Laana ya vifaranga: Tutarajie mapigo kama mafuriko, ukame, njaa, tetemeko, n.k kama sio wahusika wenyewe kupata pigo la moja kwa moja

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,023
144,381
Vyovyoyte itavyokuwa, wafanya maamuzi wetu hawawezi kukwepa lawama kwa vifaranga waliopoteza maisha na kwakuwa hii ni dhambi mbaya, lazima tutaadhibiwa kama nchi au wahiusika wenyewe ndio wataadhibiwa na NATURE moja kwa moja.

Viumbe wale hawakuwa na kosa lolote na kilio chao hakiwezi kwenda bure, na hivyo tujiandae kulipa gharama za dhambi ilioyofanyika. Tutaadhibiwa kama nchi au wahusika wenyewe ndio watakaodhibiwa moja kwa moja kutokana na maamuzi waliyoyafanya.

Nature inaweza kutushushia pigo lolote na mapigo ya aina hii yanaweza kuwa ni ukame, njaa, tetemoka au majanga mengine ya asili na tusielewe kuwa chanzo ni laana ya viumbe hawa.

kuna pigo la moja kwa moja linaweza kuwatokea wafanya maamuzi, pigo ambalo nikilitaja au kulifafanua, uzi unaweza kuondolewa hivyo sitasema chochote kuhusu hilo pigo ila kila mwenye akili mpaka hapa atakuwa ameelewa.

Sometimes Mataifa kama US hukumbwa na majanga ya asili kama vimbunga, n.k, sababu inaweza kuwa ni matokeo ya watawala katika nchi zao kuvamia nchi nyingine kwa visingizio mbalimbali na kuua watu wasio na hatia na kuwaacha wengine na vilema vya kudumu.

Laana sio ya paka tu bali hata viumbe wengine wana laana mbaya.

Muda utaongea.
 
Huu uliandikwa hapa ni ujinga wa kwanza kabisa wa Mwaka 2023. Maisha ya binadamu ni ghali na ya thamani sana kuliko kuliko ya kiumbe kingine chochote na lolote linalofanywa ni kwa nia ya kumkinga binadamu dhidi ya hatari zozote. Kama vifaranga hivyo vilikuwa na magonjwa au aina nyingine ya viashiria vya hatari kuviua ni salama kabisa kwa maisha ya binadamu.

Pengine tutakuwa tumesahahu madhira yaliyoikumba dunia kutoka na madhira ya ndege ambao walikuwa chanzo Cha Corona.
 
Wanao takiwa kupata laana ni wale walio agiza vifaranga bila kufata utaratibu huku wakijua fika kwamba serikali ilishaweka zuio la kuingiza vifaranga nchini ambapo utekerezaji wake ulianza kufanya kazi mwezi wa sita mwaka jana

Na ndio sababu kubwa ya wao kukosa vibali kutoka sehemu husika pamoja na kuwasilisha maombi hayo

Sheria zimewekwa tuzifuate...

Yule mama pale moshi kachoma vifaranga vyake sababu anazo zisema ni kukosa soko, nae sijui tumchukulie hatua? Au ndio ana sababisha ukame, mafuliko, laana nk kuongezeka??
 
Huu uliandikwa hapa ni ujinga wa kwanza kabisa wa Mwaka 2023. Maisha ya binadamu ni ghali na ya thamani sana kuliko kuliko ya kiumbe kingine chochote na lolote linalofanywa ni kwa nia ya kumkinga binadamu dhidi ya hatari zozote. Kama vifaranga hivyo vilikuwa na magonjwa au aina nyingine ya viashiria vya hatari kuviua ni salama kabisa kwa maisha ya binadamu.

Pengine tutakuwa tumesahahu madhira yaliyoikumba dunia kutoka na madhira ya ndege ambao walikuwa chanzo Cha Corona.
Binadamu huwa tunajiona ni bora kuliko viumbe wengine na hudhani tuna haki mbele za Mungu kuliko viumbe wengine ambao na wameumbwa na Mungu. Si kweli hata kidogo na haya ni matokeo ya kutafsri vibaya maandiko matakatifu.
 
Vyovyoyte itavyokuwa, wafanya maamuzi wetu hawawezi kukwepa lawama kwa vifaranga waliopoteza maisha na kwakuwa hii ni dhambi mbaya...
BUSARA Ilipaswa itumike hata kuvigawa BURE Vifaranga kwa WAFUGAJI wa KUKU badala ya Kusababidha Vifo vya VIFARANGA
 
Binadamu huwa tunajiona ni bora kuliko viumbe wengine na hudhani tuna haki mbele za Mungu kuliko viumbe wengine ambao na wameumbwa na Mungu. Si kweli hata kidogo na haya ni matokeo ya kutafsri vibaya maandiko matakatifu.
Wanachukulia haya mambo kirahisi sana mkuu, kwamba hao ni vifaranga tu si chochote si lolote......
 
Na wanaokula nyama choma je kila siku? Vipi Wachaga wanaochinja Mbuzi na wanakunywa mpaka Damu wanaita kisusio? Hao laana haiwahusu ?
 
Wanao takiwa kupata laana ni wale walio agiza vifaranga bila kufata utaratibu huku wakijua fika kwamba serikali ilishaweka zuio la kuingiza vifaranga nchini ambapo utekerezaji wake ulianza kufanya kazi mwezi wa sita mwaka jana

Na ndio sababu kubwa ya wao kukosa vibali kutoka sehemu husika pamoja na kuwasilisha maombi hayo

Sheria zimewekwa tuzifuate...

Yule mama pale moshi kachoma vifaranga vyake sababu anazo zisema ni kukosa soko, nae sijui tumchukulie hatua? Au ndio ana sababisha ukame, mafuliko, laana nk kuongezeka??
Aliye mnanga Magu kuchoma vifaranga naye amezuia vifaranga store Hadi kufa,. Ngoma ni 0-0 had sasa.
 
Vyovyoyte itavyokuwa, wafanya maamuzi wetu hawawezi kukwepa lawama kwa vifaranga waliopoteza maisha na kwakuwa hii ni dhambi mbaya, lazima tutaadhibiwa kama nchi au wahiusika wenyewe ndio wataadhibiwa na NATURE moja kwa moja.

Viumbe wale hawakuwa na kosa lolote na kilio chao hakiwezi kwenda bure, na hivyo tujiandae kulipa gharama za dhambi ilioyofanyika. Tutaadhibiwa kama nchi au wahusika wenyewe ndio watakaodhibiwa moja kwa moja kutokana na maamuzi waliyoyafanya.

Nature inaweza kutushushia pigo lolote na mapigo ya aina hii yanaweza kuwa ni ukame, njaa, tetemoka au majanga mengine ya asili na tusielewe kuwa chanzo ni laana ya viumbe hawa.

kuna pigo la moja kwa moja linaweza kuwatokea wafanya maamuzi, pigo ambalo nikilitaja au kulifafanua, uzi unaweza kuondolewa hivyo sitasema chochote kuhusu hilo pigo ila kila mwenye akili mpaka hapa atakuwa ameelewa.

Sometimes Mataifa kama US hukumbwa na majanga ya asili kama vimbunga, n.k, sababu inaweza kuwa ni matokeo ya watawala katika nchi zao kuvamia nchi nyingine kwa visingizio mbalimbali na kuua watu wasio na hatia na kuwaacha wengine na vilema vya kudumu.

Laana sio ya paka tu bali hata viumbe wengine wana laana mbaya.

Muda utaongea.
Tumekusikia ila jua sheria iliwekwa Ili tuwe na utaratibu wa kufanya mambo yetu mbona waethiopia wanakufa sana huji na porojo kama izi hizo ni hisia zako tu we unafanya makosa mangapi je MUNGU amekupa adhabu gani acheni kutisha watu na mambo ya kufikirika we unataka tuishi bila kuheshimu sheria je hao marekani na majanga Yao we umewazidi nn
 
Back
Top Bottom