Kwanini Mama wa Kambo huwa na Visa?

Kwanini Mama wa Kambo huwa na Visa?

Nimesikia story ya mama wa kambo aliyemkata mtoto wa mmewe dudu yake nikaona niweke post ya experience yangu na akina mama wa kambo.

Nakumbuka mdingi alimtema mama angu mzazi alikuwa anamzingua sana mimi nikiwa na miaka kama tano hivi, akavuta mama aliyetulea. Mbona tulionja joto ya jiwe? Unadhani mama wa kambo alinifanya mazuri basi? Mdingi alikuwa anasafiri sana.

Yaani home alikuwa anakaa siku moja au mbili anasafiri halafu huko anakaa hata wiki tatu mpaka sita. alikuwa na wamama wengine huko. Kimaisha hali haikuwa mbaya sana kwani hapo home kulikuwa na lorry tani saba enzi hizo yalikuwa machache sana, kwa hiyo ni full kazi na jumba kuuuubwa ambalo enzi hizo tulikuwa tunaona kama hekalu.

Home store ya misosi ipo full muda wote, mikaa na kuni imejaa kwenye stoo yake kwa sababu kila gari ikisafiri lazima ilete aidha mkaa, kuni, mahindi, mpunga, maharage, kuku, au nyama ya porini. Wakati mwingine vitu kadhaa kati ya hivyo vililetwa kwa pamoja.

Cha ajabu hapo home tulikuwa tunashinda njaa mpaka jioni ndio tunakula! Yaani maskini ya mungu mi sijui hata kosa nililomfanyia huyo mama I was only 5 years old, nashinda na njaa wakati ndani kuna chakula cha kutosha. Wanapewa majirani, vingine vinamwagwa, mi nashinda na njaa mdomo umekaukaaaaa! Siku mshua akirudi ndio napewa kipande cha nyama cha kuzuga.

Akiondoka kesho yake napikiwa maharage ya kula hata siku nne sikumbuki kama hata chumvi yalikuwa yanawekwa yale, na nakula jioni tu, mchana napigishwa pasi ndefu, wakati mdingi ana mahela kibao. Nimepiga hizo since 5 years old mpaka std 7 baada ya kuanza sekondari mateso yalianza kupungua kidogo kidogo.

Acheni utani nyie watu. Kulikuwa na mtoto wa kaka ake hapo home ambaye yeye (maza) ndio alikuwa anasema mwanae, huyo ndio alikuwa anaishi kama mfalme. Akawa anatuonea huruma, akipewa nyama, akipata upenyo anatufichia.

Anajifanya amekula zote baadae tukienda kulala ndio tunakula kitandani huku tumejifunika blanket maza asituone mimi na wenzangu waliokuwapo siku hiyo, hasa ndugu ndugu. Mateso makubwa yalikuwa njaa na vipigo. ​Kakosa kadogo unatandikwa mpaka unajikojolea halafu no msosi siku hiyo.

Siku ambayo siwezi kusahau ni ile ambayo njaa na tamaa viliponizidia nikadokoa nyama aliyokuwa anamuandalia mwanawe. Weee! Alinipa kichapo mpaka nika-faint. Nilipozinduka (hii ndio itafanya nije niue mwanamke siku moja) akanishika mdomo wangu akaniachamisha kwa nguvu halafu akanitemea mate ya kutosha humo.

Sijui yalikuwa makohozi yale, nakumbuka nilitapika mpaka kidogo niteme maini. Nadhani nilifaint, kwa sababu nilikuja shtukia naamshwa asubuhi niende shule tu wakati kipigo kilikuwa jana yake saa mbili usiku nilikuwa std 3.Nakumbuka hata shule sikuenda siku hiyo, nilianza safari ya kwenda kumtafuta mama yangu kwa mguu na hata sijui wapi.

Nilifuata uelekeo flani ambako ndio najua magari ya anakotokea mama angu yanaelekeaga. Nilipoenda kama kilometa tano Wasamaria wakaanza kushangaa huyu mtoto anaelekea wapi wakaanza maswali, nilipowaambia nimetoka wapi na ninaenda wapi na kufanya nini wakanikamata wakanirudisha mpaka home.

Sasa pale tunafika karibu na home akatokea mama mmoja kwa kumbukumbu zangu za wakati huo alikuwa anafanana na mama yangu) nilimrukia vibaya mpaka waliokuwa wananirudisha home wakashangaa. Sasa yule mother aliposema mimi sio mwanae wakakomaa nae mpaka wakapaone nyumbani kwake, tukaenda wote mpaka hapo sio mbali na hapo home kwetu.

Alikuwa ndio amehamia mitaa hiyo hiyo siku si nyingi hivyo nilikuwa sijawahi muona) waliporidhika, na mimi baadae nilipokubali kwamba sio mama yangu wakanirudisha kule home kabisa. Ila niliona aibu sana baadae nilipokuja tambua sasa kuwa yule niliyemkumbatia vile wala sio mama yangu. Yule mama alikuja kunipenda
mpaka nakuwa mtu mzima.nadhani huruma ilichangia kwa maisha aliyokuwa anaona naishi.

Ninachotaka kusema ni kwamba muziki wa mama wa kambo mi naujua fresh tu, toka 5 yrs old mpaka form six. Mengine mengi tu inabidi niya-skip kwa sababu story itaboa.

 
Pole sana mkuu mama wa kambo ni nuksi mm wazazi walitengana na baada ya mm std 4 nikarudishwa kwa baba nikamkuta mama wa kambo alinitesa mwanzo baadae nilikuwa namchapa makofi tu hawafai kibaya sikutaka mwanangu aje alelewe na mama wa kambo
 
Hili ni somo tosha kwa familia zenye mama wa kuja! "akina baba wenye wa mama wa kudandia gari moshi kwa nyuma' kuweni makini ndani ya nyumba zenu"*MAMA WA KAMBO NUKSI, ...ingawaje si wote wenye tabia mbaya!*
 
Dah jamani pole sana ila wengine tunaijua miziki yote ya mama wa kambo na mashangazi aiseeh acha kabisa yaani hii unaambiwa weka mbali na watoto aiseeh!!!!
 
Dah,naona wote mmeshambulia sana hawa wamama. Lkn nawafahamu watu ambao wamelelewa na mama wa kambo vizuri hadi Kuwa watu wa maana sana hapa duniani. Kwa ufupi sio mama wa kambo wote ni wabaya.
 
Wanawake kiwanja chetu motoni kimeongezwa! tutachomwa kuliko tanuru! uzuri wa hii dunia, hakuna jambo utakalofanya uache kulipwa! jema hulipwa, na baya hulipwa! so mama wa kambo, mashangazi stay tuned!
 
Siyo wote aisee mimi mama yangu amewalea kaka yangu na dada yangu ambao ni watoto wa kufikia cha ajabu baba alikuwa mkari na mchumi kwa hyo dada na kaka walikuwa wakitaka vifaa vya shule wanapitia kwa mama na mpaka leo hii kaka yetu ndiye anayeilea familia na wote tunapendana utafikiri tumezaliwa baba mmoja na mama mmoja.
 
Sijawahi kuishi na mama wa kambo, ila ninavyojijua nahisi angekiona cha mtema kuni, huyo dingi tu wakati nipo la 4 akaanza kunizungua na mambo yasiyoeleweka, siku nikayachoka nilichoanza kufanya mbona alitulia na tangu hapo alikua makini na mimi. Kuna wazazi wanafanya makusudi kabisa kuwachokoza watoto wao, eti we utulie uwe na heshima, aisee mi ilinishinda nikapasua ukweli, na mambo ya kawa shwari.

So who is mama wa Kambo, nashukuru tu sijaishi na hao wa mama, hadi leo ni mtu mzima, na even hata ikitokea now najua hawezi nitesa mimi, na ole nisikie anawatesa wadogo zangu kudadadeki, baba atajua kama amemuoa yeye au nimemuoa mimi. Waende zao huko
 
Dawa ya mama wa kambo ni kusoma kwa bidii kama upo primary soma kwa bidii, kama upo sekondari au chuo kaza buti sana, mimi naye ni muhanga wa mama wa kambo ila Mungu ni mkubwa nilisoma kwa uchungu na bidii kubwa kwa ku-recall mateso aliyopata mama yangu toka kwa mzee na baada ya kutengana maisha aliyoishi mama yangu, kwa hiyo dawa pekee ya kuwamaliza hawa ni kusoma tu kwa bidii kubwa.
 
Dont go away

Exactly...nimeshuhudia ndugu zangu wengine katika ukoo wetu wanapata shida sanaaa sabab ya hawa mama wa kufikia...namshukuru sana Mungu wazazi wangu wako pamoja mpaka leo hii nd that im already a grown big man, sikupitia hayo maisha...ila hua inaniumaga sana mwanamke anavyo mnyanyasa mtoto wa mwanamke mwenzie ukicheck bado mtoto ni mdogo mno.

Inaniumaga sanaa roho...nd nikaji promise kitu that watoto wangu hata siku moja sitokubali wapate shida as long as i breathe. Mungu anisaidie sanaa.
Seriously ivi unaanzaje kumnyima mtu chakula ilhali kimejaa kibao kingine kinamwagwa. Dah
Kweli tumeumbwa tofauti...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom