Hiyo pesa ni ndogo
Wenzako wakati tunasoma Lilikuwa 510k stationary 200k
Mipango ya biashara tulifikiri tukiwa kidato cha Sita.
Mwaka wa Kwanza ilikuwa kukusanya pesa.
Mpaka mwaka wa mwisho unakuwa ushanunua vitu vidogodogo vya Ghetto na biashara ndogondogo mtaji usiozidi milioni 2.
Laki sita alafu huna pakuishi, hapohapo mtaji ni uongo.
Kiufupi umeshajichanganya.
Hapo itakupasa laki tatu Nunua kitanda na godoro. Kitanda nunu used godoro nunua jipya.
Tafuta chumba cha elfu 40 lipa miezi mitatu 120k
Hiyo 180k iliyobaki nunua chakula cha elfu 80
Mchele wa Tsh 1800 kilo 10 =. 18,000/=
Maharage Tsh 3200 Kilo 5. =. 16000/=
Dagaa Nusu Kilo. 6000/=
Unga kilo tano mashineni 6,000/=
Kibiriti pakti chenye vibiriki 10. 500/=
Chumvi pakti 3 zile za buku
Kisado cha Viazi 4000/=
Kilo ya Kitunguamaji 2000/=
Mafuta Lita moja Alizeti 7000/=
Mahindi ya makande 2kg 2400/=
Sukari 1kg. 3000/=
Mche wa sabuni jamaa, 4000/=
Dawa ya Meno Tsh 3,000/=
Laki Moja itakayobaki
Nunua Jiko la gesi used mtandaoni elfu 10-15K. Jaza gesi Tsh 23,000/= jumla 38,000/=
Jiko la Mkaa Elfu 4
Nenda Karume,
Nunua pazia za mtumba mbili 10,000/=
Rudi tandale, shuka mbili Tsh 10,000/=
Utabakiwa na elfu 30,000/=
Hiya angalia AOB (any other bills) kama umeme hapo ulikopanga, maji au taka.
Kisha Anza msako wa KAZI, vibarua na vibolingo Association