Kwanini Mramba, na si Chenge, Lowassa, Tibaijuka na Muhongo?

Kwanini Mramba, na si Chenge, Lowassa, Tibaijuka na Muhongo?

Watu wa kaskazini hasa wachagga tumekiona cha moto utawala huu wa Kikwete.
 
Mimi sio ccm, lakini kuna wakati tuwe wakweli. Kwani muhongo ameiba nini? Au tibaijuka? Chenge, ngeleja sawa. Lakini hawa wawili ni nini? Maana muhongo hakutajwa popote, tibaijuka aliomba hela na akaikabidhi bodi ya shule
Hata akina Mramba hawakuiba bali walitumia madaraka vibaya kuisababishia hasara serikali
 
Jiulize mafisadi Idris Rashid, Mustafa Mkulo, Juma Kapuya na Ramadhan Dau hawaguswi
 
Kwanza kesi yenyewe imechukua muda mrefu sana, miaka 9! Halafu adhabu kiduchu.
 
Wabongo hawana jema,Mahakama ingewaachia huru wangesema wanalindana Imewafunga pia wanahoji mbona wengine hawajafungwa??

Kila siku watu wanalalalmika humu kuwa huko magerezani wamejaa wezi wa kuku lakini vigogo wanalindana; vigogo wanaposwekwa lupango pia wako wengine wanawaonea huruma kana vile hayo mabilioni wanayoiba huwa wanawagawia!!! Mramba ilibidi afungwe ili laana ya kuwaambia wananchi wale majani ihitimishwe!! Sasa yeye anakwenda kunyea ndoo hata akijapata msamaha atakuwa amenyooka.
 
Mpwa ukianza kuuliza maswali kama hayo utakuta kuwa wote ni wezi, sio JK tu hadi hao wengine, kichekesho ni pale mwizi anapomfunga mwizi mwenzie
Kibo10
 
Last edited by a moderator:
Kibo10

Hakuna anaeupenda ufisadi labda fisadi mwenyewe..lkn sheria kwa asieijua ina miujiza yake.."uhalifu ktk jicho la sheria unaweza kuwa tofauti kabisa na uhalifu ktk jicho la siasa".....!tusaidiane kuleta ushahidi wa kisheria ili kuwatia hatiani hao wote ambao wanatajwa kuwa ni "mafisadi" vinginevyo hayo madai yatakuwa ama ni majungu ya kisiasa, au kelele za kumsaidia mwizi ajifiche vizuri.

Mtikila(mchungaji???!!) alikuwa akituambia, na tukamuamini, kuwa mla rushwa namba moja ktk serikali ya Mkapa ni Sumaye...lkn miaka ya karibuni ametuambia tena kuwa Sumaye alikuwa kiongozi msafi!
.....
 
Last edited by a moderator:
Jiulize mafisadi Idris Rashid, Mustafa Mkulo, Juma Kapuya na Ramadhan Dau hawaguswi

Ramadhani Dau anastahili kupandishwa kizimbani kwa kosa la kutumia madaraka vibaya na kuifilisi NSSF!!! Nashangaa katika orodha ya yule YUDA Escariot ya wenye fedha nje ya nchi majina ya Chenge na Idris Rashid hayamo ili hali waingereza walizifichua account zao !!!! Zitto ni mnafiki na sio mkweli!
 
kibo10 inabidi tukusamehe maana hujui unenalo..kwa maana nyingine wewe ni zuzu
Kibo10;
 
Last edited by a moderator:
Mramba anajuwa siri chache chenge anajuwa siri zaidi ya elfu na el pia!!
 
Kwa mtazamo wako, je unaona tuhuma za hao watu zinafanana?
Tuhuma za hawa watu hazifanani tena za hawa wakina Mramba naweza kusema tuhuma na makosa yao ni madogo ukiringanisha kiwango cha fedha walichokitia kwa serikali kwani ni Billion 11, Siwatetei akina Mramba lakini ebu tuangalie viwango vingine vya fedha ambavyo serikali imepata hasara.
EPA - Billion 133
RICHMOND - Billion 122
ESCROW - Billion 312
CHENGE na Kashfa ya RADA
Kashfa ya VODACOM - Billion 700
na kuna nyingine za KAGODA, MEREMETA, ununuzi wa Mabehewa mabovu, Idara ya miundombinu Billion 256.

Zaidi ikumbukwe hadi sasa bado tunalipa Million 152 kwa siku IPTL.
Hawa wote waliohusika na kashfa hizi wengi wao waliishia kujiuzuru nyazifa zao au kuondolewa na Rais au kuhamishwa Wizara.

Ninachokiona mimi kwa hiki alichokifanya Kikwete ni kuingiza mgogolo wa kiuongozi kwani tutarajie Rais ajae na yeye lazima hawa wote wenye kashfa hizi nilizoziorodhesha hapa juu watashitakiwa na hii ndio itakuwa fedheha kubwa kwa Kikwete na utawala wake kwani kama alikuwa na nia njema ya kutoa hukumu kwa hawa watu haikutakiwa kuchukua miaka 9 eti mwaka anaomaliza uongozi wake ndio hukumu inatolewa.
 
fisadi lowasa atakuwa anatumia majini ndio maana yeye ashitakiwi
 
Mimi sio ccm, lakini kuna wakati tuwe wakweli. Kwani muhongo ameiba nini? Au tibaijuka? Chenge, ngeleja sawa. Lakini hawa wawili ni nini? Maana muhongo hakutajwa popote, tibaijuka aliomba hela na akaikabidhi bodi ya shule
na bodi ya shule wakanunua mboga na nyingine wakanunua hisa mkombozi bank
 
Kibo10

Hahaaaa inategemea comandoo wa ESCROW NANI AZAWAISI UNAWEZA IFUNGA SERIKALI...
 
Last edited by a moderator:
Kuna kitu hakiko sawa!!

issue tunataka watu wajue ccm inapambana na ufisadi. Hiki ni kiini macho, na wameamua kuwatoa kafara kipindi hiki cha uchaguzi. Ni zuga tu na kuwahadaa watz.
 
Mimi sio ccm, lakini kuna wakati tuwe wakweli. Kwani muhongo ameiba nini? Au tibaijuka? Chenge, ngeleja sawa. Lakini hawa wawili ni nini? Maana muhongo hakutajwa popote, tibaijuka aliomba hela na akaikabidhi bodi ya shule

sasa kwa nini walijiuzulu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom