Lini Wakenya watazinduka na kuitazama Tanzania kama kioo badala ya kuendelea kuiona kama adui?

joto la jiwe

JF-Expert Member
Sep 4, 2017
26,117
46,613
Kenya ni nchi yenye matatizo mengi ya kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa sasa, ukabila, rushwa, ukosefu wa usalama, upungufu wa chakula, migogoro kati ya jamii za wafugaji, miradi ya serikali isitozingatia mahitaji ya wananchi, Covid -19, dhuluma ya umiliki wa athi, vurugu za kisiasa wakati na baada ya uchaguzi ni baadhi tu ya matatizo ya msingi yanayoikabila nchi ya Kenya.

Ukiangalia kwa makini ni kwamba, kwa kiwango kikubwa, Tanzania imefanikiwa sana katika kupunguza kama sio kumaliza kabisa haya matatizo. Kwa akili ya kawaida kabisa, ilipaswa Kenya kujifunza yale mazuri ambayo Tanzania imefanikiwa na ni rahisi kuyamaliza kwa mda mfupi kama kupambana na rushwa, kupambana na ujambazi, kuzalisha chakula, kupambana na Civil -19 na kuzuia ghasia katika vipindi vya uchaguzi, haya ni mambo yanayoweza kudhibitiwa ndani ya muda mfupi bila hata kusubiri BBI na katiba mpya.

Viongozi wa Kenya lazima wakubali kwamba kuna mambo mengi mazuri wanapaswa kuiga toka Tanzania, hakuna faida yoyote ya kujisikia aibu kwa kuiga mazuri yanayofanywa na jirani yako, hata kama ni adui yako, kwa kufanya hivyo Kenya itaendelea kubaki na matatizo bila kujinasua.

"If you can't beat them, join them"
 
Tanzania hii mojaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚., what are you smoking blind patriot? πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ facts ziko wazi., extreme poverty, lack of freedom, underdeveloped mashinani (poverty 80%), utapia mlo kwa watoto! big population na uchumi hafifu Eish! how can such be a mirror? A ka section of developed Dar inakudanganyaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚, tazama the 85% kisha uzungumze., pengine ni Tz iliyo akilini mwako tu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‰πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Na nyie mtaiga jambo lipi kutoka kwetu? Kwa kawaida WaTz wa hapa JF huwa wanasema kuwa Kenya ni failed state na hakuna jambo la kuiga kutoka kwetu. Sasa kama ni hivyo mbona kila mtu asikae kwao? Nyie mkae huko na sisi tukae huku.

Hakuna haja ya kuigana kama nyie hamna jambo la kuiga kutoka kwetu. Haiwezekani kuwa nyie mnasema hamna la kuiga kutoka kwetu halafu bado mnategemea sisi tuwaige. Hio bangi kutoka Moshi Tanzania sio nzuri. Muwache kuivuta
 
...no political freedom and democracy in Tanzania!πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‰ Media zimebanwa, serikali thrives on propaganda left right and centre creating a false illusion akilini mwa raiyaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ balaa! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Labda kioo cha Kenya ya 1980's, wakati wa KANU ya dikteta Moi na kikosi chake cha Flying Squad. Bila kusahau Nyayo Torture Chambers, ambapo wapinzani walikuwa wanapelekwa kufinywa map#mb# na pliers.

Enzi wakimbizi wa kisiasa kutoka Kenya walitapakaa kote duniani. Alafu kwa mtazamo wa wakenya hakuna adui yeyote mwingine wa taifa la Kenya ukanda huu, isipokuwa Somalia.

Uadui wa Kenya dhidi ya Tanzania upo tu kwenye akili za vibwengo wa Jiwe, kama wewe. Ingekuwa hali ndio ilivyo kama unavyodai tusingewaona watanzania wenzako wakitorokea Kenya wakati mna majirani wengine wengi.
 
Kwenye huu uzi mwanzisha mada anapigwa vita na Watanzania wenzake. Sisi tupo macho tu.
Sijui ni TZ gani anayoizungumzia!
Kuna mambo ya kwenu kweli huwa siyakubali, lakini haimaanishi yote ya TZ ni mazuri kupita ya Kenya. Na baadhi ya mambo yapo katika huu uzi.

Yaani mtu anadiriki kabisa kusema Kenya wajifunze kutoka TZ kwenye kudhibiti vurugu za kisiasa kabla na baada ya uchaguzi, kweli?!! Yaani yupo MTZ na akili zake kabisa anaamini namna ya kuthibiti vurugu za kisiasa inayofanywa TZ ni ya kuigwa!

Yupo MTZ anaamini miradi inayofanywa Kenya ni tofauti na ya TZ!! Miradi ya kwetu inayozingatia mahitaji ya wananchi ni ipi: treni, umeme, ndege, barabara, madaraja?! Kweli yupo MTZ mwenye akili za kudhani hii miradi haipo Kenya!
 
Hivi ni viongozi wa nchi gani walipelekwa The Hague wakahonga mashahidi na mashaidi wengine wakatishiwa kuuawa? Halafu bila aibu wanasimama kwenye majukwaa wakijiona wasafi.
Kenya wafungue chuo cha kufundisha unafiki
 
...no political freedom and democracy in Tanzania!πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‰ Media zimebanwa, serikali thrives on propaganda left right and centre creating a false illusion akilini mwa raiyaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ balaa! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
...no political freedom and democracy in Tanzania!πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‰ Media zimebanwa, serikali thrives on propaganda left right and centre creating a false illusion akilini mwa raiyaπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ balaa! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Rudia tena kusoma mambo niliyoyataja ambayo mnapaswa kuiga Tanzania, sijasema muige kila kitu, ngoja nirudie tena kutaja mambo ya msingi ambayo Kenya mnapaswa kuiga toka Tanzania

1) Ukabila
2) Rushwa
3) Sera ya kumiliki ardhi
4) Kupambana na iyambazi
5) Kumaliza mapigano miongoni mwa wafugaji
6) Kuzuia/ Kupunguza fujo wakati wa uchaguzi
7) Kupambana na Civil -19
8) Kudhibiti matumizi mabaya ya pesa za serikali
9) Kupunguza kukopa kwa miradi isiyokua na tija

Unadhani kwamba ni busara kwa serikali ya Kenya kuendelea kushuhudia wakenya wakipukutika Kw Civil - 19 wakati majirani wa Kenya kwa kiasi kikubwa wamefanikiwa kudhibiti hilo yayiza?
 
We have our problems: tribalism, unequal distribution of wealth and corruption is still with us.we have never said we are perfect. Nevertheless, kenya has made tremendous strides socially and economically despite the numerous challenges we are facing. we are okay with where we are and where we are heading. we have nothing to learn from tz, especially the current tz.

Its only a CCM fanatic who doesnt see there is something wrong with the current tz government. we dont want to go back to the Moi regime cz thats what we will be doing if we operate like tz
 
Kenya puppet nation inaamini sana kwenye fikra za usa and western europe countries, copy and paste.

Uchumi wao upo mikononi mwa watu weupe, hata viongozi wao wanapotoa matamko, sera zao wanalinda huusiano wao na mataifa makubwa haijalishi wananchi wanaumia kiasi gani hili mradi viongozi wanapiga pesa.

Jamaa wanataka sana international recognition at any cost hata kama hawanufahiki na chochote.

In short kenya sio wenzetu, ni wala wao hawatuoni hivyo.
 
Labda kioo cha Kenya ya 1980's, wakati wa KANU ya dikteta Moi na kikosi cha Flying Squad. Bila kusahau Nyayo Torture Chambers, ambapo wapinzani walikuwa wanapelekwa kufinywa map#mb# na pliers. Enzi wakimbizi wa kisiasa kutoka Kenya walitapakaa kote duniani. Alafu kwa mtazamo wa wakenya hakuna adui yeyote mwingine wa taifa la Kenya ukanda huu isipokuwa Somalia. Uadui wa Kenya dhidi ya Tanzania upo tu kwenye akili za vibwengo wa Jiwe, kama wewe. Ingekuwa hali ndio ilivyo kama unavyodai tusingewaona watanzania wenzako wakitorokea Kenya wakati mna majirani wengine wengi.
Hayo yote unayoyasema hakuna ushahidi wowote wa kuthibitisha wapinzani wanafanyiwa zaidi ya vichwa vyenu, ukiacha kupigwa risasi kwa Lissu, mambo mengine yote ni kelele za kawaida, huyo Lema aluyekuja huko Kenya ni sababu za kiuchumi wala sio sababu za kisiasa, ili kuthibitisha hilo, ubalozi wa Marekani kamwe hautokubali kumpa hadhi ya ukimbizi kama ambavyo anataka, soon atarudi Tanzania kuja kupambana na madeni yake anayoyakimbia

Nimeoridhesha mambo ambayo Kenya inapaswa kuiga toka Tanzania, sijasema muige demokrasia ya Tanzania, ulipaswa kuchangia yale maeneo niliyotaja badala ya kutaja maeneo ambayo sijayataja, au kwako ni sawa kuwaona wakeja wanakufa kwa njaa, Corona, ujambazi na ugaidi wakati nchi zinazowazunguka zinafanya vizuri katika hayo maeneo?
 
Back
Top Bottom