LHRC: Kukiuka haki ya afya ni kukiuka haki ya kuishi kinyume na Ibara ya 14 ya Katiba

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460

01.jpg

012.jpg
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa takribani juma moja sasa kimekuwa kikifuatilia kwa karibu mjadala ulioripotiwa katika baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii juu ya mgogoro kati ya watoa huduma wa afya kutoka sekta binafsi pamoja na Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya (NHIF) kuhusu viwango vinavyotozwa na watoa huduma kutoka sekta binafsi kwa wateja wanaotokana na bima ya afya inayomilikiwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Kupitia taarifa yake kwa umma Vyama vya Watoa Huduma Binafsi za Afya nchini yaani, Association of Private Health Facilities in Tanzania (APHFTA), Christian Social Service Commission (CSSC) pamoja na BAKWATA iliyotolewa tarehe 27 Februari 2024 ilibainisha bayana kwamba vituo vya afya binafsi vingeshindwa kutoa huduma kwa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kutumia kitita kipya ambacho hawakubaliani nacho.

Taarifa hiyo ilienda mbali zaidi kwa kuwataka wanachama wa NHIF kuwasiliana na mfuko wa bima ya afya (NHIF) ili kupata hatima ya namna watakavyopata huduma hizo.Kwa upande wake Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kupata taarifa yake kwa vyombo vya habari ya tarehe 1 Machi 2024 ulikiri kuona tangazo la kusitisha huduma kwa wanachama wa NHIF kwa baadhi ya vituo binafsi, hivyo kuwataka wanachama wake kutumia vituo mbadala ili kupata huduma wanazohitaji, pili, maofisa wake watakuwa katika vituo ili kuhakikisha wanachama wenye changamoto wanasaidiwa kupata huduma katika vituo vingine, tatu, mfuko ulikuwa umeshaanza kuwasiliana na wanachama wenye matibabu yanayohitaji mwendelezo ya huduma ili kuwaelekeza vituo mbadala kwa ajili ya kupata huduma husika.

Kwa mazingira tajwa, ni dhahiri kuwa kuna mgogoro katika watoa huduma, vituo binafsi na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), mgogoro ambao moja kwa moja umeshaleta athari kwa watanzania wasio na uwezo wa kulipia vitita vya ziada au fedha taslimu kupelekea uvunjifu wa haki za binadamu kama haki ya afya na ile ya kuishi.

Kwa nyakati tofauti Mahakama kuu ya Tanzania katika shauri la Festo Balegele na wenzake 794, dhidi ya Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam, shauri namba 90 la mwaka 1991 na lile la Felix Joseph Mavika dhidi ya Tume ya jiji la Dar es Salaam, shauri namba 316 la mwaka 2000, yote kwa pamoja Mahakama kuu ya Tanzania ilitamka kuwa kukiuka haki ya afya ni kukiuka haki ya kuishi kinyume na ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

Tanzania ni nchi mwanachama wa mikataba mbalimbali ya kimataifa na ile ya kikanda ambayo yote kwa pamoja inazitaka nchi wanachama kulinda na kuhifadhi haki ya afya. Kwa mfano ibara ya 12 ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni wa mwaka 1966, ibara ya 16 ya Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu wa mwaka 1981 pamoja na ibara ya 16 ya Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto wa mwaka 1981, yote kwa pamoja inazitaka nchi wanachama kulinda na kuhifadhi haki ya afya.

Mwisho, kutokana na sintofahamu hii LHRC inatoa wito kwa Serikali na watoa huduma kama ifuatavyo:

i. Serikali itafute mwafaka wa mgogoro huu na watoa huduma ili

kuepusha kuvunjwa kwa haki ya afya

ii. Wakati mazungumzo yanaendelea na mwafaka ukitafutwa, watoa huduma waendelee kuwahudumia watanzania ili kuepusha madhara ya kupoteza uhai wa watanzania wasio na hatia.

iii. Serikali iweke wazi viwango vya gharama za kitita kinachobishaniwa ili kuongeza wigo wa Uwajibikaji na uwazi.

iv. Serikali iheshimu na kutekeleza maadhimio ya bunge lililoitaka Serikali kutatua mgogoro huu kwa njia za mazungumzo.

v. Watoa huduma wafuate utaratibu uliopo kisheria kuwasilisha

malalamiko yao wakati huduma zikiendelea kama kawaida.

vi. Kwa kuwa wahanga wakubwa ni wanawake, watoto, wazee na watu wenye ulemavu, tunashauri makundi haya yaendelee kupewa kipaumbele katika kipindi ambacho mazungumzo yanaendelea.
 
Hapo anataka kuelemeza mzani upande mmoja hivi ,labda tumuulize what abt right to property kwnye hiii ishu labda ni nani anaivunja hio haki apo
 
Hapo anataka kuelemeza mzani upande mmoja hivi ,labda tumuulize what abt right to property kwnye hiii ishu labda ni nani anaivunja hio haki apo
 
Back
Top Bottom