Kalunya
JF-Expert Member
- Oct 5, 2021
- 13,307
- 18,704
Mungu ni RohoKwani Mungu ni nini ?
Mungu ni RohoKwani Mungu ni nini ?
Weka vidhibitisho mezani na vitu gani vinakufanya uamini hivyoSio katika perception ya kidini bali katika dhana nzima ya uwepo wake imekaa kimagumashi.
Sababu kuu ni kuwa hakuna uthibitisho wa Mungu kuwepo
Unawezaa vizuri tuu tena Sayansi ndio inaeleza vizurii na kutoa majibu sahii ya uwepo wa Mungu kuliko dini zetuMungu ndio mtoa pumzi na chanzo cha upendo kwetu sisi wanadamu.
Ulimwengu si sababu ya Mungu kuwepo kwani yeye ndiye aliyeuumba.
Angeendelea kuwepo hata asingeumba ulimwengu na sisi wanadamu.
Kiukweli imani zetu za kidini hazituweki wazi sana juu ya sababu hasa ya Mungu kuumba ulimwengu.
Kwanini asingeacha tu??
Kuumba ulimwengu kunamfaidisha nini hasa??
Kutokuumba ulimwengu kunahasara gani kwake??
Je, hakujua anguko la mwanadamu kabla ya uumbaji wake??
Zaidi, baadhi ya dini zinatuambia kwamba kulingana na ukuu wa Mungu, baadhi ya maswali hayawezi kujibika kwa akili zetu na tutapata nafasi ya kuuliza maswali yanayo tutatiza tufikapo mbinguni.
NB: Huwezi kuelezea uwepo wa Mungu nje ya imani za kidini (ni swala la imani tu).
TUANZIE HAPA... KWANINI WEWE UPO?NB: Huu mjadala sio wa kubishana kama mungu yupo au hayupo.
Hapa ninataka kuwauliza Kwa upole wale tunaoamini tayari kuwa Mungu yupo...Je, kwanini yupo?
Yaani siulizi mungu ametokea wapi/ametokanaje...
Hapa naulizia Kuna ulazima Gani wa yeye kuwepo? na kwanini yupo?
Mfano mtu akiuliza kwanini viti vya kukalia vipo, huwezi kujibu kwasababu mbao zikikatwa na kuchongwa vizuri zinatengeneza kiti, hapa utakuwa umejibu viti vinatokanaje....jibu zuri ni kwasababu vinatufanya binadamu tukae na kupumzika, hivyo tumevitengeneza...Inamaana bila kuwepo binadamu wenye shida ya kukaa basi viti visingekuwepo...
Kwahyo napouliza kwanini Mungu yupo? Siulizii chimbuko lake ametokana na Nini, ila naulizia ni sababu Gani iliyompelekea/iliyomlazimu yeye awepo.
Kuna wanaosema Mungu yupo ili auumbe ulimwengu, kwahyo function kubwa ya Mungu ni kuumba na kuendesha ulimwengu.
Hilo jibu kwangu halitoshelezi kwakuwa, Ningeuliza kwanini Huu ulimwengu upo?, Kwani Kuna ulazima ulimwengu uumbwe?
Kama Kuna ulazima wa ulimwengu kuwepo, basi Inamaana ulimwengu una thamani kuliko Mungu, kama binadamu tulivyo na thamani kuliko viti. Maana sisi ndo tumeleta viti, basi Ulimwengu umemleta Mungu.(yaani kama ni lazima ulimwengu uwepo, basi ulimwengu ndio umemlazimu Mungu awepo kama ambavyo Nyumba zinawalazimu mafundi ujenzi kuwepo,Simu zinawalazimu wauza simu kuwepo,Magari yanawalazimu madereva kuwepo, wahalifu wanalazimu polisi kuwepo nk.)
Lakini common sense inakataa.
Ingewezekana TU kusiwe na chochote, Hamna Dunia,hamna,Nyota,Hamna sayari, na Hakuna Mungu.
Sasa kwakuwa hivi vitu vipo, Je ni kwanini vipo?
Na kama ingewezekana kusiwepo kitu,Je ni Nini kililazimisha Mungu awepo?
Na kama mungu alikuwepo kabla ya Ulimwengu, na hakulazimishwa kuumba ulimwengu (angeamua angeacha na kubaki mwenyewe) Je yeye kwanini yupo? Nini kilipekea yeye kuwepo?
Kwanini Mungu yupo?
Ebu tuletee vidhibitisho ya hii kauli yako kwamba majini waligoma kumuabudu munguHapana Mungu amekuwepo hata kabla ya huu ulimwengu kuwepo, uthibisho huu ulimwengu sio binadamu ndio walianza kuumbwa bali ni majini kwanza kabla ya wanadamu, binadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu baada ya majini kugoma kumuabudu Mungu.Kabla ya majini kuwepo duniani,vipo viumbe vingine vingi pia katika sayari zingine nje ya Dunia.
Mfano UFO, malaika,nk.
Na still pana mamilioni ya sayari zingine ambazo hazijagundulika kwa macho ya sayansi ya mwanadamu.
Majini wao walishahukumiwa tayari kwao ni motoniEbu tuletee vidhibitisho ya hii kauli yako kwamba majini waligoma kumuabudu mungu
Kama wanakufa wanazaliwa pia.Jini mmoja uishi hadi miaka elf 6Hivi majini bado wanazaliwa?
Mchungaji hatupo kanisani hapa weka hoja zako sawa zieleweke sio kulazimishaMtaongea weeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!! lkn Mungu kamwe hatajulikana kwa kondoo wasio wake! kwa sababu kondoo wake wanamjua mchungaji wao!!
Na mbinguni hamwendi ng'oooooooooooo!
Yah utamuadhibu ila huwezi kumpa adhabu ya kumuua wala kumpa adhabu ambayo hawezi kuhimili na kingine kwann umuadhibu kwa makosa ambayo ww Ndio umeyatengenezaNitamkanya mara tatu asiposikia nitamwadhibu
Kwann ww upoKabla hajaiumba dunia Yeye alikuwepo,kabla ya kumuumba mwanadamu na viumbe vingine Yeye alikuwepo,wewe na viumbe wengine mtakufa lakini Yeye ataendelea kuwepo
Mungu yupo kwasababu alipenda kuwepo hakuna aliyemuweka hapo alipo mpaka ahoji kwanini yupo,pia hata ukijua kwanini yupo haitakusaidia,cha kukusaidia ni wewe kujiuliza kwanini upo au kwanini uliumbwa,hiki ndicho kitakachokusaidia
Acha kupoteza muda hapa jamii forum kufikiria mambo ambayo hakuna mwanadamu ashibaye wali maharage anaweza kujibu,hata malaika ambao ni watakatifu hawataweza kulijibu swali lako,mambo yaliyoko wazi na yaliyofunuliwa kwenye upeo wa akili zetu na macho yetu hayo ni ya kwetu ila ambayo huna huwezo nayo hayo niya kwake Yeye ambaye Yuko na ataendelea kuwepo
swali ambalo unapaswa ujiulize na litakalokusaidia ni kwanini wewe upo?
Nmesema utuletee vidhibitisho sio imani yako ww jini umewahi kumuona au nani alikumbia kuwa majini yalikuepo na yalihukumiwa motoniMajini wao walishahukumiwa tayari kwao ni motoni
Huwezi kwenda motoni bila kuasi
Kama wanakufa wanazaliwa pia.Jini mmoja uishi hadi miaka elf 6
Sijataka kumuonaWw jini umewahi kumuona
Kwa mujibu wa maandikoNmesema utuletee vidhibitisho sio imani yako ww jini umewahi kumuona au nani alikumbia kuwa majini yalikuepo na yalihukumiwa motoni
Yes sababu ni uzao uliohukumiwa tayariKwahyo jini anayezaliwa leo, ameshaandikiwa moto wa jehanam mbingu hatoiona?