minyoo
JF-Expert Member
- May 25, 2013
- 21,640
- 20,366
DPP kabla ya kuwa DPP hakuwa na kitu alikuwa masikini mtu wa kawaida tu, lakini mpaka sasa kawa Tajiri mkubwa kama Naibu Rais Daud Bashite. Achunguzwe mali zake wananchi ingieni kazi mtoe taarifa za mali zake hata kama kaandika majina ya ndugu jamaa marafiki.Hii ndiyo awamu ya kwanza kumuona DPP akiongea na vyombo vya habari kama mwanasiasa. Watanzania hatukuzoea. Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema ametusemea watu wengi tulioumizwa na DPP Biswalo Mganga. Hakika Mungu atamlinda Godbless Lema dhidi ya hila zote za kishetani. Hapa nawakumbusha tu baadhi ya uovu ambao DPP Biswalo Mganga ameufanya kwa makusudi au kwa kutumika na anayemtuma;
1. Kwenye Plea bargaining wanafanya dhuluma ya wazi wazi kwa kuchukua fedha kwa watu ambao wamewakamata bila ushahidi. Watu wanasota miaka mitatu rumande kwa kisingizio upelelezi haujakamilika, then wanaambiwa waombe msamaha ili waingie plea bargain. Kimsingi Plea bargain inapaswa ifanyike na kusimamiwa na Mahakama, lakini hapa Tanzania inasimamiwa na DPP. Plea bargain ni mradi wa kujipatia fedha binafsi kati ya Jiwe na Biswalo Mganga. Kuna fedha ambayo wanaingiza Serikalini kwenye akaunti ya Plea bargain lakini kuna fedha zingine wanachukua wao binafsi ambazo hazina rekodi lakini mtuhumiwa anaambiwa atoe ili aaweze kuwa eligible.
2. Aliwaachia askari waliomuua Akwilina wa DIT na akawafungulia Mashtaka viongozi 9 wa CHADEMA ambao last week walichangiwa hela na wananchi ili wasifungwe miezi 5 jela.
3. Amewabambikia kesi akina Eric Kabendera, Tito Magoti na wenzie kwa kuwapa kesi ya kutakatisha hela ingawa kwa sabau tu ya kuikosoa Serikali
Tuombe Mungu atupe uhai, awamu inayokuja namuona Biswalo Mganga naye akipelekwa Mahakamani kama anavyopeleka wenzie pamoja na Kamanda Lazaro Mambosasa.