Madai kwamba Yesu kristo hakufa msalabani hayajaanza leo
siku ya tatu ya kufufuka kwake ndipo yalipobuniwa na tangu hapo karne na karne yamekuwa hivyo.
Wanaokataa kifufuka kwa kristo Yesu ,Mt.Yohana katika nyaraka zake amewaita hao ndio wapinga kristo.
Pia kwa baadhi ya imani kukiri kwamba Yesu kristo alifufuka ni SAWA na kukiri kwamba MAUTI ilishindwa kwa kristo Yesu. Uelewe kuwa NGUVU ya mauti ni kifo. Ushindi wa Yesu juu ya mauti na kuzimu ndilo pigo kuu ambalo linamkera mkuu wa giza.
Aidha, hamwezi elewana juu ya mada hii hiyo.Ninyi mnaongea lugha mbili tofauti.Mmoja anazungumza kwa jicho la kiroho,maana imeandikwa mambo haya yafahamika kwa namna ya rohoni; mwingine anaongea mambo hayo hayo akiongea kimwili hapo KATU hamtakaa mkaelewana.Maana hata peponi penu panatofautiana.Wakati hawa wengine pepo yao itawabidi wavikwe miili mipya,hawataowa wala kuolewa,maana watafanana na malaika; hawa wengine wameambiwa pepo yao iko chini katikati ya miguu ya wanawake.
Neema ya kristo iingilie kati tu.
HILI ULILOLIANDIKA NI KAMA ULIKULA TAMBUU YA KIBANIANI NA KUMWAGA MAPOVU YA CHOKAA, KWANI HUJAWEKA USHAHIDI WA KITABU CHOCHOTE WALA AYA YOYOTE YA BIBLIA
MAOMBI YALIKUBALIWA
Bwana Yesu Kristo wakati alikamatwa na Mayahudi na alikaribia kuteswa katika mikono ya watu, alimwomba Mungu sana.
Alianguka mbele Yake,alimkumbusha ahadi yake na alilia kuomba msaada
wa Mwenyezi Mungu.
Biblia inasema kwamba:
Yesu alienda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi akaomba akisema; Baba yangu ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke walakini si kama nitakavyo mimi bali kama utakavyo wewe. (Mathayo 26:39).
Bwana Yesu Kristo alikuwa na yakini kwamba maombi yake yamekubaliwa na ndiyo maana alipoona hali imekuwa mbaya zaidi hata kinyume cha matarajio yake, akashangaa kwa kusema "Eloi, Eloi, Lama Sabakthani? Yaani Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniwacha? (Mathayo 27:46 na Marko 15:34).
Alilia hivyo kwa sababu Bwana Yesu alikuwa na yakini ya kukubaliwa maombi yake na ya kupata msaada wa Mwenyezi Mungu. Kwa sababu Mwenyezi Mungu hukubali maombi ya waja wake, na Biblia inashuhudia kwamba maombi ya Bwana Yesu yalikubaliwa, inasema kwamba:
"Yeye katika siku hizo za mwili wake alimtolea yule aliyeweza kumuokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na mchozi akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu. (Waebrania 5:7).
Mwenyezi Mungu mwenye uwezo wa kumuokoa na kuwasalimisha watu, alimwokoa Bwana Yesu pia
kutoka kifo cha laana, kikombe cha mauti.
Na baada ya kukubaliwa maombi Bwana Yesu alimshukuru sana Mungu wake, "akasema Baba nakushukuru kwa kuwa umenisikia nami nilijua ya kuwa wewe wanisikia siku zote. (Yohana 11:41-42).
Sasa wakati Biblia inatangaza kwamba Bwana Yesu alimuomba Mungu kuondolewa kikombe na kifo cha msalaba, Mwenyezi Mungu alikubali maombi yake.
Lakini leo wapo baadhi ya wapinzani wa Yesu ambao wanasema kwamba Mwenyezi Mungu hakujali maombi na machozi ya Yesu wala hakumsaidia kumsalimisha kutoka hila za Mayahudi.
Na kikundi hiki cha Mapadri hata hawajali kufuta na kubadilisha aya za Biblia, ili waweze kutimiza matamanio na malengo yao.
Hata wanasahau kwamba kwa njia hii wanamfedhehesha Bwana Yesu na wanamtenganisha na Mwenyezi Mungu.
Lakini sisi Waislamu tunaamini kwamba Bwana Yesu alikuwa mpendwa wa Mwenyezi Mungu na alikubaliwa maombi yake.
YESU ALIKUWA HAI
Wakati wa kuondoka kutoka chumba kile alituma ujumbe kwamba wanafunzi wake wamkute Galilaya. (Mathayo 38:7 na Marko 16:7).
Baada ya kupata ujumbe huu wanafunzi wote walifika Galilaya. Baadhi yao walidhani kwamba Yesu ameshafariki tayari.
Katika somo hili Biblia inasema kwamba:
"Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu.
Wakashituka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona Roho. Akawaambia mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu? Tazama mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikeni-shikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo. Na baada ya kusema hayo aliwaonyesha mikono yake na miguu yake. Basi walipokuwa hawajaamini kwa majeraha, huku wakistaajabu, aliwaambia mna chakula chochote hapa? Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa. Akakitwaa, akala mbele yao. (Luka 24:36-43).
Tena Biblia inaondoa shaka ya kwamba Yesu hakufia msalabani bali aliendelea na uhai wake baadaye na aliendelea kukutana na wanafunzi wake.
Biblia inasema:
"Naye akiisha kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwana. Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; Kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi.
(Yohana 20:20-21).
Bwana Tomaso bado alidhani kwamba huyu siyo Yesu bali ni Roho yake. Bwana Yesu aliondoa hata shaka yake pia.
Biblia inasema kwamba:
"Basi wanafunzi wengine wakamwambia, tumemuona Bwana. Akawaambia, nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo. Basi, baada ya siku nne, wanafunzi wake walikutana ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu na milango imefungwa,
akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu. Kisha akamwambia Tomaso, lete hapa kidole chako; uitizame mikono yangu. Ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu, wala usiwe asiye amini bali aaminiaye. (Yohana 20:26-27).
Kwa njia hizi zote Bwana Yesu alithibitisha kwamba tangazo lile la kifo na kuuawa kwake lilikuwa la uwongo.
Yeye hakufia msalabani.
Alisalimika .
Sasa kabla ya kumaliza somo hili naomba usome andiko hili. Biblia inasema:
" Basi, ikiwa Kristo anahubiriwa ya kwamba amefufuka katika wafu,mbona baadhi yenu husema kwamba hakuna kiyama ya wafu? Lakini kama hakuna kiyama ya wafu, Kristo naye hakufufuka; tena kama Kiristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure. Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi. Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka. Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu. Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea. Kama katika maisha haya tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote" (1Wakorintho 15:12-19).
Katika aya hizi imeelezwa kwamba kama watu hawatafufuka, Bwana Yesu pia hatafufuka. Na sote tunajua kwamba wafu watafufuka katika Akhera wala siyo katika dunia hii. Hivyo ndivyo Bwana Yesu pia atafufuka katika Akhera wala siyo katika dunia hii.
Biblia inasema kwamba: "Wafu hawawezi kurejea duniani." (Ayubu 7:9).
na kama Kristo hakufufuka , basi imani yenu ni bure. Mngalimo katika dhambi zenu.
Yaani hakuna faida yoyote kuamini kifo cha laana na kufufuka kwake.
Habari ya tatu imeelezwa kwamba waliolala katika Kristo wamepotea.
Na ya nne, hao ni maskini kuliko watu wote.
Enyi ndugu Wakristo, sisi tunawapendeni msife mioyo. Hamna kosa bali hamkujua. Basi sasa jiungeni na dini ya Kiislam. Karibuni sana, Dini ya Kiislam itawapatieni kila heshima. Na hiyo ni njia moja ya kusalimika, Muda wa kutosha mmeupoteza tayari.
Harakisheni kueleka kwenye njia iliyonyooka, Dini ya Mwenyezi Mungu yaani ISLAM.
Karibuni sana.