Sio kweli. Kwa mfano Hadi March 2025 (mwaka huu) Maeneo mengi ya Nchi mvua hazijanyesha vizuri. Kwa hiyo Mwakani tunatarajia kuwepo na upungufu mkubwa wa chakula hapa nchini. Tukiwa na njaa tutakosa furaha. Je, hao jamaa CCM wanahusikaje na ukame uliojitokeza? Hao CCM wanauwezo gani kuondosha Ukame? Mbona na wao wanalia-lia kama sisi tusiokuwa na Chama? Mimi nadhani mambo mengine siyo ya Kisiasa na kwa hiyo ufumbuzi wake hautoweza kupatikana kwenye siasa.
Unaonaje kama:-
1. Unapata chakula safi na cha kutosha
2. Unapata huduma nzuri na toshelevu za kijamii e.g Elimu, Afya, Maji, Usafiri, Mawasiliano, Ulinzi na Usalama, Kiimani hubughudhiwi, n.k.
4. Unakuwa na Amani ya moyoni na miongoni mwa Jamii unamoishi
5. Unakuwa uko huru kufanya mambo yako kwa namna unayotaka lakini bila kuvunja sheria zilizopo.
Kama hayo 1-5 yapo na unayapata; utakuwa na sababu gani za msingi kwenda kuikumbatia Siasa???