Salam mtoa mada,
Kwanza napenda kuweka wazi kwamba mimi ni mwanasheria na wakili na napenda kutoa mchango wangu hapa kwenye hii mada yako kama ifuatavyo ili tu tusaidiane kielimu na kimawazo. Na napenda kudeclare interest pia kuwa mie ni mtu ninayempenda na kumshabikia Prof Muhongo.
Napenda kuungana na wewe kwenye uzi wako kwa upande wa chenge kwa sababu kwa ushahidi ni maeneo mengi chenge aliingiza chaka serikali na kuisababishia hasara na hata kwa ushahidi unaoweza kujengwa kirushwa chenge anapatikana na hatia bila ya shaka.
Ila napenda nitofautiane na wewe kidogo kwa upande wa Tibaijuka na Lowassa. Kwa Tibaijuka najua utapata shida kuamini ila huu ndo ukweli kuwa, criminaly ni ngumu sana kusema kuwa ana hatia yeyote ile iwe either kuipa hasara serikali au kupokea rushwa, nakueleza kwa nini, Luge alimpa ile hela tibaijuka akiwa waziri wa ardhi,sasa ili uweze kucreate mazingira ya rushwa hapo ni lazima ujenge hoja kuwa kama waziri wa ardhi alimsaidia nini Luge? Na ukiangalia suala la escrow lilikuwa na Nishati na Madini, if Tibaijuka angekuwa waziri wa Nishati na Madini basi hapo mojamoja ingekuwa rahisi sana hata kutengeneza mazingira ya rushwa au kuitia hasara serikali. Kosa kubwa la Tibaijuka lilikuwa la kimaadili yaani kutodeclare pale alipopokea zile hela. Sasa hapa kama kosa la kimaadili lingekuwa na adhabu ya jela basi obvious Mama Tibaijuka nae angekuwa mtarajiwa wa Ukonga.
Niende kwa Lowassa, Mungu anisamehe, kusema kweli namchukia Lowassa na siamini kama ni kiongozi wa kulivusha hili taifa na kulipeleka linapotakiwa kuwa ila kwenye richmond kama mwanasheria lazima niseme ni ngumu kusema kuwa aliingizia hasara serikali kwa sababu records zinaonesha Richmond haikulipwa hata senti tano, if ingetokea Richmond imelipwa hela basi leo Lowassa nae angekuwa mtarajiwa ukonga, napo kwenye Rushwa hatukuonyeshwa ni wapi Lowassa alihongwa so hapo ndo utata unapokuja.
Tuje kwa Prof Muhongo sasa, hapo ndo sijui niseme umekosea au ulilishwa matango pori ndugu yangu kwa sababu hoja yako dhidi yake haina mashiko. Kwenye ripoti zote za uchunguzi no where wamesema Prof Muhongo ndo aliyetoa ruhusa au amri zile hela zitolewe. Ripoti zote zimemtaja Mwanasheria Mkuu kuwa ndo mtu aliyesema BOT ilipe zile pesa tena kwa maandishi na ndo aliyesema kuwa hata kodi isilipwe. Kwenye ripoti zote pia no where Muhongo ametajwa kupokea hata senti tano kutoka kwa mtu yeyote yule. Sasa hapo inaonesha kuwa umekosea kumuweka Muhongo hapa, labda kama ulimweka kinafki tu kwa sababu humpendi na unamchukia. Sasa kwenye hili suala kama hasara basi wa kushtakiwa atakuwa Werema na yeye ndo mtarajiwa wa Ukonga kwenye hili suala. Hata maswi ni ngumu sana kuwa na ushahidi wa kumfunga kwa sababu records zinaonesha in good faith alijibu sana kupata uhakika na uthibitisho makini tena kwa maandishi kama zile hela zilipwe au la.
Sasa kwenye kichwa chako cha habari ungewaweka chenge, Werema na labda kina Karamagi