Kwanini Nyerere hakutaifisha seminari za Katoliki?

Status
Not open for further replies.
Mkuu UncleBen Tumsifu Yesu Kristo....We ni kijana wa Seminari ipi?
Kama umenisoma vizuri kwenye post yangu hapo juu nilisema "Vijana wanaostahilishwa kuwa mapadre japo hawakustahili"....hii ni sentensi ya kinyenyekevu mbele za Mungu,kwamba hata hao wanaokuwa Mapadre si kwamba wanastahili,bali wanastahilishwa tu,ili waweze kutangaza utukufu na sifa za Mungu.Ndio maana siku ya kiapo cha Upadre wao husema "Ee bwana ulichokianzisha ndani yangu ukitimize,si kwa ajili yangu,bali ni kwa sifa na utukufu wa jina lako,kwa maana mimi sistahili kwa lolote kuyashika yaliyo matakatifu yako"
Milele amina
Nashukuru mkuu wewe ndio umenijibu vizuri ,niliposema mimi ni mshenzi wa tabia wengi hawakunielewa ,badala yake hawakutaka kuniuliza kwanini nimesema hivyo wakaanza kuni atack kana kwamba wale wanaofanywa kuwa mapadre ni watakatifu ,kumbe hata wao sio kwamba wanastahili bali ni wanastahilishwa ,kwa kiapo hicho ambacho wengi wa wachangiaji walikua hawakijui ama wanakijua wakaamua tu kupuuza na kuniona mimi ni mkosaji mkubwa sana niliposema mimi ni mshenzi wa tabia
 
Kufuatia Azimio la Arusha serikali ilitaifisha taasisi ikiwemo hospitali, vyuo,majengo n.k. vya watu binafsi na mashirika ya kidini. Lakini shule za seminari za Kikatoliki hazikuguswa nini sababu hasa?mwenye kujua naomba msaada.
NB:
Ieleweke si kila shule inayomilikiwa na katoliki ni Seminari (mfano; St. Francis High School = sasa Pugu Sec. hii haikuwa seminari per se).
Chemsheni bongo msitoe majibu laini laini kama kawaida ya watanzania, hii sio kipima joto cha ITV kubwabwaja utumbo hapa ni "pweinti" tu zinatakiwa.
Mtoa mada naona una mshawasha ngoja wakunaji waje wakukune
 
Kufuatia Azimio la Arusha serikali ilitaifisha taasisi ikiwemo hospitali, vyuo,majengo n.k. vya watu binafsi na mashirika ya kidini. Lakini shule za seminari za Kikatoliki hazikuguswa nini sababu hasa?mwenye kujua naomba msaada.
NB:
Ieleweke si kila shule inayomilikiwa na katoliki ni Seminari (mfano; St. Francis High School = sasa Pugu Sec. hii haikuwa seminari per se).
Chemsheni bongo msitoe majibu laini laini kama kawaida ya watanzania, hii sio kipima joto cha ITV kubwabwaja utumbo hapa ni "pweinti" tu zinatakiwa.
Utangulie milembe unaweza kupata msaada haraka
 
Ndio maana kanisa katoliki limekuwa viongozi makini, si kwa Tanzania tu bali barani Afrika na duniani tofauti na yule Mzee wenu wa "kuzima na kuzinduka"
 
Kwa hiyo ulitaka na Madrasa zitaifishwe? Seminary ni shule kwaajili ya kufundishia wanafunzi wa upadre na Viongozi wa Dini si kwajili ya Elimu Dunia.
 
Mtoa ameuliza seminari za Kikatoliki (na sio shule za kawaida za kanisa, sijui St. Francis=pugu n.k)

sasa kuna seminari za kiislam zilizokataifishwa mkuu...nijuze tafadhali vinginevyo udini unawasumbua baadhi y watanzania
 
Kwanza elewa maana ya SEMINARY, ambayo ni madrasa ya dini,huko wanafunzwa kuwa viongozi wa dini husika.
 
Seminari ni vituo maalum vya Kanisa kwa ajili kufundishia viongozi wenye wito wa kulitumikia Kanisa. Kutaifisha ingekuwa sawa na kutaifisha majengo ya makanisa!
Jibu zuri sana hilo na sidhani kama atauliza tena swali kama hilo!! Anashindwa kuelewa kuwa seminary ni shule kwa ajili ya kuandaawatu kuelekea Upadri!!
 
Kwa hiyo ulitaka na Madrasa zitaifishwe? Seminary ni shule kwaajili ya kufundishia wanafunzi wa upadre na Viongozi wa Dini si kwajili ya Elimu Dunia.
Acheni basi upotoshaji ,sio kwa ajili ya kufundisha elimu dunia ? Hao madaktari ,mainjinia na wanasheria waliopita seminari maana yake ni nini ???
 
Kama lengo ni kuandaa mapdre peke yake kwanini wasisome theology kuanzia o level na A level mpaka chuo kikuu ?? Kwanini kuna PCB,PCM,HGL,HKL,EGM na kadhalika ? Bora hata mimi nakubali ni mshenzi wa tabia ,hao ambao wewe unawaona watakatifu ,unajua kashfa zinazo isumbua kanisa sasa hivi ?? Wanaofanya si hao hao mapadri na ma sista ??

unashibdwa kuelewa kwamba Elimu dunia ni muhimu pia hawa viongoz kwan wanawaongoza binadamu wenye taaluma mbalimbali co malaika. kuhsu kash
fa hawa ni binadamu na wana mapungufu yao mmoja mmoja ila co kanisa.

kingne ukijue co mapadri wote lazma watokee seminarini.
 
Seminari ni vituo maalum vya Kanisa kwa ajili kufundishia viongozi wenye wito wa kulitumikia Kanisa. Kutaifisha ingekuwa sawa na kutaifisha majengo ya makanisa!
Seminari ni vituo maalum vya Kanisa kwa ajili kufundishia viongozi wenye wito wa kulitumikia Kanisa. Kutaifisha ingekuwa sawa na kutaifisha majengo ya makanisa!
Daaah kama hatokuelewa kwa haya majibu mafupi lakini halisia hakuna atakae muelewa.
Thnx kwa majibu mazuri.
 
unashibdwa kuelewa kwamba Elimu dunia ni muhimu pia hawa viongoz kwan wanawaongoza binadamu wenye taaluma mbalimbali co malaika. kuhsu kash
fa hawa ni binadamu na wana mapungufu yao mmoja mmoja ila co kanisa.

kingne ukijue co mapadri wote lazma watokee seminarini.
Ume elewa hoja yangu ilipoanzia ? Ungesoma comments zote ungeelewa kwamba nilichokua na pinga ni hoja ya mdau mmoja anayesema ukisoma seminari lazima wote wawe ma padre ,ndio nikamkatalia
 
Shule za seminari ni mahsusi kwa ajili ya kuwaandaa Mapadre na watawa wa kanisa katoliki,ukizitaifisha viongozo hawa watatoka wapi?uendeshaji wake ni wa kikanisa na misingi yake pia.

tukisema lengo kuu ni kutoa mapadree au watumishi wa kanisa co saws., hiz seminsri malengo yake mengne ni kuwasaidia vijana wa kikatoliki ili wapate Elimu pia itakayowasaidia ktk maisha yao na jamii yao kwa ujumla. na ukienda kule hakuna anae kulazimisha kuja kuwa padri Bali we mwenywe utakavyokigswa. njia ya kwenda kusomea upadri ni tofaut na kusoma seminari. kuna watu wanakuwa mapadri bila kupitia shule xa seminari.
 
Watanzania ni wavivu kufikiri, mtoa mada kauliza kwa nin SEMINARI za KATOLIKI hazikutafishwa mtu anakuja kusema zilitaifishwa ikiwemo Forodhani? Really? Forodhani ilikuwa SEMINARI toka lini? TOFAUTISHENi SEMINARI vs SHULE ZA KAWAIDA ZA KANISA> Takbiiiriiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii..................
Wewe na mtoa mada pia ni wavivu wa kufikiri... Mngetafuta maana ya seminari kwanza mpate msingeleta hilo swali... Wanamjibu utani sababu na yeye kauliza swali la utani.
 
seminari ni shule za kutayarisha watumishi watakaokuja kuhudumu kanisani kama mapadri masista maburuda n.k wala si za biashara ndiyo sababu hawachukui mtu ni mtu tu kusoma huko .kuna selection kali sana huko ya watu wavumilivu na wanaodtahili kuendelea na masomo ya juu sasa mtoa mada ulitaka zitaifishwe ili iweje au ulitaka kanisa life?.kwa kukosa watendaji au wakasomee nje ya nchi?.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom