kibogo
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 9,739
- 4,746
Mimi sio ccm, lakini kuna wakati tuwe wakweli. Kwani muhongo ameiba nini? Au tibaijuka? Chenge, ngeleja sawa. Lakini hawa wawili ni nini? Maana muhongo hakutajwa popote, tibaijuka aliomba hela na akaikabidhi bodi ya shule
Jitahidi kuwa na uelewa mpana na kujua Mramba na Yona wamehukumiwa kwa kosa gani, hawa watu wamehukumiwa kwa kosa la kuisababishia hasara Serikali kwa kuruhusu misamaha ya Kodi je hawa waliohusika na masakata ya EPA, RADA,MEREMETA,KAGODA,RICHMOND na ESCROW wewe kama wewe unawaweka kundi gani? kwa nini hakuna hatua stahiki zilizochukuliwa kuwatia hatiani? na cha ajabu wale wa EPA rais mwenyewe alitamka hadharani kuwa warudishe hizo fedha ingawa hatujui kama walirudisha na ni akina nani na je kwa nini Rais aliwaficha hawa watu na hawakutajwa hadharani?