Kwanini Tanzania hatuna furaha? Nini kifanyike?

Kwanini Tanzania hatuna furaha? Nini kifanyike?

Hata kama ni wewe umalize degree uambiwe uende veta
Utapeliwe na LBL
Utapeliwe na Kalynder
Utapeliwe na Dr.Manguruwe
Utapeliwe na Nicole utakuwa na furaha kweli?
hahaha kote huko unatapeliwa hushtuki
 
Ni kweli vijana lazima tupige kazi Ili tujipate.
Na hlilo linaanza na wewe.
Hivi ni nani anayetoa ruhusa/kibali au nani anauwezo wakujenga mambwawa makubwa ya kutunzia maji Ili yaje yatumike kwenye kilimo Cha umwagiliaji pindi mvua itapokuwa adimu.
Ujenzi wa mabwawa sio suluhisho endelevu (sustainable solution)kama hakuna mvua zitakazo nyesha-Utabaki na bwawa lako hapo na ukame utaendelea kwa wakati wake. Anza na Mazingira.
Wakina nani wanaochochea upepo mzuri au m-baya wa shughuli mbalimbali za kijamii,kiuchumi na kisiasa kwenye eneo husika.
Ni sisi wenyewe wakaaji wa eneo husika:
1. Kama tunadhani ni chama cha siasa kilicho madarakani; basi ni sisi wenyewe tulikiweka hapo kwa hiari yetu. Kwa hiyo kama chama hicho ndo tunaona ni kisababishi, bado tunao uhuru wa Hiari ya Kuiondoa na kuweka chama kingine tunachodhani kitaweza kutoa suluhisho.
2. Tujikite kwenye Utunzaji na Uhifadhi wa Mazingira e.g. tusikate miti hovyo bila sababu na Utaratibu, Tupande miti kila inapowezekana -itasaidia kupunguza makali ya mabadiliko ya Tabianchi
3. Wahudumu (watumishi, Taasisi na Mashirika)walio kwenye Huduma za Kijamii, Uchumi na Wanasiasa kwa Ujumla watangulize Uzalendo kwanza kabla ya mengine yote. Waache au waepuke "Umimi na Upendeleo" Nepotism and Egoism wanapotoa huduma kwa Jamii.
Aidha mimi naona sio sahihi sana "kumtafuta mchawi" na badala yake tuone kwamba sisi wakazi wa eneo husika Tumepotoka wapi na Tunaweza kufanya nini kabla ya kumnyoshea kidole mtu mwingine.
 
Mpaka mwisho wa 2010, Hosni Mubarak na wenzie walikuwa wanaishi kama CCM wanavyoishi sasa, wakiamini wameishika nchi hakuna wa kuwatoa.

Kufika 25 January 2011, kila kiongozi wa Misri alikuwa anatafuta pa kujifichia.

Wakati ukifika, utastaajabu inaweza ikawa hata mwendawazimu akawa ndio sababu ya kung'oka kwa CCM madarakani. Hawatotawala milele. Ni swala la wakati tu.

Na anguko hasa la CCM linaletwa na kiburi chao cha kuhisi wamefika.

Na sisi keyboard warriors tutakuwepo kushangilia nyuma ya pseudonyms zetu.
Nami naishi katika imani ya "HAKUNA MAREFU YASIYO NA NCHA" ila kila nikipiga mahesabu ya kibinadamu, hesabu zinagoma kwa hali ilivyo, watanzania tuna uvumilivu uliopitiliza mpaka kwenye uzezeta, sasa na uzezeta wetu huu, kuchomoka, labda waje watutie vidole vya macho.
 
hahaha kote huko unatapeliwa hushtuki
Kwani toka viongozi wetu wa kiserikali waanze kututapeli, tulishtuka lini, mara viwanda kubinafsishwa, mara ununuzi wa rada, epa na richmond, mara bandarj, sijui wanyama, ripoti ya CAG kila siku ina madudu lakini tupo kimya tu. 🤣 🤣
 
Natumaini ni kwema wakuu.

Kwa mujibu wa ripoti mpya ya orodha ya nchi zenye furaha duniani, Tanzania(136) tumepitwa mpaka na Somalia(122).

Imesikitisha sana hii habari ni kana kwamba naishi nchi ya majonzi,huzuni, na masononeko!
Somalia lazima ikupiteni, utakuaje na furaha wakati kuna watu wanafanya mauwaji ya kikatili kwa albino, watoto na wazee na kuwabaka/kuwaingilia kinyume na maumbile mpaka kufa, na wengine kuwaharibu kisaikolojia, unanyofoa sehemu za siri kwa wanawake, ushirikina, kuwauwa wezi na wengine kuwachoma moto, kamari, zinaa n.k.

Nikuulize tu, ushaona israel 🇮🇱/mayahudi wana amani furaha?? unadhani kuikalia ardhi ya wapalestina na kufanya mauwaji ya kikatili kwa watoto, wamama, wazee na vikongwe unadhani utapata amani na furaha! Laana ziendelee kuwatafuna mazayuni hao


Waafrika wengi ni makatili.
 
Nami naishi katika imani ya "HAKUNA MAREFU YASIYO NA NCHA" ila kila nikipiga mahesabu ya kibinadamu, hesabu zinagoma kwa hali ilivyo, watanzania tuna uvumilivu uliopitiliza mpaka kwenye uzezeta, sasa na uzezeta wetu huu, kuchomoka, labda waje watutie vidole vya macho.
Aisee mpaka kwenye uzezeta sheikh 🤣🤣🤣
 
Nami naishi katika imani ya "HAKUNA MAREFU YASIYO NA NCHA" ila kila nikipiga mahesabu ya kibinadamu, hesabu zinagoma kwa hali ilivyo, watanzania tuna uvumilivu uliopitiliza mpaka kwenye uzezeta, sasa na uzezeta wetu huu, kuchomoka, labda waje watutie vidole vya macho.
Kwa macho ya kawaida na kuangalia kiuhalisia wa muda waliokuwa madarakani ni ngumu kuamini kuwa CCM watatoka madarakani.

Ila nyakati zinabadilika, hazina kubwa ya CCM ilikuwa ni ubumbuwazi wa Watanzania. Dunia imebadilka kwa sasa, utandawazi taratibu unaamsha hata wale mambumbumbu wa mwisho.

Kwa sasa hazina pekee iliyobakiwa nayo CCM ni pesa, kutumia pesa kulaghai wachache wenye sauti kuaminisha wengine kuwa CCM inapendwa. Ila uhalisia mimi na wewe wote tunaujua, CCM haipendwi.

Hata hao wanaopiga kelele za mama hiki na mama kile, ndani ya mioyo yao wanajua fika kuwa wanauza propaganda za uongo ili kulisha matumbo yao.

Lini uliwahi kuona CCM ikitumia nguvu kubwa kujinadi kuliko wakati huu? Ni kwamba haikubaliki ila ina force kuaminisha watu kuwa inakubalika. Right now, they are desperate, ni wafa maji.

Labda naweza nisiishi kuona CCM ikiwa chama pinzani, lakini nina hakika mtoto wangu akiwa umri wangu, hakutakuwa na CCM tena.
 
Ningeona vigezo ningejifunza jambo, ila bila shaka hili dubwana la chama cha manyang'anyi lazima TU litakua linatukosesha furaha watanzania.
 
Mimi nafikiria labda kama marehemu MAGUFULI angekuwa bado raisi Asa hivi tungekuwa na furaha kiasi fulani.

Maisha ni magumu sana kiukweli watu hawapati hata milo 3 kwa siku sasa kutakuwa na furaha gani.

Wengi wana umia kwa ukali wa maisha na wachache wana furahia maisha wakiwa kwenye dimbwi la anasa kwa kutumia hovyo hela za walipa kodi.

Kwa kifupi tupo kwenye hali mbaya sanaaaaa.
 
Natumaini ni kwema wakuu.

Kwa mujibu wa ripoti mpya ya orodha ya nchi zenye furaha duniani, Tanzania(136) tumepitwa mpaka na Somalia(122).

Imesikitisha sana hii habari ni kana kwamba naishi nchi ya majonzi,huzuni, na masononeko!
Jipime.
 
Ni sahihi kabisa. Zamani kidogo mwanzo wa Azimio la Musoma-1974, vijana - ambao ndo nguvu ya Taifa lolote duniani, walipitia mafunzo ya JKT (mujibu wa sheria na kujitolea) kwa mwaka 1. (mwaka mmoja) na huko walipata mafunzo ya kina na Hamasa iliyoujenga na kuchochea uzalendo wao kwa Taifa. Siku hizi JKT???? Dah! Eti ni miezi 3 (Tatu) kwa wale wa Mujibu wa sheria i.e. Ni kwa lazima. Hawa wa Mujibu wa Sheria ndo wanaotegemewa baadaye kwenda vyuoni kujifunza fani mbali mbali ili mwisho wakirudi waje kutoa Huduma kwa Wananchi na Jamii kwa ujumla. Inashangaza sana kwani Lengo la JKT ni Mafunzo yahusuyo Ulinzi wa Taifa, uzalendo, Ujasiliamali, Ujasili (kupitia mafunzo ya Kilimo, Ufugaji na Biashara) kwa nyakati tofauti tofauti kadri ya maelekezo kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Je, kweli hilo 👆 👆 linaweza kutekelezeka ndani ya miezi mitatu(3)???? Waheshimiwa viongozi wetu kama yupo atakayebahatika kuisoma koment hii; Tusidanganyane hata kidogo. Sisi wote (nyie Viongozi na sisi Raia)ni watu wazima. Tuwe wakweli.
Juzi juzi kulikuwa na mafunzo ya vikosi almaarufu kama Jeshi la Mgambo, Chipukizi (sio wale wa vyama vya kisiasa hapana), Skauti na katika masomo ya Darasani esp. Shule za msingi, kuliwekwa kwa namna fulani Hamasa ya watoto kuitambua na kuipenda Nchi yetu. Siku hizi, Dah! Watoto S/M wamekazaniwa Haki za watoto, Jinsia, Afya ya Uzazi n.k. n.k.
Naam,Furaha yetu imejificha hapo!
 
Ukiwa muoga Utakosa Furaha
WaTz waoga sana

Tunaishi na watesi wetu kama ni wenzetu
Watesi ni hawa:

Machawa

Wanaoijiita manabii sijui Watumishi

watawala

Hawa wanaochangia kufanya WaTz wakose furaha na Amani mioyoni.

Tunaishi ilimradi siku iende tu!
 
Hatujakopa hovyo mkuu; ila Tulishakopa tayari. Kwa hiyo kwakuwa tulishafanya kosa la kukopa (tulishakopa i.e. tunamadeni tunadaiwa) tusahau kupata Furaha sio? Kama ndo hivyo; basi duniani hakutakaa kuwe na Furaha kwani kila Taifa duniani hukopa na kukopesha. Kila familia hukopa na kukopesha; hata ndugu na ndugu hukopa na kukopesha. Mwanamme na mwanamke nao pia hukopa na kukopesha.
Kopa kidogo sasa unakopa na Huna uhakika
 
1-5 yote ni tatizo kubwa na wadau wanadai chanzo kikuu ni mifumo iliyowekwa na CCM wametoa mpaka na mifano.
Hebu kwa utulivu wadau tuliangalie suala la Chama kilicho madarakani na uwepo wa Hizo changamoto 1-5.
1. Chama chochote kile kitakachokuwa ndo kipo madarakani , Jukumu lake la kimsingi ni Kuisimamia Serikali.
Chama kinaisimamia Serikali ili ifanye vizuri na kwa Mujibu wa Ahadi zake walizotoa wakati wanajinadi kwa Wananchi ili wapate rridhaa ya kuwepo Madarakani. Kwa mantiki hiyo Kama hao chama walikuwa na Ahadi ambazo tuliziona sio sawa, basi tungewahoji jukwaani au tungewakataa kwenye sanduku la Kura. Usiniambie waliiba kura. Wewe uliuwa umelala? Kwanini wewe nawe usiibe kama hiyo ndo Order of the day??
2. Serikali ndo Mtekelezaji Mkuu na ndo yenye Wataalam ambao huishauri Serikali na Wanasiasa (Bunge) ambao hutnga Sera na Kuweka Dira ya kutufikisha huko tuanako lenga kufika. Je hao Wataalam wametoa Uhauri au nao Wamekuwa ni sehemu ya Upotofu wetu kama Jamii?? Sijawahi kusikia au kumwona Mtaalam e.g. Wahandisi, ma PhD holders et al wakipendekeza kwa ADABU hoja mtambuka inayotarajiwa kupelekwa bungeni kama Muswada. Wataalam(Wengi) wanapopendekeza jambo hawaoneshi kwamba huo ni Ushauri tu bali wao huongea kwa mtindo wa kukosoa tena wanafoka (kimaandishi au hata kwa kauli za mdomo)kana kwamba hawatambui hao wabunge (hata kama ni std 7) ndo Boss wao anapokuwa amekalia kiti Bungeni. Watoe ushauri kwa unyenyekevu na kwa Adabu.
3. Kule Bungeni yupo Katibu wa Bunge ambaye ni Mwajiriwa wa Serikali i.e. ni Mtaalam. Chini yake wapo wataalam wa fani mbalimbali. Hao wanashindwaje kufanya marekebisho katika Sera ili ziwe Rafiki kwa wananchi na Wabunge? Mbona wanaziacha zinaingia Bungeni zikiwa Uncensored?
Mimi nashauri ingelifaa kila mtu katika nafasi yake ajitahidi kufanya Kwa Uzalendo huku akijua kwamba anavyoligema ndivyo atakavyolinywa - Leo Afisa Mtaalam yupo Ofisini anabweteka na anasahau kwamba kesho atastaafu na atayakuta na kuyaishi yale yale (Kero)aliyoyaidhinisha alipokuwa Ofisini.
 
Na hlilo linaanza na wewe.

Ujenzi wa mabwawa sio suluhisho endelevu (sustainable solution)kama hakuna mvua zitakazo nyesha-Utabaki na bwawa lako hapo na ukame utaendelea kwa wakati wake. Anza na Mazingira.

Ni sisi wenyewe wakaaji wa eneo husika:
1. Kama tunadhani ni chama cha siasa kilicho madarakani; basi ni sisi wenyewe tulikiweka hapo kwa hiari yetu. Kwa hiyo kama chama hicho ndo tunaona ni kisababishi, bado tunao uhuru wa Hiari ya Kuiondoa na kuweka chama kingine tunachodhani kitaweza kutoa suluhisho.
2. Tujikite kwenye Utunzaji na Uhifadhi wa Mazingira e.g. tusikate miti hovyo bila sababu na Utaratibu, Tupande miti kila inapowezekana -itasaidia kupunguza makali ya mabadiliko ya Tabianchi
3. Wahudumu (watumishi, Taasisi na Mashirika)walio kwenye Huduma za Kijamii, Uchumi na Wanasiasa kwa Ujumla watangulize Uzalendo kwanza kabla ya mengine yote. Waache au waepuke "Umimi na Upendeleo" Nepotism and Egoism wanapotoa huduma kwa Jamii.
Aidha mimi naona sio sahihi sana "kumtafuta mchawi" na badala yake tuone kwamba sisi wakazi wa eneo husika Tumepotoka wapi na Tunaweza kufanya nini kabla ya kumnyoshea kidole mtu mwingine.
Dah!sawa bhana ngoja tuone kwenye uchaguzi wa mwaka huu japo najua ya mwakajana uliyasikia na miaka iliyopita umeyasikia, japo malalamiko yapo Kila siku maeneo mengi tu duniani wakati wa uchaguzi ila hapa bongo kwanijuavyo🤓🙌

Na sibishi ni sisi ndo wakuondoa tusichotaka ila Uingereza,Ufaransa,Urusi,Ujerumani n.k walitumia njia ngumu sana kuondoa wasichotaka na mpaka Sasa hivi angalau raia wakisema jambo fulani wanasikilizwa ,nadhani wote (wanasiasa na Rai) wanakumbuku juu ya kile kilichotokea enzi hizo za mababu zao(chanzo,matokeo yake,madhara na faida yake)

DAMU ZILIMWAGIKA❌🔥😔😎
 
Ukiwa muoga Utakosa Furaha
WaTz waoga sana

Tunaishi na watesi wetu kama ni wenzetu
Watesi ni hawa:

Machawa

Wanaoijiita manabii sijui Watumishi

watawala

Hawa wanaochangia kufanya WaTz wakose furaha na Amani mioyoni.

Tunaishi ilimradi siku iende tu!
uoga wako ndio umasikini wako, na umasikini ndio chanzo cha kukosa furaha.
 
Back
Top Bottom