Kwanini Mungu yupo?

Kwanini Mungu yupo?

Hapana sijakosea, mungu yupo ili kuwasimamia wanadamu ni mtazamo wa wanadamu juu ya uwepo wa mungu.
Nje ya mtazamo wa mwanadamu mungu yupo bila sababu maalum ni kama reality itself.

Nikikuuliza wewe kwanini upo hai utajibu nini?
Anawasimamia binadamu katika lipi?

Ukraine kuna massive murders watu wanakufa afu we unasema anatusimamia.

Ukiniuliza kwanini nipo hai jibu ni moja tu

Nipo hai kwasababu ya juhudi zangu binafsi za kuepukana na hatari zinazoweza nisababishia nisikuwepo though active cells nazo zinanifanya nizidi kuongeza number ila zikichoka nitakufa tu
 
Hakukuwa na error isipokuwa amevipa viumbe free will na ujuzi wa kutambua baya na jema lakini wanatakiwa na anawataka wafanye mema na yule mwenye kushinda huo mtihani atazawadiwa na aliyeshindwa ataadhibiwa.
Ili freewill iwepo inatakiwa Mungu asijue atachoenda kuchagua mtu
 
Wahenga walisema fimbo ya mbali haiui nyoka au hela iliyo mkononi ina thamani kuliko iliyopo kibindoni au hisani yaanzia nyumbani (charity starts at home) au ndege aliyekuwepo mkononi ni bora kule mia waliopo porini (a bird in hand worth hundred in bush).

Anza na wewe mwenyewe kujua kwanini upo duniani ??!!--- baada ya hapo you move a step further to ask other related questions.
Sidhani kama kuna shida kwenye swali lake linalofanya ashindwe kupatiwa majibu kwasababu kuna vingine vinavyo muhusu yeye havijui.

Unaweza usijue vinavyo kuhusu wewe lakini hiyo haikuzuii wewe kushindwa kuhoji vingine.

Ni sawa na mimi hapa mtaani nisiwe na mjua balozi wa nyumba kumi, nikawa nataka kujua waziri wa fedha wa Tanzania ni nani, sidhani kama nitashindwa kujibiwa swali hilo kwa wanaojua eti kwakua tu simjui balozi wa nyumba kumi.
 
Kuheshimiwa Kuna faida nyingi sana...Tena sio Kwa mwanangu TU, natamani niheshimiwe na kila mtu. Kuheshimiwa Kuna faida nyingi ila faida kuu, ni kuwa ukiheshimiwa huwezi kufanyiwa mambo mabaya kama
Kutukanwa,Kuibiwa,Kupigwa,kudharauliwa,Kutengwa,nk. Nk.
Kumbuka sisi binadamu ni social primates ..yani tunaishi Kwa kutegemeana sana.

Turudi Kwa Mungu, yeye anatutegemea sisi? Jibu ni nadhani utasema ni Hapana.
Na kama ukisema ndiyo, Bado swali litabaki kuwa "Je sisi binadamu na Mungu tunaotegemeana, tupo Ulimwenguni Kwa Nini?"

Sasa sidhani utajibu hiyo ndio.

Tuendelee...Kama hapana Mungu hatutegemei...Sasa sisi ametuumba wa Nini??

Mimi binadamu sitegemei Simu ili niishi, lakini nimeunda simu inayowaka,inayotumia chaji,inayotachi(kama binadamu anavyokula na kusali) ili niitumie Kwa faida zangu binafsi kama Kuwasiliana,Kutunza kumbukumbu nk.
Kama simu Haina hizo faida siwezi kuinunua/kuiunda.

Sasa Mungu aliyetuumba sisi wanadamu na hatutegemei, Je ni kwanini alituumba? Tuna faida Gani kwake?

Na most importantly, Je hiyo faida tunayompatia Ina uhusiano wowote na Sababu ya yeye mwenyewe kuwepo???
Upo na maswali mazuri sana, unajitahidi kutoa mifano kabla ya kuuliza ili anayejibu akuelewe vizuri ila nasikitika kukwambia kwamba hayawezi kupata majibu kwa hawa wanadamu wenye fikra ndogo....naamini hata wewe huwezi kujibu maswali haya kwa mujibu wa dini yako labda uyajibu bila kushirikisha dini.

Narudia kusema una maswali mazuri sana na ya kufikirisha zaidi. Majibu ya kuridhisha tutayapata kwa Mungu mwenyewe tukifika
 
Unatafuta nini!?..namaanisha ukijua kwa nini yupo unapata nini?..unahitaji nini katika hilo?
Usimtishe mtoa hoja.
Tafuta jibu aweze kukidhi dukuduku lake.

Mie naamini Mungu yupo. Lakini kwa nondo alizoweka hapo nimejichimbia kusaka jibu
 
Kama kuna faida yeyote anayoipata basi huyo Mungu sio mkamilifu na hajitoshelezi, kwa
sababu kuna vitu ana lack na ili avipate anatuhitaji sisi tumtimizie

Kuna mapungufu makubwa tunayoyaishi kumuhusu Mungu , ambayo yaliwekwa na wezi wachache wenye mamlaka hayo ili kumtambulisha Mungu kwa ajili ya maslai yao binafsi

Mungu tunae muishi ni feki japo kuna kaukwel flani kumuhusu japo mengi tumepotoshwa kwenye vitabu vya din kwa malengo ya watu wachache , upo sahihi kabsa kuona mapungufu ya Mungu kwa maudhui ya mwandishi yalivyomwainisha kwenye vitabu vya din , ila Mungu yupo hata kabla ya chochote ikiwemo din , na watu walipata grace ya kumfahmu wakaweka maono yao katika gumbo mbalimbali kwa lugha tofauti kiyunani kigiriki , kiarabu , kichaga kisambaa na nk , sasa wajanja wachache wakakusanya hayo magumbo na kujumuisha kuwa sehemu moja ili wafanikishe maslai yao

kumbuka hayo magumbo yalifunuliwa kwa watu tofauti na jamii tofauti na tamaduni tofauti na kwa ufunuo tofautina kwa wakati tofautitofauti , na ndio maana unaona kma yanapingana kimantik.
 
Kuna mapungufu makubwa tunayoyaishi kumuhusu Mungu , ambayo yaliwekwa na wezi wachache wenye mamlaka hayo ili kumtambulisha Mungu kwa ajili ya maslai yao binafsi , Mungu tunae muishi ni feki japo kuna kaukwel flani kumuhusu japo mengi tumepotoshwa kwenye vitabu vya din kwa malengo ya watu wachache , upo sahihi kabsa kuona mapungufu ya Mungu kwa maudhui ya mwandishi yalivyomwainisha kwenye vitabu vya din , ila Mungu yupo hata kabla ya chochote ikiwemo din , na watu walipata grace ya kumfahmu wakaweka maono yao katika gumbo mbalimbali kwa lugha tofauti kiyunani kigiriki , kiarabu , kichaga kisambaa na nk , sasa wajanja wachache wakakusanya hayo magumbo na kujumuisha kuwa sehemu moja ili wafanikishe maslai yao , kumbuka hayo magumbo yalifunuliwa kwa watu tofauti na jamii tofauti na tamaduni tofauti na kwa ufunuo tofautina kwa wakati tofautitofauti , na ndio maana unaona kma yanapingana kimantik.
Binafsi sikubaliani na swala la uwepo wa Mungu
 
Shog wewe

Huja jaribu Bado alafu una nambia Ni try it.

Majibu gani italeta?? umesha pata formula ya kutengeneza gari au injini la meli??

Umesha jua kwa Nini mashoga Yana shamiri??
tumia lugha nzuri unapoongea na mimi tafadhali, ndio nimeshajaribu na ndo my lifestyle.
 
Binafsi sikubaliani na swala la uwepo wa Mungu
ni hoja gani zinasababisha usikubaliane ? naomba hoja hizi ziwe nje na taratibu za kidin kwasababu mimi sio mfuasi wa din yoyote .
 
ni hoja gani zinasababisha usikubaliane ? naomba hoja hizi ziwe nje na taratibu za kidin kwasababu mimi sio mfuasi wa din yoyote .
Sio katika perception ya kidini bali katika dhana nzima ya uwepo wake imekaa kimagumashi.

Sababu kuu ni kuwa hakuna uthibitisho wa Mungu kuwepo
 
ALL IS FOR THE BEST IN THE BEST OF POSSIBLE WORLDS.
 
Kama kuna faida yeyote anayoipata basi huyo Mungu sio mkamilifu na hajitoshelezi, kwa
sababu kuna vitu ana lack na ili avipate anatuhitaji sisi tumtimizie
Na kama hapati faida...Inamaana huku kumuabudu,kumsifu,kumlilia,kumuimbia ni kazi bure
 
ukisema yeye, unabinafsisha uwezo mkuu wa nguvu kuu na intelligence kuu iliyoweka mipaka na isiyokua na mipaka , kitu chenye cause lazima kiwe frem na mda flan ambapo pia mda ni illusion , ambayo ni man made illusion.
Kwahyo pasipo binadamu hakuna muda?
Ukifunga nyumba yako ukaondoka, muda pale unaganda? Ukirudi unaganduka?

Kama umeacha chakula wazi nyumbani ukarudi baada ya siku 3 utakikuta kipo vilevile au kimebadilika?

Maana kama hakuna muda basi hakuna mabadiliko. Uwepo wa mabadiliko ndio umeleta muda...Na Huu muda utaendelea kusonga mbele bila kurudi nyuma kwasababu ya 2nd law of thermodynamics, the law of entropy.
Entropy always increases, so time will always go forward.
 
Kulingana na imani za dini, Mungu alikuwepo, yupo na ataendelea kuwepo (haitaji sababu ya nje ili awepo)

Kama hilo jibu halijitoshelezi kwako, basi inabidi uipinge hiyo imani na kukataa kabisa uwepo wa Mungu.
Ukisema Mungu haitaji sababu ya kuwepo, Kwahyo Mungu Hana purpose yoyote kwenye Huu ulimwengu? ....Inamaana hata asingekuwepo, kusingekuwa na Hasara yoyote?
 
Upo na maswali mazuri sana, unajitahidi kutoa mifano kabla ya kuuliza ili anayejibu akuelewe vizuri ila nasikitika kukwambia kwamba hayawezi kupata majibu kwa hawa wanadamu wenye fikra ndogo....naamini hata wewe huwezi kujibu maswali haya kwa mujibu wa dini yako labda uyajibu bila kushirikisha dini. Narudia kusema una maswali mazuri sana na ya kufikirisha zaidi. Majibu ya kuridhisha tutayapata kwa Mungu mwenyewe tukifika
Tuta fikaje huko?
 
Kwa nini JUA lipo? Kwa nini linatokeza Mashariki na kuzama Magharibi na si Kaskazini au Kusini?

Huwezi ukahoji uwepo wa nature au maumbile yake namna ilivyo. Nature inakuwepo tu pasipo ridhaa yako na baada ya hapo unachotakiwa kuhoji ni SABABU ZA UWEPO WAKE na si kwa nini ipo

Kwa mfano, huwezi ukahoji kwa nini wewe umezaliwa mwanamme au mwanamke ila unaweza ukahoji sababu za wewe kuzaliwa mwanamme au mwanamke.

SI KILA SWALI ULILONALO KICHWANI KWAKO, LINA MAJIBU AMBAYO YANAWEZA KUTOLEWA NA MWANADMU
Sawa asante, nimekuelewa....Naomba SABABU ZA UWEPO wa mungu
 
Kwa maoni yangu majibu yatatoka kwenye hii statement yako:

"Kama Kuna ulazima wa ulimwengu kuwepo, basi Inamaana ulimwengu una thamani kuliko Mungu, kama binadamu tulivyo na thamani kuliko viti"

Aliyeumba viti ana thamani kuliko viti, aliyeumba ulimwengu kwann thamani ya ulimwengu iwe kubwa kuliko ya aliyeumba ulimwengu?

Back kwenye swali lako la kwann MUNGU yupo? Turudi kwenye mfano wako wa kiti, kwann kiti kipo? Binadamu anajua ni kwann kiti kipo ila kiti kinajua kwann kipo? Jibu lako linaweza kuwa kiti hakina utashi wala ufahamu hakiwezi kujua kama kipo, kama suala ni utashi na ufahamu, Kama jinsi ambavyo unakifahamu kiti na unafahamu kuwa hakina uwezo wa kukuchunguza wewe uliyekitengeneza sababu hukukipa huo uwezo Na je, alipotuumba alitaka tuwe na ufahamu wa kiwango cha kufahamu kwann yeye yupo? Kama hakutaka na hakutupa kiwango hicho cha ufahamu tutapata jibu la kwann yupo? Kama alitupa kiwango hicho cha ufahamu basi ni suala la muda kufahamu kwann yupo, nyakati zitasema ila kwa sasa bado sababu huenda kuna mengi ya kufahamu kabla ya kufahamu kuhusu sababu za uwepo wake. Huenda tukifahamu siri ya kifo tutajua kuhusu uwepo wa MUNGU.

Concept ya MUNGU kwann ipo? Ipo kwa sababu ya baadhi ya majibu ambayo binadamu anayahitaji ila hana hivyo anajikuta anamtafuta MUNGU, ni suala la kiimani. Mpaka pale majibu yatakapopatikana ndipo hii imani inaweza kupotea. Sasa sababu ni suala la imani utalijadili vipi nje ya imani? Na ukiweka imani jibu la swali lako ni simple sana, Sisi tupo kumwabudu aliyetuumba na fikira zetu ni ndogo sana kuuchunguza sababu za uwepo wake. Hata ukiwa na midomo elfu moja na zaidi huwezi kumaliza kuuzungumza ukuu wake. Jibu la kiimani.
Mfano wangu wa kiti hukuuelewa...Hapo nilisema hivyo kuwa
"Kama Kuna ulazima wa ulimwengu kuwepo"
Nikimaanisha Kwa wale wanaosema Sababu ya Mungu kuwepo ni ili auumbe ulimwengu na kuusimamia.

Sasa ndo nikasema, kama Main purpose ya Mungu ni kuumba ulimwengu, Inamaana ulimwengu ndio umemleta Mungu.

Ni sawa na gari lilivyomleta dereva....aliegundua gari wa kwanza hakuwa dereva, ila baada ya kulitengeneza ndio tumepata fani ya madereva ambayo Leo hii watu wanaishi Kwa udereva.

Ndio maana nikasema
"kama binadamu tulivyo na thamani kuliko viti"
Nikimaanisha, kama shida yetu ya kukaa imetuletea viti, Ndio kama jinsi shida ya ulimwengu ulitakiwa uwepo ukasababisha Mungu awepo kwaajili ya kuuteneneza, Basi huo ulimwengu ndio umemleta Mungu.
Kama sisi binadamu tulivyovileta viti.
 
na kwanini yupo?
Kwa nini JUA lipo? Kwa nini linatokeza Mashariki na kuzama Magharibi na si Kaskazini au Kusini? Huwezi ukahoji uwepo na maumbile ya nature. Nature inakuwepo tu pasipo ridhaa yako na baada ya hapo unachotakiwa kuhoji ni SABABU ZA UWEPO WAKE na si kwa nini ipo

Kwa mfano, huwezi ukahoji kwa nini wewe umezaliwa mwanamme au mwanamke ila unaweza ukahoji sababu za wewe kuzaliwa mwanamme au mwanamke.

SI KILA SWALI ULILONALO KICHWANI KWAKO, LINA MAJIBU AMBAYO YANAWEZA KUTOLEWA NA MWANADMU
Sawa asante, nimekuelewa....Naomba SABABU ZA UWEPO wa mungu
Sababu pekee ya uwepo wa Mungu ni Ibada!
Asingekuwepo; wewe pia usingekuwepo. Mungu yupo ili mimi na wewe pamoja na viumbe vingine, vilivyopo, vinavyoonekana na visivyoonekana, tuweze kumwabudu.
Ni Mungu pekee anayestahili kuabudiwa
 
Sio katika perception ya kidini bali katika dhana nzima ya uwepo wake imekaa kimagumashi.

Sababu kuu ni kuwa hakuna uthibitisho wa Mungu kuwepo
ni kitu gani kilichopangilia mfumo wa fahamu , mfumo wa mmengenyo wa chakula , na nk je huo mpangilio hauna intelligence ya aina yoyote?

je unafikiri ni nini kilisababisha vitu viwepo kwenye mfumo maalumu na kwasababu maalumu je vipo tu bila nguvu yoyote? na sababu za kuwepo ni nin ? ili iweje ? na je vyote unavyoviona vime arise kutokea wap na kwa nguvu ipi?
 
Back
Top Bottom