Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Nawaza tu haya makanisa wangefuata tu mfumo wa kila muumini anatoa sadaka ya mazao anayolima au anayozalisha na sio lazima iwe pesa sijui watu wenye biashara kama yangu ya kuuza majeneza ingekuwaje
 
Haha..
Mwalimu bwana, series ya Askofu Rashid nilifanikiwa kuitia machoni ila bado haikuwa sababu ya Mimi kutokwenda ibadani.
Ingekuwa Rashid ni askofu wako ungeendelea kwenda? Mimi badala ya kusali ningekuwa naikumbuka Ile miuno yake..ningejitia dhambi bure bora kukaa nyumbani nisali na TV
 
Kichwa cha habari kilipaswa kuwa" kwanini uliacha kwenda kwenye nyumba ya ibada" na sio "kanisani"

Anyway,.

Mimi niliacha kwenda msikitini kwa sababu ya uwepo wa majini. Acha niishie hapa.

Nitakuja kuwapa stori kamili wakati mwingine.
Pole Sana...mkuu natumai huko uliko Sasa hakuna majini?
 
Aisee.Tulimpa dada yetu jukumu la kufatilia mirathi ya baba,bahati mbaya mirathi ikatoka tukiwa mbali kikazi,sister akachukua million 5 akapeleka kanisani km fungu la kumi. Aisee tulimmaind lkn haikusaidia kitu
Toka hapo mimi church kwa heri ilikuwa 2012 sijawah kanyaga

Sent from my SM-G531H using JamiiForums mobile app
Mngemkata kwenye fungu lake la.kugawana.
 
Mimi sio mhubiri mkuu, ila umesema kweli mahubiri ya kiislamu yanasisimua sana....muda wote mnafundishana na kuonyana kuhusu kumpendeza Mungu ila sisi huku daah ni mwendo wa kuelezana baraka tu za mwilini, utasikia kununua magari, kujenga kupata kazi. Yaani siku hizi ukisikiliza mahubiri ya kikristo ni kama vile unasikiliza warsha au semina ya wajasiriamali...kinachoongezeka ni kuwa tu huku anatajwa Mungu
Pokea...MAGARI I RECEIVE...POKEA Majumba I receive ..pokea MUME I receive..
 
Niliacha kwenda kanisani sababu ya kuyaheshimu masanamu tuliyoyatengeneza, hasa kipindi cha ijumaa kuu na Xmas. Nikaamua kuslimu, huko ndiko nilikokutana na dini ya kweli ya Mwenyezi Mungu na mtume wake
MashaAllah...Nakuombea Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema..akukunjulie riziki na akifanyie Mambo yako yawe mepesi..

Hakina dini ya kweli.Mbele Ya Allah Ni uisilamu...
 
Mimi nilikuwa mwana kwaya tena mpiga vyombo vya muziki.....sasa Kila tunapoanza kipindi wananiteua mimi kufungua kwa maombi na mimi hiyo TARANTA sina...yaani mbele za watu maneno yanapotea kabisa nakwama....mbaya zaidi wananicheka...siku nikawambia jamani tuheshimu vipawa vya Kila mtu humu ndani mwenye kupiga gitaa apige..mwenye kuimba aimbe..mwenye kujua kuomba atuwakilishe,,lakini wapi,nikaendelea kukomolewa tu....nikaona isiwe tabu...siwezi kuumbuka Kila siku.....na siwezi kwenda nikakaa kwa waumini hawatonielewa.....NASALI ZANGU NYUMBANI kwa kukwamakwama hivyo hivyo.
 
Mchungaji alinipora dem wangu church nikaona niwaachie tu kanisa lao.
 
Pale nilipotongozwa na mchungaji mkuu wa kanisa nikaona isiwe tabu nikakata mguu wangu
 
Siku Papa Francis alipotangaza mashoga wanakubalika kwenye kanisa wakati Biblia inapinga kabisa ushoga, nikajua hizi ndizo dini bandia tunazosoma kwnye Biblia, wale wanaosemwa na Yesu sikuwajua ninyi kamwe!
Wewe n I.... kweli sasa kabla kulikuwa na mapapa wangapi?
 
Sisi tunaokwenda kila siku na tuliojiapiza kuifia imani yetu tunakoment wap
 
Back
Top Bottom