Leonardo Da-Vinci

Leonardo Da-Vinci

mkuu umemsikia alivyosema,
"vilivyobakizwa nakala zipo vatcan kavunje uchukue"
ndio maana niligusia vatcan kipindi fulani.
hii tu inathibitisha kuwa vipo vitabu vilivyoachwa kwa sababu ya walioviacha zaweza kuwa nzuri au mbaya kwangu mimi naona kitendo cha kuacha hakikua kizuri.
ulisema najiuliza maswali ambayo hayapo na kuwa hakuna kitabu kama cha mary magdalena kama kingekuwa tungeshakiona.

sasa unamsikia ndugu tedo anasema kavunje vatcan?
vitabu vipo na viliachwa makusudi. wao wanadai kwa maslai ya kanisa na imani.
mimi naendelea kusema ni kwa maslai yao binafsi wala sio kanisa.

Ngoja nikuulize,hivi ni kitu gani kinakufanya uamini hivi vitabu vipo?
Umeshaviona?

Kama umesha viona,ni kitu gani kunakufanya uamini viliandikwa na hao wahusika na sio kwamba vilitungwa tu na watu kwa maslahi yao binafsi?[kuleta coffusion]
 
sasa mkuu unakuja katika pointi zangu, kama kanisa katoliki huliamini na kumbuka kanisa hilo linaongoza mamilioni ya wakristo na kuamua mambo mengi sana ya ukristo
Sio kweli kuwa wanaamua mambo mengi ya Ukristo
Sema wanaamua mambo ya Wakatoliki
na huku wakidai wanaongozwa na mungu,
Hata wewe unaweza kudai kuwa unaandika haya kwa uongozi wa mungu
Suala tatizo ni kuwa ni mungu yupi anaekuongoza

Tatizo sio watu kudai kuongozwa na mungu
Suala ni mungu yupi huyo?
Kuna Mungu na miungu na yote inadai ni miungu
Lakini kila Mungu ana sifa zake na namna ya kufanya kazi
Huwezi kusema wewe ni binadamu na huna sifa za ubinadam

Kanisa katoliki kwa upande wake lina mengi na mengi kati ya hayo yako kinyume na Mungu
Kuna sanamu nyingi sana zinazowakilisha upagani
Katikati ya uwanja wa wazi kule Vatcun kuna kitu kinaitwa obelski jaribu kufuatilia utajua hii maana yake nini
Kanisa katoliki lina mtu anaitwa Qeen of heaven unamjua ni nani huyu?
Huwa anasanam yake amebeba mtoto mikononi mwake
Unajua hii ni nini?

Kuna mambo mengi sana yanayoweza kukuonesha kundi fulani linamuabudu au kuongozwa na mungu yupi!
unapingaje madai yangu kuwa mazao ya kanisa katika ukristo yanakasoro wakati mwingine????????????
Sijui unamaanisha nini hapa
Lakini nataka nikuweke wazi tu kuwa,kanisa linaweza kuwapotosha waumini wake kama hawasomi maandiko lakini kamwe haliwezi kuyavuruga maandiko matakatifu kwa kuwa yanalindwa na Mungu mwenyewe!
na kutokuamini hukuhuku ndiko kunakonilazimisha na mimi nisiamini waliochagua vitabu vipi viingie katika biblia hawakuwa wamefanya hivyo kwa nguvu za mungu bali mapenzi yao wenyewe na sababu zao wenyewe.
Mh!
Unajicontradict dada!

Why unamuamini Mungu wa Ibrahim,Isaka na Yakobo?
Huyu Mungu umempata wapi?

Halafu unatengeneza hatari moja iliyoko mbele yako
Utakuja kutokuwa muamini wa Mungu soon

Biblia haimuelezi Mungu kama alivyo bali inamuelezea baadhi ya sifa zake na namna ya kuishi vyema,hakuna namna nyingine yoyote ya kuishi ya kumpendeza Mungu tofauti na hiyo,kama unatilia mashaka hilo ni bora ukaacha hata kusali kwa kuwa huna uhakika wa unalofanya

Halafu hata huyo Mungu unaedai unamjua humjui na unamkana ukuu wake kwa kushindwa kulilinda neno lake ambalo aliahidi halitapita,kitendo ambacho kama bado unaendelea kumuabudu unajiingiza kwenye ktego wako mwenyewe

Unaweza kuniambia kuwa umemuona Mungu nje ya biblia lakini kitendo cha kutaja Mungu huyo ni wa Ibrahim.Isaka na Yakobo tayari umemtaja Mungu wa kwenye biblia!
 
umekosa tofauti yangu mimi na wewe ni kuwa wewe unaona vitabu vilivyoachwa kuingizwa katika biblia si vya muhimu ama havipo. na kwamba biblia ni timilifu.
Sio kwamba naona sio vya muhimu tu bali hivi vitabu kama vipo vimeandikwa na wapinzani wa Mungu ili kuwachanganya watu kama nyie
mimi kama ulivyo wewe naiamnii biblia kwa maana yale yaliyoandikwa kwa vitabu vilivyopo sasa vinatosha kunipa elimu fulani.
Hapa unatumia tafsiri gani ya Imani?
BUT siamini kuwa haijachakachuliwa, na kumbuka ni imani tu ndiyo inayonifanya niimani biblia.
Nimeshakuambia kuwa unafall kwenye trap ya waislam ya madai yao kuhusiana na hili,kwa wewe tu kudai imechakachuliwa umekosa sifa ya kuitumia vyovyote vile kwani nitakuambia ni kwanini unamuamini Mungu ambae ameshindwa hata kulinda neno lake mwenyewe?
Ni eneo gani imechakachuliwa na kwa ushahidi gani?

Kauli yako ya "imani tu ndo inanifanya niiamini biblia" inapofusha maana nzima ya imani,inaonekana kuwa na imani ni kama ujinga fulani hivi,yaani unakwenda kikondoo bila kuhoji jambo ambalo sio kweli

Tazama maana ya imani ndani ya biblia
"Imani ni kuwa na hakika na mambo ya jayo ni bayana ya mambo yasiyoonekana"

Una imani kweli wewe?

ila kwa kusema naiamini hainikatazi kuhoji pale ninapoona kuna shida. kwani chochote kilichofanywa na binadamu hakikosi kasoro au mapungufu. ni mungu pekee ndiyo mtimilifu. laiti biblia ingekuwa imeshuka toka mbinguni, kwa kuthibitika hivyo nisingekuwa na shaka.[/QUOTE]
 
mimi nikikuwa nakuuliza maswali yale si kwamba siamini biblia au mungu, rejea post zangu zote utaona, ila nilipishana na wewe uliposema kuwa yale yaliyochaguliwa kuwa katika biblia ndio matakatifu na mungu kawaongoza waliochagua na yale yalioachwa si matakatifu ndio maana hayapo tena na kwamba mungu neno lake halipotei.
hapa tu ndipo mimi na wewe tunapopishana hadi sasa mkuu.
msingi wa maswali yangu ni kuwa una uthibitisho gani kuwa haya yaliyo katika biblia yetu ya sasa ni matakatifu na yaliyoachwa si matakatifu?
Dada,unajichanganya vibaya sana
Huwezi kuamini jambo fulani limefanywa na fulani halafu uje ukane tena kuwa hajafanya
Kauli yako ya kwanza inasema unaamini biblia kuwa ni kamilifu,halafu unakuja kusema siamini na hili linathibitishwa na kauli zako hizi za "mimi nikikuwa nakuuliza maswali yale si kwamba siamini biblia au mungu" na hii " una uthibitisho gani kuwa haya yaliyo katika biblia yetu ya sasa ni matakatifu" hizi kauli hazitoki kwa mtu makini na anachikifanya[samahani kwa hili]

Kama kweli ungekuwa unajua Mungu ni nani na unasoma maandiko usingeniuliza kuwa ninaamini maandiko hayo ni matakatifu kivipi kwa kuwa majibu yako yanaishia tu pale utakapojua kuwa Mungu hawezi kushindwa kulinda neno lake!
mchezo wa binadamu ni mchafu akiwa na nia chafu ili hali ipo katika uwezo wake kwa nini ashindwe
Kwanini asiiondoe aishie kuchakachua?
Hivi unajua kuwa Kanisa katoliki lilijaribu kuiangamiza biblia likashindwa?

naamini yaliyo katika biblia na naamini pengine yaliyoachwa kuwa pia ni mazuri kuachwa kwake kuingizwa katika mjumuiko wa biblia ndio tatizo kwangu.
What make you believe this?
Huamini hata uwezo wa Mungu wako unaedai unamuabudu?
 
mkuu
ninaisoma biblia kwa sababu ina mambo yanayumzungumzia mungu.
biblia ninayoisoma ni ile inayoitwa biblia takatibu yenye agano la kale na jipya.
hakuna sehemu mungu alipotajwa jina lake ambalo labda mimi na wewe tunayajua kuwa ni majina ya watu. amekuwa akiitwa kwa majumuisho tu mungu wa baba zenu, mungu wa isaya, mungu wa jakobo na kuendelea.
Dada umenishangaza sana
Mazoea yanakusumbua sana

Wewe unadhani jina ni kitu gani?
Hujui kuwa ni utambulisho?
kwa maana ya majina haya tunayoyajua.
Majina tunayoyajua ni nini?
Ulitaka Mungu aitwe Hassan ndio ujue ni jina?
mungu hana jina watu wamekuwa wakimuita kwa majina mbalimbali wengine bwana, wengine baba, na mengine mengi ikiwa kuna jina la mungu naomba nijulishe n ami nitakuwa nimejifunza kitu.
Kwanini usiulize tangu mwanzo kama ulikuwa hujui?
Kitendo chako cha kusema majina tunayoyajua kimeonyesha level ya juu sana ya kiwango cha ujinga[kutokujua] ulichonacho
kutoka sura 3 mstari wa 14-15 musa alitumwa kwenda kuwaambia watu kitu, akamuuliza mungu watu hao wataniuliza ni mungu gani huyo anaitwa nani, mungu akamjibu musa akamwambia kawaambie MIMI NIKO AMBAYE NIKO amenituma kwenu.
Dada hebu achana na mazoea ya kuona majina kama ya Juma,Anet,Justine n.k na kuamini hayo na ya mtindo huo ndio majina tu na mengine sio majina
Inaonekana uwezi wako wa kuchambua mambo ni mdogo sana hebu tumia muda wako kufanya tafiti ya mambo mbalimbali na utapata ufahamu

Kuna jamaa yangu mmoja amemuita mtoto wake Utukufu,kwako hili sio jina kwa sababu haliko ki mtindo wa Chrstina,lakini ukikuta Glory utasema hili ni jina!

Sikujua kama hii ndo level yako ya kufikiri!
sasa mimi niko ni jina?
Ki ukweli nimejisikia vibaya sana kwa swali lako hili!
Haya ndio matatizo ya kukariri!
 
Bila samahani!
Mimi ni mkristo lakini sina dhehebu!

Ok sasa kama ni mkristo ila huna dhehebu ..... inamaana unaamini biblia bila shaka.....sasa hujui kuwa biblia ilitengenezwa na hao wa roma na ndo kanisa la kwanza sasa iweje usiwaamini roma wakati unaamini biblia waliyo tengeneza
 
Ok sasa kama ni mkristo ila huna dhehebu ..... inamaana unaamini biblia bila shaka.....sasa hujui kuwa biblia ilitengenezwa na hao wa roma na ndo kanisa la kwanza sasa iweje usiwaamini roma wakati unaamini biblia waliyo tengeneza

Acha kurukia mambo
Soma post zangu zingine!
 
mkuu huyo mwandishi DAN BROWN aliandika vitabu vyake vyote baada ya miaka mingi sana kupita tangu kufa kwa Leonardo Davinci ,kutokana na michoro ya davinc..hakuibua yeye taarifa hizo.....Leonardo alizikuta taarifa hizo......, usimuhukumu mwandishi...tuambie uzushi huo ulianza lini na kwa nini.....kwa nini wanatheologia wanawashambulia sana watu wanaoleta taarifa hizo..kwa nini wengine waliuwawa, kwa nini waliokuwa wanahoji kuhusu bible na ukristu kwa ujumla waliishi kwa tabu sana zama hizo?.........mkuu usichezeshe Lugha......tunajua fiction ni kitu cha Kubuni....lakini hii kitu ni Fact though is highly probable

Ukweli daima utabaki kuwa uzushi upo tangu kitambo yaani zama za kale,Dan Brown ni mtunzi wa vitabu wa zama zetu sasa unaposema unaamini fiction zake nakushangaa sana kwa sababu ni sawa na kuamini hadithi zilizotungwa kama Alfu Lela Ulela (siku elfu na moja) amabazo ni maarufu kuanzia Persia ,mashariki ya kati hadi Afrika kusini.Zimesimuliwa enzi na enzi na zilisimuliwa ndani ya Safina ya Nuhu(wanavyoamini watunzi kwani ni mkusanyiko wa hadithi nyingi).Kuhusu kanisa kuficha ukweli ni kosa la kipindi kile cha giza yaani Middle Ages ambapo ni kipindi cha historia ya Ulaya tangu kuanguka kwa dola ya Roma mwaka 1000 mpaka kuanguka kwa Constantinople 1453.Viongozi wa kanisa walizuia watu wasisome biblia na waliokutwa nazo walchomwa moto.Viongozi hawa hawakuweza kuwaza nje ya box na hawakupenda mawazo mapya ndiyo maana akina Nicolaus Copernicus wa Poland (1473-1543) alipokuja na wazo kuwa Jua lipo kati kati likizungukwa na sayari zingine na sio dunia pamoja na wanasayansi wengine kama Galileo Galilei walipingwa vikali na kuonekana wanakufuru.Uzushi wanaJF ni mwingi na wanaibuka wazushi wengi kupinga kweli kutokana na watu kuwa na mismamo na mitazamo tofauti.
 
kwikwiiiiikwiii
inawezekana kabisa mkuu, ila upo pia uwezekano kuwa ndiyo huyohuyo wa kwetu afrika na ndiyo huyo wa isaya na yakobo ila namna tu alivyokuwa akiitwa na kufikiwa, sisi tuliamini mito mikubwa ni mungu,milima mawe na vinginevyo pengine ni namna tu ya kumwita na kumuabudu.

si kweli km waafrika walikua wanaamin mito mikubwa au milima ndio mungu, bali wanaamini ni sehemu takatifu ambazo nguvu za mungu zinakua zinafanya kazi kwa urahisi au zinatendeka na ndio maana wanaenda kuomba huko

kwa mf kuna makabila kule kilimanjaro walikua wanasema ni mlima wa mungu na sio kwamba ule mlima ndio mungu, naomba uelewe hio tofaut
 
Daah this is not fair uzi umehamishwa kutoka Leonardo Da Vinci na michoro yake na kuwa mada ya kidini!!!!!!!!Dhehebu lako ni lipi?unaamini biblia au huamini?Yesu alikufa au la?JAMANI JAMANI TUTUMIE COMMON SENSE TU SI LAZIMA KUCHANGIA IL MURADI KUCHANGIA ILI KULUMBANA TUWE NA LOGIC NA VIELELEZO PIA.TURUDI KWENYE MADA KUU
 
Isaya 53 : 5-12
53.5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
53.6 Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.
53.7 Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.
53.8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
53.9 Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
53.10 Lakini Bwana aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake;
53.11 Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao.
53.12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini alichukua dhambi za watu wengi, Na kuwaombea wakosaji.


..........ile aya katika Biblia inayosema kuwa 'kila mtu atabeba furushi lake mwenyewe' ina maana gani ??:A S-confused1:

ikiwa Bwana Yesu amebeba dhambi za watu wake, huwa Kanisani mnatubu dhambi zipi ambazo Yesu hakuzibeba !???:shocked:
 
[/B]

..........ile aya katika Biblia inayosema kuwa 'kila mtu atabeba furushi lake mwenyewe' ina maana gani ??:A S-confused1:

ikiwa Bwana Yesu amebeba dhambi za watu wake, huwa Kanisani mnatubu dhambi zipi ambazo Yesu hakuzibeba !???:shocked:

Ile aya hipi, weka ushahidi siyo unaandika tu.
 
Ok sasa kama ni mkristo ila huna dhehebu ..... inamaana unaamini biblia bila shaka.....sasa hujui kuwa biblia ilitengenezwa na hao wa roma na ndo kanisa la kwanza sasa iweje usiwaamini roma wakati unaamini biblia waliyo tengeneza

biblia zinazotumika sasa ni product ya ENGLISH REVOLUTION as commanded by King James I,kwahiyo kilichofanyika ni kuzitafsiri toka kiyunani na kilatini mpaka kiingereza na hatimaye kiswahili(KING JAMES VERSION) KIPINDI CHA RENAISSANCE 15TH CENTURY.
 
Mimi nilimsikia Leonado Da Vinci kwa mara ya kwanza nikiwa darasa la 4 toka kwa class mate aliyeitwa Peter Bakilana (RIP), alimtaja Da Vinci akitutambulisha picha yake ya Mona Lisa ndio ilikuwa the most expensive painting of all the time mpaka kesho!. Kwa sasa haiuziki tena, inasemekana its value ni priceless!. Tangu hapo nikilisikia tuu jina la Leonado Da Vinci, namkumbuka Peter Bakilana.

Nilimuuliza ni nini kinachoifanya picha iwe ghali kiasi hicho?, Peter akajibu ni ubunifu uliowekwa na mchoraji wakati akichora, akamuelezea Da Vinci kuwa ni Genius!. Akanionyesha hiyo picha ya Mona Lisa, na nyingine mbili za Madonna na Last Supper, akaniambia niziangalie nione ninaona nini!. Mimi niliziangalia nikamwambia naona picha tuu sioni kingine chochote!. Ndipo Peter akaniambia ili uweze kuona zaidi ya hicho unachokiona, lazima kwanza uwe na uwezo wa kuona zaidi ya kuona tuu, akaanza kuielezea picha ya the Last Supper, kuwa kati ya wale mitume 12 wa Yesu, mmoja alikuwa ni Mwanamke ila alivaa nguo za kiume wakati woite na watu hawakumtambua hata mara moja na mwanamke huyo alikuwa jirani na Yesu wakati wote!. Siku ya kutezwa kwake, alimuachia Kitambaa chenye picha yake!.

Da Vinci alipochora Madonna alimaanisha ni Bikira Maria, na alipoichora Mona Lisa, ambayo ndio picha yake ya mwisho kabla hajafa, alianza kuichora mwaka 1503 na kuikamilisha mwaka 1519, alitumia miaka 15 kuichora na kikubwa alkichokuwa anakifanya ni kuficha hizo secret codes!, alimchora huyo Mwanamke with coded lines ukiitazama sana itamuona Yesu ndani yake!. Mimi nilitazama sana sikuona kitu kwa vile sikujaaliwa huo uwezo wa kuona zaidi ya kuona.

Tangu pale nikadevelop interest na Leonado Da Vinci na mambo ya paintings hadi kuwajua kina Va Gogh, Pablo Picasso Michelengelo na wengine. Inasemekana kwenye michoro yake ameweka secret codes zenye siri ya Yesu!.
Mfano hebu soma hii hapa

  • Leonardo was a member of the Priory of Sion and knew the secret of the Grail. The secret is in fact revealed in The Last Supper, in which no actual chalice is present at the table. The figure seated next to Christ is not a man, but a woman, his wife Mary Magdalene. Most reproductions of the work are from a later alteration that obscured her obvious female characteristics.
  • The androgyny of the Mona Lisa reflects the sacred union of male and female implied in the holy union of Jesus and Mary Magdalene. Such parity between the cosmic forces of masculine and feminine has long been a deep threat to the established power of the Church. The name Mona Lisa is actually an anagram for "Amon L'Isa", referring to the father and mother gods of Ancient Egyptian religion (namely Amun and Isis).
Pasco.
 
[/B]

..........ile aya katika Biblia inayosema kuwa 'kila mtu atabeba furushi lake mwenyewe' ina maana gani ??:A S-confused1:

ikiwa Bwana Yesu amebeba dhambi za watu wake, huwa Kanisani mnatubu dhambi zipi ambazo Yesu hakuzibeba !???:shocked:

"If anyone would come after me, he must deny himself and take up his cross daily and follow me" (Luke 9:23).

But Jesus meant something far deeper when He told His disciples to carry their cross. He said to them, In Jesus' day, a cross wasn't just a symbol of pain and suffering; it was mainly a symbol of death. What Jesus was telling them is that they needed to put to death their own plans and desires, and then turn their lives over to Him and do His will every day.

You see, Jesus doesn't simply call us to believe that He existed, or even to believe that He can save us. He calls on us to commit our whole lives to Him—to trust Him alone for our salvation, and then to follow Him as His disciples. He said, "Anyone who does not carry his cross and follow me cannot be my disciple" (Luke 14:27).
 
majibu yako ya post #164 na # 165 ndio limmekuja suali hili


kama hutaki kujibu ndio au sio si lazima

Sijaona mahusiano kati ya nilichoandika huko na maswali yako
Toa ufafanuzi upewe majibu

Sitaki kujibu nisichokijua!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom