JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Wanaharakati wa Katiba na Haki za Binadamu wamekosoa kauli ya Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro juu ya kutoa elimu ya Katiba kwa kipindi cha miaka mitatu, wakidai mpango huo unalenga kuchelewesha mchakato na upotezaji wa fedha za umma.
Tamko hilo limetolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) na Jukwaa la Katiba (JUKATA) likieleza Elimu ya Katiba mpya imeshatolewa na Tume ya Jaji Warioba na Bunge la Katiba, hivyo fedha zilizotengwa zitumike kuanzisha mijadala kuendesha mchakato shirikishi na waharaka.
Wanapendekeza muda wa kuandaa Katiba hadi ipatikane na kutumika usizidi miaka mitano, kwa kuwa kutoa elimu kwa miaka mitatu kunaweza poteza muda mwingi wa kuandaa mchakato na inaweza kufika Mwaka 2030 wakati wa Uchaguzi Mkuu pasipokuwa na Katiba mpya.
Wanaharakati wa Haki za Binadamu wakizungumza na Waandishi wa habari wakati wakitoa tamko la kupinga mpango wa Serikali wa kutoa elimu ya katiba kwa miaka mitatu wakidai hatua hiyo ni kupoteza muda na fedha za wananchi.
Tamko hilo limetolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) na Jukwaa la Katiba (JUKATA) likieleza Elimu ya Katiba mpya imeshatolewa na Tume ya Jaji Warioba na Bunge la Katiba, hivyo fedha zilizotengwa zitumike kuanzisha mijadala kuendesha mchakato shirikishi na waharaka.
Wanapendekeza muda wa kuandaa Katiba hadi ipatikane na kutumika usizidi miaka mitano, kwa kuwa kutoa elimu kwa miaka mitatu kunaweza poteza muda mwingi wa kuandaa mchakato na inaweza kufika Mwaka 2030 wakati wa Uchaguzi Mkuu pasipokuwa na Katiba mpya.
Wanaharakati wa Haki za Binadamu wakizungumza na Waandishi wa habari wakati wakitoa tamko la kupinga mpango wa Serikali wa kutoa elimu ya katiba kwa miaka mitatu wakidai hatua hiyo ni kupoteza muda na fedha za wananchi.