Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Nimesoma majibu yote uliyojibiwa kuhusu jambo lako, mimi nakushauri hivi pia.

Tafuta hela ya kutosha inayoweza kukukalisha kule kwa angalau siku 5.

Ukiripoti waulize watatumia muda gani kukuita rasmi ukaanze kazi, wakikuambia haijulikani ila watakupigia simu, nakushauri urudi nyumbani uje usubiri hiyo simu. Nauli ya Kasulu - Kibaha haiwezi kuwa kubwa na gharama utakayotumia kukaa kule kwa siku angalau 3.

Au kwa kusamaraizi, karipoti halafu rudi nyumbani, nauli ya kwenda na kurudi haiwezi kuwa kubwa ukilinganisha na gharama utakayotumia kukaa kule kwa angalau siku 3.

Reference: Case study.

Kuna mlamba Asali wa JKCI alitoka mkoani akapeleka barua, akaambiwa asubiri kupigiwa simu akakaa Dar kusubiri, zikapita wiki 2 bado hajapigiwa, hadi akakaukiwa mfukoni akaanza kulalamika(alileta uzi humu), tukaanza kumwambia alikosea, alitakiwa kurudi nyumbani kwanza.

Na wewe usije ukafanya hilo kosa.
Aisee umempa ushauri mzuri sana bwana Mwifwa Binafsi Mimi nilichukua barua utumishi mwishoni mwa Mwezi wa pili na nikaenda kureport Mwezi wa pili. U can imagine ijumaa ya tarehe 5 may ndio nilipigiwa simu kuitwa kazini. Asijichanganye kabisa kusubiri aende kureport then arudi home
 
Aisee umempa ushauri mzuri sana bwana Mwifwa Binafsi Mimi nilichukua barua utumishi mwishoni mwa Mwezi wa pili na nikaenda kureport Mwezi wa pili. U can imagine ijumaa ya tarehe 5 may ndio nilipigiwa simu kuitwa kazini. Asijichanganye kabisa kusubiri aende kureport then arudi home
Ni miezi 2 tangu kuripoti mpaka kupigiwa simu, je mshahara ulianza kuingia lini na ile posho ya kujikimu uliipata muda gani?
 
Usikute makofia360 ndo Kitenge mwenyewe
emoji1.png
emoji1.png
emoji1.png
(jokes)

Sent using Jamii Forums mobile app

Itatoka Leo kwel au ndo zitakaa hapo mpaka waajiri watupgie simu 😜😜😜
Kutoka sijajua ila kama sii wiki hii basi ijayo
 
Mshahara wa mwezi April nilipata. Na fedha ya kujikimu nimepewa Juma3 baada ya kureport kazini
Angalau wamejitahidi kufukia maumivu kwa kukupa mshahara wa April ambao ni haki yako kabisa maana ulisharipoti kazini tayari. Kama utaratibu ukiwa hivyo kuwa unaposubiri kupigiwa simu inahesabika uko kazini hapo ni sawa.
 
Wakuu naomba msaada wenu
Barua yangu imeandikwa nmeipokea tarehe 30 mwezi wa 3 badala ya Leo tarehe 11, inanitaka kureport katika kituo Cha kazi ndani ya siku 14 na sehemu niliyopangiwa ni mbali kidogo wilaya ya mji wa kasulu.
Sasa naona siku 14 zinaisha Leo, hii imekaaje wakuu, itakuwa walikosea kuichapa niwarudishie tena??
Usiogope soma vizuri imeandikwa "uripoti kituo cha kazi ndani ya siku 14 toka tarehe ya kupata barua"
Hata hivyo kama ni halmashauri watakupigia.
 
hii imekaaje wadau mbona taasisi zingine hawatoi?
Huu ni utaratibu wa kiutumishi kwa mujibu wa Government Standing Orders toleo la 2009, na marekebisho yake ya mwaka 2011. Kama hawajakupa unaandika barua kwa mwajiri ukiomba kulipwa posho ya kujikimu baada ya kuripoti kazini kwa ajira mpya. Wala huna haja ya kupoteza muda na maafisa utumishi ukiwadai kwa mdomo!!
 
Huu ni utaratibu wa kiutumishi kwa mujibu wa Government Standing Orders toleo la 2009, na marekebisho yake ya mwaka 2011. Kama hawajakupa unaandika barua kwa mwajiri ukiomba kulipwa posho ya kujikimu baada ya kuripoti kazini kwa ajira mpya. Wala huna haja ya kupoteza muda na maafisa utumishi ukiwadai kwa mdomo!!
Pesa ya kujikimu sawa taasisi nyingi wanalipa ila hii ya transportation mbona taaasisi nyingi hazitoi kwa first appointment
IMG-20230509-WA0022.jpeg
 
Pesa ya kujikimu sawa taasisi nyingi wanalipa ila hii ya transportation mbona taaasisi nyingi hazitoi kwa first appointmentView attachment 2618260
Pesa ya serikali hutoka kwa kuiandikia. Kwa afisa utumishi mwenye roho nzuri huwa mkiripoti tu mnajaza personal particulars halafu anawaelimisha kuhusu stahili zenu na namna ya kuzipata. Kwa kawaida huwa zipo fomu maalumu ambapo utajaza madai yako ya 1. posho ya kujikimu siku 7 kila siku ni sh 100,000/=. 2. Nauli kutoka kwenu hadi kituo cha kazi. Nyumbani kwenu ni kwaq mujibu ya jinsi ulivyojaza kwenye personal particulars. Kama una mke na watoto, na wenyewe wanapatiwa nauli na nusu ya posho ya kujikimu kwa siku hizo saba. 3. Gharama ya kusafirisha mizigo binafsi/personal effects. Hii haipungui tani 1.5. Kati ya hizo tani moja ni kwa parcel rate na zilizobaki ni kwa goods rate.

Sasa hili la kupewa pesa ya kusafirisha mizigo waajiri wengine huwa hawatoi na wanajua kabisa waajiriwa wapya hawatadai!! Lakini ukiidai kwa maandishi lazima utapewa, kama siyo leo kuna siku waqtalazimika kukupa maana ni haki yako ipo kisheria.

(Made under Standing Orders J.3, J.8, J.10, J.25) THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA STANDING ORDERS FOR THE PUBLIC SERVICE, 2009 SCALE OF LOCAL TRANSPORT AND TRAVELLING PRIVILEGES Category Posts CLASS OF ACCOMMODATION AMOUNT OF LUGGAGE DOMESTIC SERVANT’S TICKET Railways Road Services Lake or Coastal Steamers First appointment, transfer, termination of appointment, retirement Duty convalescent leave Travelling on leave at Government expense (excluding leave pending retirement, termination or appointment) First appointment, transfer, termination of appointment, annual leave, safari Duty (not entailing convalescent leave) (i) (ii) (iii) (iv) (v) (vi) (vii) (viii) (ix) (x) A Public servants in the TGS.J – Q and above Reserved 1st class berth compartment Upper Class First Class 5,000 kg 100 kg 100 kg 2 1 B Public servants in scales TGS.E – I First Class Upper Class First Class 5,000 kg 100 kg 100 kg 2 1 C Public servants in Scales TGS.C-D Second Class Upper Class Second Class 5,000 kg Public servant’s in Scales TGS.A-B Third Class Lower Class Deck 3,000 kg 50 kg 50 kg - -
 
Back
Top Bottom