MESTOD
JF-Expert Member
- Nov 12, 2010
- 4,798
- 2,008
Dah jamani pole sana ila wengine tunaijua miziki yote ya mama wa kambo na mashangazi aiseeh acha kabisa yaani hii unaambiwa weka mbali na watoto aiseeh!!!!
Aisee acha tu. Miye maza wa kambo ilikuwa vipigo bila kosa. Majirani wakaingilia kati nikapelekwa kwa bibi kijijini. Huko nimekaa wakanambia (miaka hiyo) kuwa kwa mazingira haya huyu hawezi kufaulu, so nikahamishiwa kwa aunt. Hapo ndo niliona mziki. Unaamka saa kumi na moja unafanya kazi zoote za ndani (leo naona ilikuwa sawa tu maana leo hivyo vitu havinisumbui), aunt akiamka akukute hujaondoka shule hata kama ulikuwa na kazi nyingi anakutimua bila chai. Mchana unarudi msosi bado unaogopa fimbo za kuchelewa unaosha. Acheni Mungu aitwe Mungu, kwani kati kati ya njaa kali unakuta rafiki anakupa andazi. Usiku unafanya kazi mpaka karibu saa sita.
The thing ambayo sitasahau ni baada ya mama yangu kufariki nikiwa kwa aunt mkoa mwingine. Wiki moja baada ya aunt kupewa taarifa aliniuliza 'eti ukisikia mama yako amekufa utafanyaje?'. Nikamwambia sijui, akasema basi mama yako amekufa, at that time nikiwa darasa la nne. Niliingia chumbani nikalia sana. Alivoona nalia alinivurumushia matusi na sikuruhusiwa kwenda hata kuliona kaburi la mama yangu. From that day niliapa sitazaa mtoto nje ya ndoa Mungu anisaidie katika hili. Wanawake huwezi kuwaelezea, huwezi jua rangi zao. Utakapofikiri ni nyeupe kumbe ni nyekundu.
Ila good thing mama wa kambo alibadilika sana though nilikuwa namuogopa she was so nice to me nikiwa form two hadi leo. Aunt alikuwa tia maji tia maji hivyo hivyo ila leo mimi ndo nimekuwa msaada mkubwa kwao, na sina kinyongo now! I really love them maana pamoja na yote nilipata fursa ya shule.