amesema kuwa kuna tume ya maadili ipo na kuna PCCB, ameeleza wazi kwa wao hata ukituma SMS ni mali kwao Mwenyewe amesema anapokea SMS za tuhuma mbalimbali na zote zinashughulikiwa. Amesema, hata ukisemea mwembe Yanga au ulaya au hata kama ni minog'ono wao wanayafanyia kazi.
Jamani nasikia njaa ngoja nikapate msosi, foleni imepungua. Kaongea mengi sana ya maana jamani.
It was one of the best HOTUBA.
Unedited
Mzee wa Dom kwa leo