Nilivyokuwa najiona mjanja, nikaishia kutapeliwa Milioni 42

Mr mutuu

JF-Expert Member
Jan 27, 2023
2,025
10,006
Wasaalam wakuu,

Nimeona kisa kimoja Cha Analyse akizungumzia mambo ya utapeli nikakumbuka balaa ambalo limewahi kunikuta, aisee tukizungumzia matapeli sio Hawa sijui wa Mr kuku, sijui kalynda, qnet na upuuzi mwingine ambao hizi chain scam wanafanikiwa kwa jinsi watu wanavyopenda kufuata mkumbo na kutajirika wakiwa kitandani, Kuna matapeli aisee wanatumia akili nyingi sio utani, mi Kila nikiwaza hata Leo njia waliotumia wakirudia bado Wana asimilia ya kunipiga tu, Kila nikiwaza nilipokosea hata sipaoni, unakutana na matapeli wapo radhi kutumia mamilioni na muda hata wa miezi 6 kujenga Imani, siku wakikupiga unabaki mdomo wazi.

Katika kisa hiki ntaleta vipande viwili tu, Moja ntaelezea maisha yangu ya awali ambayo yalinifanya nijiamini sana na kujiona mtoto wa mjini na kipande Cha pili japo kitakua kirefu sana ntaelezea nilivyotapeliwa M42 cash.. kipande Cha pili hata kama ntakiandaa kwa siku 2 ila siku nikikidondosha nakileta chote sitaki mambo ya episodes nyingi. Haya fuatilia kipande Cha kwanza.

Nilichaguliwa kwenda o level shule ya serikali, hapo hapo nilikua nimefanya interview na kupata shule ya private, Mzee akaniambia chagua shule unayotaka kwenda sitaki kukupangia Cha msingi sitaki matokeo ya kijinga kwangu, basi bana baada ya kuwaza sana na kusoma 'joining instructions' ya shule zote mbili nikaamua niende government school maana nilihisi ntapata uhuru sana wa kufanya mambo yangu, private nilijua tu Itakua geti Kali na mambo ya kufatiliana sana, nakumbuka bi mkubwa akaniita na kuniuliza mbona umechagua kwenda serikalini kwanini usisome private tu? Nikamwambia Mama usijali shule niliyochaguliwa japo ni ya serikali lakini Ina matokeo mazuri kitaifa kushinda hata Hio private, kwa shingo upande akakubali, ye Mzee nilivyomwambia chaguo langu Wala hata hakuniuliza chochote akasema sawa tu.

Siku ikafika nikapelekwa shuleni, wakati naandikishwa nikaona mabinti warembo wakiwa ofisini pale na visketi vifupi nikasema enhee mambo si ndo haya, watoto kama Hawa na uhuru wa
shule za government mbona mambo yamejipa yenyewe mapema hivi, baada ya kumaliza process zote na kupelekwa bwenini kuweka vitu tukarudi ofisini Mzee akiniandikishia pocket money ofisini(kipindi hicho pocket money unaandikiwa kwenye kitabu unakua unachukua kidogo kidogo ofisini)... Nikamsindikiza akaniachia na elf 30 nyingine(nyingi sana kipindi hicho wali nyama canteen unauzwa mia mbili). Basi akaitwa kiranja akaambiwa anipeleke darasani, kufika darasani naangalia vizuri aisee nilihisi kuzimia.

Nikapepesa macho nikawa siamini, kila nikirudia Kuangalia nikawa sielewi... Darasa limejaa mibaba mitupu, dah Kuna wengine mpaka videvu vimesagika, akilini hapo nawaza mbona sioni sketi hili darasa? Basi nikapewa dawati nikakaa bado nikawa naangaza angaza sielewi. Akili ikanijia kua watakua Wana utaratibu wa wavulana kusoma wenyewe na wasichana kua na darasa lao, utaratibu Gani huu nikawa nawaza, kwani tupo msikitini? Kinyonge nikatulia mpaka kengele ya lunch ilipogongwa, kutoka nikapata ujasiri nikamuuliza mmoja wa form one(njuka) mwenzangu mbona sioni wasichana darasani,? kuskia ivo huyu njuka akawa anacheka kinoma, kumbe bana tunavyotembea kuna ki mwalimu nyuma yetu kilikuaga ki andunje kinoma kimeniskia navyouliza, nikaskia kibesi huku nyuma kinajibu "shule hii boys tupu, we pumbavu umefata kitabu au umefata sketi huku" dah, kwa uoga nikanyamaza mpaka kufika hall.

Nafika hall nikawa sielewi naona wasichana tena huku, ndo yule njuka akaniambia shule Ina wasichana form 3 na 4 tu, serikali ilipitisha sheria ya kuwatoa kwa Hio intake ya form 2 na sisi form 1 ndo tumeanza kuja boys tupu. Kwa hio wakigraduate Hawa form 3 na 4 ndo ivo tena tunabaki vidume tupu!! Wajinga Hawa hawakubalidilisha joining instruction zao hivyo tulizopewa zilikua za miaka iliyopita ndo maana kule Kuna maelekezo yanaelekeza wasichana wabebe Nini na Nini, moyoni nikasema hapa nishaingia cha kike.

Anyway maisha yaliendelea poa tu, baada ya miezi 6 ya kuzoea shule nikawa nishajuana na watu wengi sana hasa hasa wanaonizidi kidato, ila akili yangu ikawa inawaza hapa nawezaje kutengeneza mfumo wa kupata pesa nikiwa shuleni, tulivyokaribia kumaliza form 1 nikawa nimeanza ka biashara ka kukopesha form 1 wenzangu(wale wanyongenyonge) pesa kwa riba, aisee naonaga sa ivi sijui walimu wanalia wanakopeshwa kwa riba kubwa na vikampuni Uchwara naishia kucheka tu, enzi zetu ukipewa elf 3 shule ikifunguliwa unaleta elf 10 na hakuna kubembelezana.

Form 2 biashara ilizidi kuimarika sana, mpaka nafika form 3 nilishakua alwatan shuleni hapo. Nilikua najikuta mtoto wa mjini sana, imagine o level nilikua nafahamika shule nzima kwa Dili za kukopesha pesa kwa riba, enzi izo watoto wa mama tunawakopa elf 5 unarudisha 15, Kuna jamaa wawili walikua wametoka shinyanga mipande ya watu(Mathias na Pascal)Hawa ndo walikua 'enforcers' wangu yaani nilikua kama nimewaajiri, ukizingua kulipa wanakuja kukudai Hawa wazee wa kazi ukiona sura lazima mkojo ubane, shule za government izo hakuna mambo ya kusemezea kwa walimu.

Nikawa napiga pesa sana, siku ya kufunga shule unanikuta na kitabu Cha mahesabu ni mwendo wa kukopesha waliokula nauli na nilikua na principle zangu mbili.

1) kama una mbavu mbavu au ni mbishi mbishi huwezi kupewa mkopo hata ukilia machozi ya damu

2) walionizidi kidato na ambao kwao sio mambo safi aisee pesa yangu utaishia kuiskia kwa wenzako tu

Hustle zikaendelea mtaji ukawa mkubwa, kufika form 4 nikawaza hapa nikimaliza shule ndo bye bye hakuna Cha kupeana mikopo Wala nini, basi nikanunua diskman tatu , nikachoma CD za kutosha Shuleni nikaanza biashara ya kukodisha diskman. Betri unanua mwenyewe mi nakupa diskman na CD tu, kila lisaa mia mbili, usiku mzima 1000. Kimasihara nilitengeza pesa nikawa mpaka nalaza elf 8 Kila siku. Maisha ya o level niliishi vizuri sana na nilijifunza hustles nyingi sana.

Advance mimi tena huyo shule ya government, mtaji ushakua, likizo Kuna biashara za home nilikua nasaidia nikawa sikosi vichenchi, nikawaza huko naenda kupiga hustle Gani, nikapata wazo. Kipindi hicho hakuna hata dalili za smartphone, simu za kishua zilikua Nokia double screen yaani ujinga mtupu hazina hata la maana na N- series za Nokia ndo zilikua zimetoka, Bei mlima!! Motorolla nao walikua wameleta L7 simu inayotumia memory card. Kipindi hicho nadhani ni N- series tu za Nokia na huyu motorolla ndo zinasupport memory card, kiufupi ilikua unyama mwingi Sana enzi hizo, baada ya ku scout mazingira ya shule na Kuona hakuna ukuda,
Nikanunua motorolla L7 nne na memory card zake kwa akiba niliyokua nimeipata kwenye hustle zangu za o level na kipindi Niko likizo.

Kila memory card nikajaza miziki na video za ngono(x) za kutosha. Nikaanza biashara ya kukodi simu 500 kwa lisaa. Aisee asikuambie mtu wanafunzi wanaangalia x Kama vichaa, ndani ya mwezi nishajulikana shule yaani mpaka form 6 wananiheshimu kinoma, chimbo la biashara lilikua kwa mwanangu mmoja alikua social prefect so alikua na ofisi huko huko ndo tunachajia simu, kama kawaida hizi biashara bila 'mbavu' hua haziendi kwa io nikampa jamaa mmoja wa form 6 'ajira isiyo rasmi' akawa ndo anawafatilia Hawa watu warudishe Simu kwa wakati na wasije tapeli simu!!

Kazi yangu Kila jumamosi nashuka mjini kulikua na mshkaji ana burn cd ana kibanda chake naenda futa x zilizopo nawawekea mzigo mpya, kazi ilikua ya Moto sana kuna siku mpaka raia wanagombania simu, changamoto pekee tuliopata Kuna siku mjinga mmoja kakodisha simu kufika muda wa kurudisha akadai imeibiwa, tukazungushana nae kama siku 3 ikafika mahali mbavu akaniambia huyu ngoja nimtie vitasa iwe fundisho na kwa wengine, nikawaza nikamwambia hapana hapo utaharibu maana biashara hizi haramu walimu wakijua tumekwisha.

Jumamosi kama kawaida nikashuka town, nilivyorudi jioni nikakuta Kijiji Cha wanafunzi kinasubiria si wanajua mzigo mpya, nikawaambia nimesitisha biashara, kuuliza kwanini, nikawajibu siwezi poteza simu ya laki mbili( kipindi icho mlima mkubwa) kisa kufukuzia jero jero zao, aisee ilikua kama msiba, wazee wa kukodisha wakawa hawaelewi.. acha kitu inaitwa addiction Mzee, Kuna watu walifanya kazi kama fbi haikupita wiki simu iliyopotea ikapatikana, alikua huyo huyo mjinga alijifanya kaibiwa.

Form 6 nikaongeza simu nyingine 3(Nokia express music). Niliipata pesa nyingi sana Mungu anisamehe kuna watu nahisi pocket money zao zote ziliishia kwangu mpaka nikawa nawapa ofa tu, biashara ilikufa miezi kama mitatu kabla ya kufanya mtihani wa mwisho kuna waalimu wakuda waligundua hii ishu ya simu japo hawakujua mambo ya x so ikabidi niachane nayo. Itoshe kusema advance nilipiga sana pesa, kipindi hicho shule wananiita 'smart gangster' basi nilikua najiona mjanja kupita maelezo

Baada ya kumaliza advance, nikawa namsaidia Mzee biashara zake huko Nako nikawa sikosi 20 kwa siku, mpaka naenda chuo kwenye akaunti yangu ya crdb nilikua na mzigo wa kutosha, chuo napo nilikua najiona mjanja sana nakumbuka 1st year nawaona wanapanga foleni kuchukua hela ya boom na stationary (620,000/=) nikawa nawacheka kimoyo moyo nawaona Wana njaa sana, pesa yangu Nilichukua baada ya kama miezi miwili mpaka mhasibu akawa ana mind ulikua wapi muda wote huo.

Miezi kadhaa mbele nilivyozoea jiji Kuna mshkaji akawa ananipeleka kkoo kwa mhindi mmoja anatuuzia flash na hizi scientific calculator Bei Chee sisi tunakuja kuuza chuo na kusupply calculator mashuleni. Baada ya miezi kadhaa biashara ikakua sana ikafika mahali mhindi anatupa mzigo mkubwa tena kwa Mali kauli, tuna supply stationary za mashuleni kwa mkopo, wanauza wanatupa pesa zetu zikitimia tunampelekea muhindi maisha yakasonga tukazidi kujitanua mpaka mikoa ya karibu

Kuna siku nipo Facebook naongea na mwanangu mmoja ye aliacha shule tukiwa form 3 akaenda marekani mama yake aliolewa na mzungu Kule, akanipa Dili ambalo lilinitengenezea mamilioni ya pesa, kipindi hicho ipad ndo zimetufikia huku, tena ni ipad 2 ndo ziko sokoni, kkoo wanaogopa kuziuza maana Bei ilikua mlima sana kipindi hicho, ukitaka ipad kuna duka posta ndo wanaziuza, 1.3M kipindi hicho, jamaa akanipa mchongo akawa ananitumia ipad used kwa Bei ndogo tu mi nikawa naziuza laki 6 tu, tena zinakua kwenye Hali nzuri Yani kama mpya, hii kitu iliniletea umaarufu sana chuo, ma sista du na ma braza men kipindi hicho ukiwa na ipad umemaliza (wajinga Samsung walivyoleta tablet zao soko likapungua). Nilikua na uwezo wa kupewa hata pesa ya ipad kumi mzigo haujafika ukifika ndo naanza kumpa Kila mtu ya kwake, yaani nilikua nauza kwa order na pesa inatangulia, kila ipad ilikua Inaweza kunipa kuanzia laki na nusu au zaidi kama faida

3rd year nikanunua usafiri wangu(ka baby walker) utaniambia Nini, jamaa zangu kipindi hicho wakawa wananiita 'mastermind' yaani Kila Dili nipo, nilishawahi kufanya sana kazi za kuprint t shirt za shule yaani napokea order ya shule nzima na sikua hata na printing office basi tu kujuana na watu, mpaka shule za Tanga huko!!! Chuo nilifanya biashara nyingi sana mpaka na graduate nakaribia 50M kwenye account.

Basi bana na ujanja wangu wote nikaja kupewa Dili la kuzama china kuchukua mzigo, kipindi Hiko chimbo la china ndio kwanza linagundulika,wachina huku nadra kuwaona sio kama siku hizi wamejaa kama siafu! hapo sasa ndo nilikutana na watoto wa mjini haswa nikasokotwa M42 cash, yaani jasho langu kuanzia form one mpaka chuo Kuna wase*ge wakaja kunipiga kifala, hapo ndo niliamini bado sijawa mjanja town na niliamini Kuna kuchezewa kiini macho, tukutane kipande kijacho nikuelezee mwanzo mwisho nilivyotapeliwa, hii sehemu ya kwanza nimeileta tu ili muone jinsi pesa niliyoitolea jasho inavyopigwa na wahuni kizembe, hii sehemu ya pili ndo itabeba mkasa mzima wa kisa changu, ntaandika hata kama ni siku mbili afu ntaileta yote hakuna mambo ya...

Itaendelea....
 
Siti hii hii itanifaa!
JamiiForums1527087124.jpg
 
Back
Top Bottom