Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,891
- 155,907
Ubadhirifu na wizi, matumizi mabaya ya fedha za umma na rasilimali za taifa kutumiwa kwa maslahi ya watu wachache kumeongezeka sana.
Mbaya zaidi Rais amesikika mara kadhaa akisema kwamba upigaji kwenye Halmashauri ni mkubwa sana. Tozo zinapigwa, fedha za miradi zinapigwa, fedha za misaada zinapigwa, yaani mchwa, nzige, tunutu, madumadu, nzige na maparare yako huko.
Ripoti za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali zimekuwa zikibainisha madudu ya ajabu kwenye idara mbalimbali za serikali.
B. O. T watu waliiba mabilioni wakasingizi kwamba ni hela chakavu. Lakini baada ya uchunguzi ikagundulika kwamba hela hazikuwa chakavu, ila ni fedha mpya zilikuwa zikikatwa.
Wizi umetamalaki kila sehemu, je serikali ya CCM haioni? Au ina faidika na hali hii? Kwanini hawajengi magereza mapya ili mijizi yote ichukuliwe hatua ikapumzishwe huko?
Haya mambo ya mtu akifanya ubadhirifu ahamishwe kituo sasa yafike mwisho.
Mbaya zaidi Rais amesikika mara kadhaa akisema kwamba upigaji kwenye Halmashauri ni mkubwa sana. Tozo zinapigwa, fedha za miradi zinapigwa, fedha za misaada zinapigwa, yaani mchwa, nzige, tunutu, madumadu, nzige na maparare yako huko.
Ripoti za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali zimekuwa zikibainisha madudu ya ajabu kwenye idara mbalimbali za serikali.
B. O. T watu waliiba mabilioni wakasingizi kwamba ni hela chakavu. Lakini baada ya uchunguzi ikagundulika kwamba hela hazikuwa chakavu, ila ni fedha mpya zilikuwa zikikatwa.
Wizi umetamalaki kila sehemu, je serikali ya CCM haioni? Au ina faidika na hali hii? Kwanini hawajengi magereza mapya ili mijizi yote ichukuliwe hatua ikapumzishwe huko?
Haya mambo ya mtu akifanya ubadhirifu ahamishwe kituo sasa yafike mwisho.