Kwanini vijana wengi wanakuwa ‘jobless’?

Kwanini vijana wengi wanakuwa ‘jobless’?

Habari zenu wakuu

Kumekuwa wimbi kubwa sana la vijana wasiokuwa na kazi wala vibarua mitaani zaidi ya kufanya day-work kwa kupata pesa ya kujikimu siku mbili tatu then ikiisha wanarudi tena kijiweni kwa kuangalia tena day-work na hawajui kama hilo ni tatizo kubwa sana la maendeleo yao.

Hiyo ndio inapelekea wingi wa vibaka na wapolaji wa mtaani kuanza tabia zisizofaa kwenye jamii na wazazi/walezi wao kuwaficha wanapofanya matukio kuto onyesha ushirikiano kwa polisi jamaii mpaka kwenye serikali kuu bila ya kujua kuwa mfuga mamba umtafuna mwenyewe.

Ndio haya mambo tunayoyasikia sasa hivi mara panya road mara sijui mamwitu na mawashawasha na makundi mengine ya ovyo ovyo na kupelekea kuwapoteza vijana wao kwa kuuliwa na raia wenye hasira kali kwa vitendo vyao visivyopendeza kwenye jamii mara wizi, uporaji mpaka uuaji na ubakaji.

Kazi/vibarua zipo nyingi sana ila vijana wengi wanapenda mafanikio ya haraka hawawezi kuvumilia mpaka siku za mishahara kupelekea kumuibia boss mpaka kufukuzwa makazini wamejawa na tamaa na hawajui kubana matumizi % ya vijana wengi mtaani kwenu ukiweza kuhesabu ni wajinga wajinga sana waelevu ni wachache sana wengi wavuta masigara, mabange mpaka kuwapelekea kuwa ma-adted wa maunga mpaka kuwapelekea kuwa na muonekana mbovu kushindwa mpaka kutoweza kuanzisha familia na kuilea uzuri.

Wanasababisha maisha yao kuwa magumu wao wenyewe kwa kukosa subra, uvumilivu.

Muhimu sana kuwatafuta watu wa kuwasaidia kujitambua kama wanajiona hawatoweza kujiongoza sio mpaka waharibikiwe.

Huruma sana kwa kijana/binti ukiwa haujielewi unaonekana kabsa anguko lako “ bila hata kutumia ramli au tambiko lolote.
Akili zao zimebobea kwenye bongofleva tu na panya road.
 
Sema we jamaa hadi unaandika hapa itakua ushatoboa kimaisha umekuja kutufokea tunaojitafuta

Maisha magumu mzee.. sema matoz/masister duuh hawawezi kujiuzisha sura barabarani kuuza maji, juisi au karanga wanataka wapigwe na ice-mda wote “ wanataka wale kiraisi
 
Kwamba ni wauza karanga wangapi wanaweza ku-sustain maisha yao na kubaki na disposable income ? Na unaongelea wauza karanga wapi wenye mashamba kule kijijini ambao wateja sometimes ni wa kubahatisha na wakija walanguzi wanachukua mzigo kwa bei hafifu pesa ambayo haimalizi mwaka..

Au unaongelea wauza rejareja mtu anatembea kutwa nzima na akiuza sinia lote huenda anachopata kisitoshe hata kununulia kiatu ambacho soli itakuwa imekwisha mwisho wa mwaka ?

Ni kupotoka kudhani kwamba taifa linaweza kujengwa na wachuuzi au wote kuwa wachuuzi, tunahitaji kuwa na sera za watu wetu kuwa more productive na sio kudalaliana na kula cha juu au kutegemea majanga ya mwingine ili wewe ndio upate fursa..

Sio sawa sawa kwenda kuwapola na kuwaibia watu au wakina dada kuwa makahaba mkuu
 
Ukijaribu kujiajiri tu mwigulu na TRA wanakuja na tozo vibanda vya machinga havitakiwi boda hawaruhusiwi kuingia mjini unataka wafanye kazi gani sasa kama ww una pakujishikiza shukuru mungu.

Mada itaanzia hapo mkuu..
 
Me nilichelewa wapi sijui
Nilijua wezi wote Ni wale wasio na kazi Hadi nilipokuja kujua kuwa wezi hatari wapo maofisini na wanavaa mashati meupe😂.

HAKUNA mtu anazaliwa mwizi ila wanajifunza na hii ni ishara tosha huwezi pata pesa sawa na mahitaji yako.
 
Ukweli 100% ni tanzania pekee unakoweza kukuta kijana hajui atakula nini jioni lakini wakati huo anawaza kula tunda kimasihara,hopeless kabisa yaani tena sisi wenye karama ya kusaidia wahitaji tunachoka yaani kila siku wenye shida wanaongezeka
M-bora sasa naona unatusimanga
 
Kashone na wewe kama ni kazi rahisi,kijana kumbatia sana kazi uliyonayo isije kukutoroka mtaani maisha ni magumu watu wanaishi kwa mkate

Ndio ninachofanya hicho mkuu.. na sifanani na vijana wezi wezi.. nashona viatu na kuuza viatu kwa siku nikishona viatu vyangu vinne vya elf- moja moja na nikiuza kiatu changu kimoja cha elf-sita nina elf-10 badget ndogo ya meza mke wangu tunapelekana mdogo mdogo” mambo yatakaa sawa tu na siachi kutembezi CV zangu kila kukicha lakini najua kuna sehemu nimetegea hata buku linaingia “ one day game litakubali tu- siwezi kwenda kukata watu mapanga kwa kusingizia serikali “ tabia zao mbaya tu na malezi mabovu “ maisha ni kujitegemea sio kutegemea
 
Me nilichelewa wapi sijui
Nilijua wezi wote Ni wale wasio na kazi Hadi nilipokuja kujua kuwa wezi hatari wapo maofisini na wanavaa mashati meupe[emoji23].

HAKUNA mtu anazaliwa mwizi ila wanajifunza na hii ni ishara tosha huwezi pata pesa sawa na mahitaji yako.

Hao sio wezi hao wanachukua haki zao mkuu.. mbona wanaiba kila siku na hawafukuzwi kazini kwa sababu wana ingiza faida mkuu
 
Sababu serikali ya ccm imeshindwa, serikali makini uandaa watu wake wapite wapi hadi tangu mwananchi anazaliwa hadi anakufa anajua njia. Panyaroad ni zao la kushindwa kwa serikali.
 
Sababu serikali ya ccm imeshindwa, serikali makini uandaa watu wake wapite wapi hadi tangu mwananchi anazaliwa hadi anakufa anajua njia. Panyaroad ni zao la kushindwa kwa serikali.

Nan! Sasa ataweza kuisimamia vyema hii nchi hii mifumo ya kiuraisi hata nimeshindwa kuiamini .. bora nchi iongozwe na JESHI tu
 
Kwa hio mtu anapenda kuwa jobless Ili ashinde njaa
 
Serikali makini uweka mipango bora ya watu wake kupitia kodi zao. Serikali iyofeli uacha vijana wake wanaelea elea. Hakuna mpango utoke wapi uende wapi
 
Yule bwana aliua uchumi,hata kazi za kubeba zege zimepotea,badala ya kujenga skimu za imwagiliaji,kaenda kujenga bwawa la umeme
 
Nan! Sasa ataweza kuisimamia vyema hii nchi hii mifumo ya kiuraisi hata nimeshindwa kuiamini .. bora nchi iongozwe na JESHI tu
Mfumo wa raisi sio mfumo bora wa kuongoza watu na wawe na maendeleo.Uraisi ni ajira kama zilivozingine kama uwaziri,uDC,RC na lengo kuu ni kutengeneza maisha binafsi, hawana tofauti na wapigania UHURU wao walipigania maslai yao binafsi kwa kuwahadaa waafrika eti wanawakomboa.
 
Yule bwana aliua uchumi,hata kazi za kubeba zege zimepotea,badala ya kujenga skimu za imwagiliaji,kaenda kujenga bwawa la umeme
Bora la umeme mvua zikinyesha ticha inapatikana,kuliko kutupa tilioni moja na nusu kununua ndege.
 
Huwa najiuliza hv inakuwaje Ukraine iweze kuzalisha ngano ya kuuzia nchi kadhaa Africa na yenyewe ijitosheleze kwa ngano lakini nchi yangu inashindwa hata kuzalisha ngano yake yenyewe tu hata isiuze wala kuagiza nje.
 
Ukweli 100% ni tanzania pekee unakoweza kukuta kijana hajui atakula nini jioni lakini wakati huo anawaza kula tunda kimasihara,hopeless kabisa yaani tena sisi wenye karama ya kusaidia wahitaji tunachoka yaani kila siku wenye shida wanaongezeka
"Ukweli 100% ni tanzania pekee unakoweza kukuta kijana hajui atakula nini jioni lakini wakati huo anawaza kula tunda kimasihara..."

Sahihi kabisa! Vijana wengi hawajielewi.
 
Ndio ninachofanya hicho mkuu.. na sifanani na vijana wezi wezi.. nashona viatu na kuuza viatu kwa siku nikishona viatu vyangu vinne vya elf- moja moja na nikiuza kiatu changu kimoja cha elf-sita nina elf-10 badget ndogo ya meza mke wangu tunapelekana mdogo mdogo” mambo yatakaa sawa tu na siachi kutembezi CV zangu kila kukicha lakini najua kuna sehemu nimetegea hata buku linaingia “ one day game litakubali tu- siwezi kwenda kukata watu mapanga kwa kusingizia serikali “ tabia zao mbaya tu na malezi mabovu “ maisha ni kujitegemea sio kutegemea
"...siwezi kwenda kukata watu mapanga kwa kusingizia serikali “ tabia zao mbaya tu na malezi mabovu..."

[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115] hiyo ndiyo point.
 
Back
Top Bottom