Ladha ya maisha unaipata kwenye nini?

Ladha ya maisha unaipata kwenye nini?

Swali lako Lina maana sana lakini majibu Sasa ,Ni kama Kuna mashindano ya kuchekeshana. Kumbukeni kuwa serious.
 
Swali lako Lina maana sana lakini majibu Sasa ,Ni kama Kuna mashindano ya kuchekeshana. Kumbukeni kuwa serious.
Watu wa JF ndivyo walivyo hakuna kitu nimeandika mpka mtu akashindwa kuelewa kabisa

Mimi nachulia watu wa sample hiyo kama watu wasio na hoja

Na hainisumbui kabisa
 
AFYA NI MTAJI NO 1.
KUNA KIPINDI NILIKUWA NA MAMILIONI LAKINI SINA AFYA DAHHHHH!!!!!!
Hapo hapo kuna majamaa wanenda kwa waganga kumpa jogoo punje za mahindi wagawane miaka na umasikini. So ukisema ladha ya maisha ni uzima wakati mtu jogoo kala punje 10. Sijui inakuwaje. Nafkiri hili la afya kuwa ladha ya maisha si la wote.
 
Watu wa JF ndivyo walivyo hakuna kitu nimeandika mpka mtu akashindwa kuelewa kabisa

Mimi nachulia watu wa sample hiyo kama watu wasio na hoja

Na hainisumbui kabisa
Vizuri. Hakika focus na watu makini. Hilo swali lako ni zuri sana,kwanini ,kwa sababu maisha ni kama Game na kila mtu anacheza hili game.Kanuni ya hili Game ni kwamba hata ukishinda unakufa. Hakuna atayebaki kuwa hai ndani ya hili game.

Mfano unaweza kupambana ndoto zako,labda uwa tajiri au Raisi ,ukashinda na kufikia ndoto hizo.Lakini utakufa .

Kwa hiyo kikubwa si kushinda Bali ni kufurahia hili Game. Kwa hiyo swali lako kuhusu ladha ya maisha hakika Lina maana sana.
 
Hapo hapo kuna majamaa wanenda kwa waganga kumpa jogoo punje za mahindi wagawane miaka na umasikini. So ukisema ladha ya maisha ni uzima wakati mtu jogoo kala punje 10. Sijui inakuwaje. Nafkiri hili la afya kuwa ladha ya maisha si la wote.
Huu utajiri wa kuku hivi hua kweli🤔
 
Back
Top Bottom