Kwao hawanitaki kisa mkurya.

Kwao hawanitaki kisa mkurya.

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,932
Reaction score
11,851
Jamani mimi ni kijana mwenye miaka 28 baada ya kumaliza masomo nimepata kazi hapa mjini, sasa nikaamua kutafuta mke ili nioe niache kumbwela mbwela nisije kufa kwa ngoma, nimepata mtoto wa kihehe wa kule mafinga tayari nimempeleka kwetu(Tarime) na amekubalika kwa wazazi wangu, kimbembe kimekuja baada ya kwenda kwao wazazi wake wamekataa wamesema mtoto wao hawezi kuolewa na mkurya kwani eti si watu wazuri wanapiga wanawake na ni wakorofi, nifanyeje kwa sababu nampenda sana huyu binti.
 
Achana naye, mbona Nyantira, Kemakorere, Sirari, Borega, Nyasincha, Nyamongo, Nyamwaga kuna warembo???

Dah.... Ukabila ni dhambi mbaya sana!!

Kumbe na wewe wa kule, kiukweli naumia sana kwa sababu binti anajiheshimu na mpole sana isitoshe tumefahamiana tukiwa tuko chuo.
 
Fita ni fita mura,usikubali hata kidogo, oa mnyaru huyo by any means.
cc. Mwita Maranya , Mamndenyi kwa msaada zaidi..
 
Last edited by a moderator:
FAIDA 10 ZA KUISHI BILA MPENZI
1:Unalala vizuri
2:Hujali unavyoonekana
3:Hakuna sms usiku wa manane
4:Unaweza kuongea na yeyote
5:Utaishi maisha marefu bila kubughudhiwa na
mtu
6:Utaepukana na fitina za watu
7:Utaepukana na ugomvi usio wa lazima
8:Hutakuwa mwenye kudanganyana
9:Utatulia kimawazo
10:Utajihisi uko huru kwa maamuzi yako .JARIBU
UONE.!
 
Achana naye, mbona Nyantira, Kemakorere, Sirari, Borega, Nyasincha, Nyamongo, Nyamwaga kuna warembo???

Dah.... Ukabila ni dhambi mbaya sana!!

umini-impress sana kwa kuyatamka kwa ufasaha maeneo haya!! nkohanchele mwiseke!
 
Achana naye, mbona Nyantira, Kemakorere, Sirari, Borega, Nyasincha, Nyamongo, Nyamwaga kuna warembo???

Dah.... Ukabila ni dhambi mbaya sana!!

Du, umerenga kwenyewe. Inaonekana nawe unatokea pande hizo, si bure. Mimi kwetu ni Itiryo, nimesoma Nyansincha Sekondari hadi form II kabla ya kutimkia kwenye public school. Amang'ana gaoo Charminglady?

Kuna watu wanaendekeza ukabila na wamekariri vibaya sana. Mimi hili lilinipa shida xana, hata ktk kupata partiner/girlfriend. Huwa nawaambia kwamba mimi ni MZANAKI. Kuna siku nilinyimwa chumba cha kupanga kwa ajili ya kabila langu. Baadhi ya wabaguzi wa ukabila wameenda mbali zaidi--hata ukijitambulisha kwamba unatokea kanda ya ziwa unaweza ukakosa mke au nyumba ya kupanga. Chezea wakabila wewe!
 
ila na nyie wakurya mmezidi ubabe kila mahali mpaka kwenye kugegedana haya sasa angalia unakosa mambo matamu,pole sana.
 
Jamani mimi ni kijana mwenye miaka 28 baada ya kumaliza masomo nimepata kazi hapa mjini, sasa nikaamua kutafuta mke ili nioe niache kumbwela mbwela nisije kufa kwa ngoma, nimepata mtoto wa kihehe wa kule mafinga tayari nimempeleka kwetu(Tarime) na amekubalika kwa wazazi wangu, kimbembe kimekuja baada ya kwenda kwao wazazi wake wamekataa wamesema mtoto wao hawezi kuolewa na mkurya kwani eti si watu wazuri wanapiga wanawake na ni wakorofi, nifanyeje kwa sababu nampenda sana huyu binti.
Molembe nakuhakikishia kuwa wewe hujawa tayari kumuoa huyo binti wa Kinyalu, kama ungekuwa unamhitaji kwa udi na uvumba wala usingekuja hapa kuomba ushauri, akili yako mwenyewe ingeshafanya kazi na kujua nini cha kufanya.

Mimi nimeoa msukuma na nilikutana na mazingira kama hayo unayoyasema. Sikumuuliza mtu nini cha kufanya lakini ukweli ni kwamba mke nilioa na hadi leo ninaye na wazee wake wananikubali "kinoma noma."

Katika hili wala sikupi ushauri wowote wewe mwenyewe tu akili ku mkichwa.
 
Last edited by a moderator:
hahahaaaa!! iam caught today!! kanambe nke ndakobhore mokungu!! tamaha uni hano nde!

kana hai olenge mosubhati weito!!

watetwa?
Oranyore ona ishing'ombe, nuwe nkeghanya ushe ontete, nkerenge mwiseke.
 
Kaka yangu ameoa mkurya na familia ilimkubali binti bila tatizo lolote (bila kwere) Lakini navyowajua ndugu zangu ingekuwa ni dada yao anaolewa huko hata kama wangekubali ingekuwa ni kwa shingo upande....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom