Kwenye msitu wangu kuna black mamba/ koboko natafuta njia za kumwangamiza bila kuleta madhara kwenye jamii

watamalizwa na wakulima huwa wanakula karanga wale
Hapana nguchiro (mangoose) Hali karanga ni carnivore!
Ziko species ambazo ni omnivores zinachanganya Milo kama banded mangoose lakini hazili karanga nzima nzima kama rodents hao labda uwape peanut butter
Ila slender mangoose ni pure meat feeder anawinda NYoka,mijusi,panzi,kuku nk
 
Ndio mkuu wanapenda jua sana nahisi hivyo maana wanapenda juu kabisa
Wanaopenda juu ya miti ni green mamba ambao huwinda ndege sana black mamba hupendelea zaidi chini!

Na akiteleza huteleza haswa anapenda sana wanyama wadogo wadogo mfano wa panya na mijusi aina zote
Ukimkuta mtini ujue amekusa mlo chini kaamua kutafuta viota vya ndege!!
 
Wanaopenda juu ya miti ni green mamba ambao huwinda ndege sana black mamba hupendelea zaidi chini!

Na akiteleza huteleza haswa anapenda sana wanyama wadogo wadogo mfano wa panya na mijusi aina zote
Ukimkuta mtini ujue amekusa mlo chini kaamua kutafuta viota vya ndege!!
Mkuu wewe unaelewa sana na wajuu kuhusu Hawa viumbe
 
Hapana nguchiro (mangoose) Hali karanga ni carnivore!
Ziko species ambazo ni omnivores zinachanganya Milo kama banded mangoose lakini hazili karanga nzima nzima kama rodents hao labda uwape peanut butter
Ila slender mangoose ni pure meat feeder anawinda NYoka,mijusi,panzi,kuku nk
Nimesoma Wikipedia hapa ni vile vile ulivyosema wewe. Miaka ya nyuma walikuwa wengi sana lakn Cha ajabu walikuwa wanashambiliwa sana na wanakijiji na walikuwa wanishi kwenye mashimo ya vichuguu basi wakikurupushwa kutoka mashambani mwenye shamba atawazimba Kwa kutumia miba nao hufa Kwa njaa Kwa sababu hawezi kutoka akitaka kutoka anachomwa na miba Hadi kufa.

Nimejaribu kuangalia kumbe hata vicheche ni jamii Moja na nguchiro mkuu nilkuwa sijui na nilijua kuwa kicheche yeye anakula nyama na wadudu tu. Ahsantee sana

Hawa ndo kwetu walikuwapo Kwa wingi sasahivi wameshatoweka kabisa
 

Attachments

  • Screenshot_20240327-204106.jpg
    Screenshot_20240327-204106.jpg
    359.9 KB · Views: 3
Nimesoma Wikipedia hapa ni vile vile ulivyosema wewe. Miaka ya nyuma walikuwa wengi sana lakn Cha ajabu walikuwa wanashambiliwa sana na wanakijiji na walikuwa wanishi kwenye mashimo ya vichuguu basi wakikurupushwa kutoka mashambani mwenye shamba atawazimba Kwa kutumia miba nao hufa Kwa njaa Kwa sababu hawezi kutoka akitaka kutoka anachomwa na miba Hadi kufa.

Nimejaribu kuangalia kumbe hata vicheche ni jamii Moja na nguchiro mkuu nilkuwa sijui na nilijua kuwa kicheche yeye anakula nyama na wadudu tu. Ahsantee sana

Hawa ndo kwetu walikuwapo Kwa wingi sasahivi wameshatoweka kabisa
Sahihi!
Wanakijiji waliwaua kwa sababu wanashambulia kuku na vifaranga!
Na hata kwenye hivyo vichuguu ambavyo huishi humo ni vichuguu vilivyokufa either kwa kuvamiwa na siafu au wanyama wanaokula mchwa kama vile muhanga na nunguri!
Hawana uwezo wa kuchimba kama mole rats ndio maana walivyowekewa miba wakashindwa ku plan B kutoka nje
 
Sahihi!
Wanakijiji waliwaua kwa sababu wanashambulia kuku na vifaranga!
Na hata kwenye hivyo vichuguu ambavyo huishi humo ni vichuguu vilivyokufa either kwa kuvamiwa na siafu au wanyama wanaokula mchwa kama vile muhanga na nunguri!
Hawana uwezo wa kuchimba kama mole rats ndio maana walivyowekewa miba wakashindwa ku plan B kutoka nje
Uhakika
 
Mi ushauri ninaokupa ondoa hofu NYoka wako Kila mahali na bila uwepo wao ikolojia itakufa NYoka hawana shida na binadamu ila binadamu ndio muharibifu
Hapo kwenye pori lako endeleza mradi wako,NYoka wanakuona na kukuhisi kabla haujatokeza ukianza pilikapilika hapo watasepa kutafuta sehemu tulivu!
Hapa ninapokaa Kuna brown house snakes zaidi ya ishirini na huwa ikifika jioni nawaona wakitoka chini ya mawe kuwinda Mende,panya nk na Mimi na wao hatuna ugomvi isipokua niwakute ndani kwangu ndio nitaua
 
Mi ushauri ninaokupa ondoa hofu NYoka wako Kila mahali na bila uwepo wao ikolojia itakufa NYoka hawana shida na binadamu ila binadamu ndio muharibifu
Hapo kwenye pori lako endeleza mradi wako,NYoka wanakuona na kukuhisi kabla haujatokeza ukianza pilikapilika hapo watasepa kutafuta sehemu tulivu!
Hapa ninapokaa Kuna brown house snakes zaidi ya ishirini na huwa ikifika jioni nawaona wakitoka chini ya mawe kuwinda Mende,panya nk na Mimi na wao hatuna ugomvi isipokua niwakute ndani kwangu ndio nitaua
Sawa mkuu naishi na ushauri wako
 
Jf salaam

Ni muda sasa tangu aanze kuonekana huyu nyoka hatari koboko na inasemekana wapo wawili.

Taarifa zilianza kunifikia kutoka Kwa wazee wangu maana huo msitu ukweli sio wangu ni wa mzee ila kaniruhusu kufanya shughuli zozote za kujiingizia kipato.

Mara kadhaa amekuwa akionekana na muda wa usiku kupiga kelele flani Hivi.

Nakumbuka baada ya kupata mapumziko mafupi nilienda kijijni kwa wazee wetu. Nikafika na nikaenda mlimani(msituni) lengo nikufanya research kwa kina Ili niwekeze ufugaji wa nyuki (asali).

Nilimchukua dogo mmoja ambae Huwa anachunga mbuzi wangu tukaenda naye huku akinifotoa picha za kila aina na Kila Rangi.

Mwisho tukafika kwenye mti mzuri wenye kijani kibichi wenye matawi mazuri akanipigia picha za kutosha pale.

Baada ya hapo tukakaa chini ya mti huo kwenye jiwe huku nikipitia picha nilizopigwa na kufuta zile sikuzipenda

Tukiwa hapo tunapiga story ghafla tukasikia kelele za ndenge flani juu ya mti Mimi kelele zile nazijua huwa ni Alert ya hatari fulani wameiona wale ndege.

Kuinua macho juu sikuamini nilichokiona ni yeye koboko mtesa ametulia tulii Wala hatikisikii kama amekufa.

Dogo(muha) kumuona akapanic akaanza mbio nikamwambia simama hapohapo akasimama huku nami nikitoka eneo la tukio hadi kwa dogo.


Nyoka ni mkubwa na anaogopesha na kwa mazingira yale huwezi mshambulia kwa kutumia njia zetu hizi za asili(fimbo)

Maana ni mstuni vinginevyo anakuua ndani ya muda mfupi tu hakuna sehemu ya ku escape asikudhuru.

KUMBUKUMBU ZANGU

Miaka ya nyuma tukiwa wadogo nilishuhudia maiti za Watoto wenzetu watu na ng'ombe 7 zikiwa zimelala Chali (kufa).

Ni baada ya Hawa Watoto kuona huyo nyoka aina ya koboko na kumshambulia ndipo alipowageuka na kuwauma wote wawili na ng'ombe zao zote Saba na zilikufa hapohapo!

Nakumbuka kipindi hicho hicho nikiwa primary mtoto mwingine darasa letu Moja akiwa anaenda kuokota maembe kwenye mti wa mwembe akamuona koboko Kasimama wima naye pasina kujua alianza kumshambulia.

Hapo hapo alimgonga na kufa mama yake alisikia kelele za mwanae akilia Kwa uchungu Kwa sababu ilikuwa mbali na mwembe na mara zote walikuwa wanaenda Watoto kadhaa kuokota maembe pale. ile anatoka akamsaidie alimkuta tiyari kashafariki na nyoka amepanda juu ya mtu flani mfupi.

Ndipo alipo piga yowe kuomba msaada na walifanikiwa kumuua.

Inavyosemekana na Mimi naweza kuwa shahidi wa hili ni kwamba....

Nyoka aina ya black mamba ni wapole kupita kiasi pale anapokuwa katika Hali yake ya kawaida.

Pia anasikia kuliko kawaida anaupeo mkubwa wa kuhisi hatari na hata harufu na hivyo kujiweka tiyari Kwa ajiri ya mapambano.

Akiona mazingira aliyopo sio salama kwakwe kufanya shambulio hujiondokea kabla hujamfikia Wala kumuona.

Lakini pale ukimuona wewe jua kakusubiri na amejiandaa Kwa muda mrefu sana amegojea tu ulianzishe upate unachostahili.

Kwa matukio hayo mawili ambayo siyo ya kusimuliwa na hili langu Mimi mwenyew Tena mwezi 2 tu mwka huu nakubaliana na hili kuwa Hawa nyoka ni wapole na ni hatari.

Tukio la wale watoto wawili na ng'ombe wao. Sisi ndo tulikuwa wa kwanza kumuona yule nyoka na ilikuwa Hivi.....

Siku Moja tunaenda machungani katikati ya njia kulikuwa na mti flan Hivi kama kichaka (ipo miti Ina randa na kutengeneza kichaka kizito)

Tulipitisha mifugo yetu yote salama na sisi wenyewe tukapita salama mtu wa4 ndo akatumbia oneni yule nyoka tukarudi kumtazama asee alikuwa mrefu sana na ametulia kama hajui kinachoendelea...

Tulichokifanya ni kwenda kuwambia wakubwa wetu karibu na eneo lenyewe. Na walipokuja wakamuona na kumtambua walitumbia ondoeni ng'ombe na mifugo yenu hapa tukafanya hivo.

Nao walipoona tumeondoka waliondoka pia bila kumfanya chochote.

Bahati mbaya sana Kwa wenzetu siku chache mbele wao walipo muona tu ujasiri uliwaingia na kuanza kumshambulia huo ndo ulikuwa mwisho wao na ng'ombe wao pia.

Yowe lilipigwa nyoka huyo akauliwa.

Nimekuja kuomba ama kufundishwa njia/mtego Ili nimuue bila kuathiri watu wa maeneo hayo.

Msitu huu nimepanga kufugia nyuki Kwa wingi lakni kinacho niogopesha ni uwepo wa black mamba kwenye eneo hili.

Eneo ni zuri sana Kwa nyuki kwani maji yapo si zaidi ya mita250 na nyuki ni wengi sana hasa kwenye mapango ya miti,mawe na wengine hujitengenezea asali juu ya mti tu.

Najua humu Kuna watu wa maliasili na wataalamu wa maswala haya naombeni namna ya kumuondoa huyu mdudu na nimeambiwa wapo wawili.

Wapo walio waona Kwa nyakati tofauti na maeneo tofauti na usiku hupiga kelele zao Kwa kupokezana wasi wasi wangu zaidi watazaliana na kuongezeka zaidi.

Ahsanteen sana.

View attachment 2945391
Kwani mkuu ukimuona let's say kwenye mti na ukazungushia petroli ukawasha eneo Hilo, huwezi mpata tena. Au unaweza chukua chumvi ukamwaga maeneo yake, maana chumvi huwa inamkata kata, au unaweza nunua oil chafu ukamwaga maeneo alipo, maana hawezi kuslide lazima tu akiona hyo Hali hakai ataondoka tu. Wapo wanaochukua uji wa Moto na sufuria juu then wanaenda alipo hasa kwa watu wa musoma na kisha wanaenda eneo na kuanza kumchokoza,akitoka juu ya mti huwa ni moja kwa moja kwenye sufuria la uji,hapo lazima afe
 
Kwani mkuu ukimuona let's say kwenye mti na ukazungushia petroli ukawasha eneo Hilo, huwezi mpata tena. Au unaweza chukua chumvi ukamwaga maeneo yake, maana chumvi huwa inamkata kata, au unaweza nunua oil chafu ukamwaga maeneo alipo, maana hawezi kuslide lazima tu akiona hyo Hali hakai ataondoka tu. Wapo wanaochukua uji wa Moto na sufuria juu then wanaenda alipo hasa kwa watu wa musoma na kisha wanaenda eneo na kuanza kumchokoza,akitoka juu ya mti huwa ni moja kwa moja kwenye sufuria la uji,hapo lazima afe
ushauri wako ni mgumu kuutekeleza mkuu. Daaah ni mgumu asee
 
Kwani mkuu ukimuona let's say kwenye mti na ukazungushia petroli ukawasha eneo Hilo, huwezi mpata tena. Au unaweza chukua chumvi ukamwaga maeneo yake, maana chumvi huwa inamkata kata, au unaweza nunua oil chafu ukamwaga maeneo alipo, maana hawezi kuslide lazima tu akiona hyo Hali hakai ataondoka tu. Wapo wanaochukua uji wa Moto na sufuria juu then wanaenda alipo hasa kwa watu wa musoma na kisha wanaenda eneo na kuanza kumchokoza,akitoka juu ya mti huwa ni moja kwa moja kwenye sufuria la uji,hapo lazima afe
Ushauri wa uji wa moto kubeba kichwani ni story kama za sungura na fisi! Koboko anagonga popote na vimeno vyake vidogo vya mbele(front fixed fang) anaweza rukia p*mbu,kidole,sikio,tumbo nk

Striking yake ni ya kudonoa kama kuku tofauti na boomslang au vine snakes(back fanged) ambao hung'ata
 
Back
Top Bottom