Kama CHADEMA wana akili wangejikita kwenye Katiba

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Nchi yetu ina matatizo ya aina 2
1. Matatizo ya kimfumo ambayo haya chanzo kikuu ni Katiba

2. Matatizo ya kiasili ambayo haya msingi wake ni Ujinga na mada hii ni pana sana.

Ili tuweze kupambana na matatizo ya kiasili ni muhimu na vizuri turekebishe matatizo yetu ya kimfumo ambayo msingi wake ni Katiba.

Katiba yetu ina matatizo makuu 2
1. Imetoa nguvu/ mamlaka makubwa kwa Wanasiasa kuliko watendaji wakati kiuhalisia mifumo thabiti ya nchi inajengwa na watendaji maana wanasiasa ni watu wa kupita na wa msimu

2. Katiba yetu haijaweka misingi imara ya uwajibikaji hasa kuwajibishana katika level ya Wanasiasa. Ni mara nyingi Sheria zinavunjwa na kukiukwa lakini hakuna kinachofanyika. Hii ni kwa sababu hakuna misingi ya kuwajibishana kikatiba.

Matatizo makubwa ya Nchi yetu yana msingi wa kikatiba. Na endapo mkazo ungewekwa katika Katiba basi nchi hii ingepiga hatua sahihi za kimaendeleo.

Nikiwasilikiza Chadema nacheka sana. Wanafanya siasa za pata potea tu. Haya maandamano yangekuwa na msingi sana endapo hoja kuu ingekuwa mabadiliko ya muhimu na haraka ya Kikatiba badala ya Sheria za uchaguzi.

Kama kilio Chao ni sheria za uchaguzi. Nina uhakika matatizo ya Tanzania hayataondoka hata kama wakija kuongoza chadema kama hatujatatua tatizo la msingi ambalo ni umbwe la Kikatiba.
 
Ungekua unafuatilia mikutanao yao sawasawa usingedhani kua chadema hawana hakili, yani wewe tatizo lako halieleweki kifupi nikua kila mkutano wa chadema kwasasa wanapinga katiba ya sasa lakini pia wanajenga hoja kwa kuchambua baadhi ya vipengele vilivyomo kwenye katiba hii kua havifai sasa tatizo wapi lipo?
 
Ungekua unafuatilia mikutanao yao sawasawa usingedhani kua chadema hawana hakili, yani wewe tatizo lako halieleweki kifupi nikua kila mkutano wa chadema kwasasa wanapinga katiba ya sasa lakini pia wanajenga hoja kwa kuchambua baadhi ya vipengele vilivyomo kwenye katiba hii kua havifai sasa tatizo wapi lipo?
Hoja kuu ya maandamano ni mapendekezo yao katika miswada ya Sheria iliyopelekwa Bungeni kutozingatiwa
 
Nchi yetu ina matatizo ya aina 2
1. Matatizo ya kimfumo ambayo haya chanzo kikuu ni Katiba

2. Matatizo ya kiasili ambayo haya msingi wake ni Ujinga na mada hii ni pana sana.

Ili tuweze kupambana na matatizo ya kiasili ni muhimu na vizuri turekebishe matatizo yetu ya kimfumo ambayo msingi wake ni Katiba.

Katiba yetu ina matatizo makuu 2
1. Imetoa nguvu/ mamlaka makubwa kwa Wanasiasa kuliko watendaji wakati kiuhalisia mifumo thabiti ya nchi inajengwa na watendaji maana wanasiasa ni watu wa kupita na wa msimu

2. Katiba yetu haijaweka misingi imara ya uwajibikaji hasa kuwajibishana katika level ya Wanasiasa. Ni mara nyingi Sheria zinavunjwa na kukiukwa lakini hakuna kinachofanyika. Hii ni kwa sababu hakuna misingi ya kuwajibishana kikatiba.

Matatizo makubwa ya Nchi yetu yana msingi wa kikatiba. Na endapo mkazo ungewekwa katika Katiba basi nchi hii ingepiga hatua sahihi za kimaendeleo.

Nikiwasilikiza Chadema nacheka sana. Wanafanya siasa za pata potea tu. Haya maandamano yangekuwa na msingi sana endapo hoja kuu ingekuwa mabadiliko ya muhimu na haraka ya Kikatiba badala ya Sheria za uchaguzi.

Kama kilio Chao ni sheria za uchaguzi. Nina uhakika matatizo ya Tanzania hayataondoka hata kama wakija kuongoza chadema kama hatujatatua tatizo la msingi ambalo ni umbwe la Kikatiba.
Ulisoma mapendekezo ya CHADEMA kwa kamati ya Bunge juu ya sheria za uchaguzi?
Tafuta ule uzi humu jukwaani,utaona ayo yote unayo lalamikia matatizo ya kimfumo kikatiba yameelezwa mule kwa kina.
 
Maandamano bado yapo sana, baada ya majiji, yatahamia kwenye miji mikuu.

Dai la Katiba Mpya ni kama vile lilipotezewa muda na yale maridhiano ya uongo, Chadema wakaweka matumaini yao kwenye mazungumzo matupu, kumbe upande wa pili ulikuwa unaongozwa na msanii.

Msanii mwenyewe akawadanganya mazungumzo yawe siri ili aendelee kuwapotezea muda, siku wakijakushtuka wasiwe na hoja ya kuwaambia wananchi kuhusu Katiba Mpya wakaeleweka ndani ya muda mfupi.

Ndio maana sasa wameona wahamie kwenye marekebisho ya sheria za uchaguzi, hili linaweza kufanyika ndani ya muda mfupi uliobaki na kuleta matunda kwenye chaguzi zetu zijazo za hivi karibuni.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Bora wewe ni CCM uliyemchukia Magufuli,na kumpamba sana Samia nyakati za mwanzo za uongozi wake.
MwanaCCM wa hivi hajawahi kuipenda nchi hii wala kuiwazia mema, mwanaCCM wa hivi huwaza tumbo lake,Hawezi kuitamani katiba bora.

Tafadhari stick na kumsifia Samia,usiwapangie CHADEMA cha kufanya.
 
Miaka 10 sasa toka rasimu ipendekezwe na kupuuzwa, bado tunaitaka ile au mchakato mpya?
 
Wakati wao wanafanya maandamano ww umejificha mpaka jina humu unatumia Bandia ww mchango wako ni upi wa kuipata Katiba mpya.
 
Kitu muhimu sana sasa si katiba ila tume halisi huru ya uchaguzi NA uchaguzi huru pia.
Haya yote mengine ya katiba n.k yatajinyoosha baada ya uchaguzi huru 100%.
 
Kitu muhimu sana sasa si katiba ila tume halisi huru ya uchaguzi NA uchaguzi huru pia.
Haya yote mengine ya katiba n.k yatajinyoosha baada ya uchaguzi huru 100%.
Hakuna mwanasiasa atakayeonja nguvu alizonazo chini ya Katiba hii atataka kuibadilisha. Amini maneno yangu
 
Maandamano ya CDM yanataka Katiba irekebishwe Ili kumpoka Rais mamlaka ya kuteua Tume ya Uchaguzi na wajumbe wake.

Hilo hujaliona wewe kuwa ni madai ya Kikatiba?
 
Nimeona mahali Mbowe anasema eti "Makonda katuchokoza,tunaanza nae" hapo ndipo niliona Mbowe hana akili kabisa.
Makonda anafurahisha wapiga kura sana,mambo anayofanya wananchi wanafurahia kwa kuwa wanajua mfumo umeshindwa kuyashughulikia.

Wanajua wanasiasa wote sio waaminifu na asilimia kubwa wapo kwa ajili ya maslahi yao na si ya umma.

Kitendo cha Mbowe kutaka kujaribu kupambana na Makonda kwa sasa,ni hatua nzuri ya kujimaliza mwenyewe kisiasa na kudharauliwa.
 
Back
Top Bottom