LATRA: Mabasi 759 yanayofanya safari za Usiku yanazidisha Speed na kuchezea mfumo wa ufuatiliaji taarifa za gari (VTS)

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,119
Mwezi mmoja tangu Serikali iruhusu safari za mabasi kwa saa 24, tathimini ya mamlaka za usimamizi imeonyesha kuwepo ukiukwaji mkubwa wa sheria na kanuni za usalama barabarani, hali inayohatarisha usalama kwa abiria na mali zao.

Kutokana na ukiukwaji huo, ndani ya muda huo mabasi 759 yamekamatwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (Latra) kwa kushirikiana na Kikosi cha Usalama Barabarani kwa kuzidisha mwendo na kuchezea mfumo wa VTS unaodhibiti na kutoa taarifa za kasi ya gari.

Taarifa ya pamoja iliyotolewa jana na Mkurugenzi Mkuu wa Latra, Habibu Suluo na Kamanda wa Trafiki, Ramadhan Ng’anzi ilieleza kati ya mabasi hayo, 723 yalipewa onyo na mengine kusitishiwa leseni.

“Mabasi yaliyositishiwa leseni mpaka mamlaka itakapojiridhisha kwamba wamebadilika ni 36.

“Kati ya mabasi 246, asilimia 80 (mabasi 197) yamebainika yanaendeshwa kwa mwendo kasi kati ya kilomita 86 hadi 89 kwa saa, huku asilimia tisa yakiendeshwa kwa kilomita 90 hadi 103 kwa saa,” ilisema.

Madereva waliofungiwa
20231111_082936.jpg
20231111_082938.jpg
20231111_082941.jpg

20231111_082939.jpg


Orodha ya Mabasi yaliyofungiwa
20231111_082929.jpg
20231111_082931.jpg
 
Kati ya mabasi 246, asilimia 80 (mabasi 197) yamebainika yanaendeshwa kwa mwendo kasi kati ya kilomita 86 hadi 89 kwa saa, huku asilimia tisa yakiendeshwa kwa kilomita 90 hadi 103 kwa saa,” ilisema.
Wameona biashara zao zinakufa wameanza visingizio! I hate it, nchi ya ajabu sana hii, uendeshe speed 80 usiku si utasinzia? Au wanataka tufe wafurahi?
 
Sioni Logic ya kuendesha speed 80 usiku, LAZIMA tukubali kubadilika, at least wazungumzie speed 100 sio 80. Mabasi yote ya usiku ni mapya na ni mazima, usiku hakuna kelele nyingi, iweje tuendelee kushikilia Sheria za kipumbavu? Mwanzoni walisema usiku kutakua na ajali nyingine, MUNGU kawaumbua Sasa wanakuja na ujinga mwingine
 
Sikuelewi kabisa! Kwamba ni speed ndogo? Kwamba ukiendesha kwa speed kubwa biashara za viongozi zitakufa hivyo wanalazimisha speed iwe 80?
Hayo machadomo akili zao ni finyu sana 🤣🤣🤣🤣🤣

Inahitaji kuwa mpumbavu ndio uwaelewe. Akili zao zinakosa consistency na utulivu Kwa sababu wamejaa chuki.
 
Tulipiga kelele sana hapa JF, eti ilikua ikifika jioni huwezi kusafiri, Nchi nzima mnalala! Saa hizi unatoka Dar to Arusha saa tatu usiku, Dar Mwanza saa mbilli usiku, saa nne usiku, saa saba na saa Tisa usiku

Hakika kwa hili maendeleo yataenda kwa kasi,kilio changu ni upanuzi wa barabara ili kupunguza ajali amana barabara zetu hasa high ways ni finyu sana.
 
Sioni Logic ya kuendesha speed 80 usiku, LAZIMA tukubali kubadilika, at least wazungumzie speed 100 sio 80. Mabasi yote ya usiku ni mapya na ni mazima, usiku hakuna kelele nyingi, iweje tuendelee kushikilia Sheria za kipumbavu? Mwanzoni walisema usiku kutakua na ajali nyingine, MUNGU kawaumbua Sasa wanakuja na ujinga mwingine
Una matatizo makubwa sana kwenye hili jambo. Magari yakiwa mapya ndiyo hayapati ajali yanapoendeshwa kwa kasi? Unajua factors zinachangia ajali ya usiku? Unajua tofauti ya gari lililo kwenye mwendo mkali linapopata ajali na lililo kwenye mwendo wa kawaida?
 
Sikuelewi kabisa! Kwamba ni speed ndogo? Kwamba ukiendesha kwa speed kubwa biashara za viongozi zitakufa hivyo wanalazimisha speed iwe 80?
Tulia usome Tena Mpwa, biashara zinakufa Kwa kua wengi tulikua tunalazimika Kulala njiani ambako kuna biashara zao mfano pale Kahama, Tabora, Kaliua etc

Speed 80 Kwa usiku ambako hakuna mwenda Kwa miguu, hakuna Wanafunzi, magari ni machache, barabara zinapitika na nyingi zina alama ambazo ni reflective Kuna Sababu Gani ya kukufanya utembee speed 80 wakati unaenda Bukoba??
 
Una matatizo makubwa sana kwenye hili jambo. Magari yakiwa mapya ndiyo hayapati ajali yanapoendeshwa kwa kasi? Unajua factors zinachangia ajali ya usiku? Unajua tofauti ya gari lililo kwenye mwendo mkali linapopata ajali na lililo kwenye mwendo wa kawaida?
Bahati nzuri unaongea na MTU ambaye nasafiri Kila wakati, najua ninachoongea! Labda kama unahitaji tu tubishane which I am not ready for that!
 
Hakika kwa hili maendeleo yataenda kwa kasi,kilio changu ni upanuzi wa barabara ili kupunguza ajali amana barabara zetu hasa high ways ni finyu sana.
Hili ndio la msingi! Na kuweka sehemu za parking za dharura hasa Kwa Malory na kuongeza huduma ya breakdown Ili ikitokea shida lory liondolewe haraka
 
Uongo uo mmeona hesabu haziji hamkai loud usiku mnakaa nawake zenu na usiku toch hakuna mabosi wa mabasi wote wamekaza wanatembea usiku mnahisi mtakufa njaa zamani tuliwahisi mabosi wa hakuna kulala ndo wanazuia izi route kumbe ni nyie
 
Tulia usome Tena Mpwa, biashara zinakufa Kwa kua wengi tulikua tunalazimika Kulala njiani ambako kuna biashara zao mfano pale Kahama, Tabora, Kaliua etc

Speed 80 Kwa usiku ambako hakuna mwenda Kwa miguu, hakuna Wanafunzi, magari ni machache, barabara zinapitika na nyingi zina alama ambazo ni reflective Kuna Sababu Gani ya kukufanya utembee speed 80 wakati unaenda Bukoba??
Speed 80 kwa barabara zetu usiku ni reasonable kabisa. Hii ni kwa sababu barabara zetu ni nyembamba na hazina ubora. Ukitembelea 100 na ikitokea ajali inakuwa fatal.
 
Back
Top Bottom