Kwanini lugha ya Kiswahili haitumiki kufundisha kwa ngazi zote za kielimu?

ASIWAJU

JF-Expert Member
Nov 18, 2022
1,939
1,625
20230130_201350.jpg


Maswali kwa Wizara ya Elimu Tanzania na kwa wadau wote humu Jamiiforums:

Kwa kuzingatia takwimu za matokeo ya kidato cha nne 2022.

1. Kwanini wizara haijaamuru matumizi ya lugha ya kiswahili katika kufundisha na kuondoa matumizi ya lugha ya kiingereza katika ngazi zote za kielimu hapa nchini?

2. Je, Serikali inafahamu madhara ya kufundisha kupitia lugha isiyo na matumizi makubwa na kuacha lugha yenye utumizi mkubwa katika taifa?

3. Kwanini kuna matumizi ya lugha ya Kiingereza katika kufundishia huku mazingira ya kazi yakihitaji zaidi matumizi ya lugha ya kiswahili?

4. Kwanini Kiingereza kisibaki kama yalivyo masomo mengine kama Kichina, Kifaransa, Bailojia, Fizikia, Kemia n.k
 
View attachment 2500540

Maswali kwa Wizara ya Elimu Tanzania na kwa wadau wote humu Jamiiforums:

Kwa kuzingatia takwimu za matokeo ya kidato cha nne 2022.

1. Kwa nini wizara haija amuru matumizi ya lugha ya kiswahili katika kufundisha na kuondoa matumizi ya lugha ya kiingereza katika ngazi zote za kielimu hapa nchini ?

2. Je serikali ina fahamu madhara ya kufundisha kupitia lugha isiyo na matumizi makubwa katika na kuacha lugha yenye utumizi mkubwa katika taifa ?

3. Kwa nini kuna matumizi ya lugha ya kiingereza katika kufundishia huku mazingira ya kazi yaki hitaji zaidi matumizi ya lugha ya kiswahili ?

4. Kwa nini kiingereza isibaki kama yalivyo masomo kama Kichina, kifaransa, bailojia, fizikia,kemia n.k
Bado sanaa,kufikamoo🤔,kwani yale ya msingi sana tunayashindwa.
 
Kwa mtazamo huo wengine watataka kutumia lugha zetu za kibantu ambazo ziko kwenye damu😂😂 (kisukuma,kimakonde,kinyakyusa,kimatemwe.. n.k)💪🇹🇿👍
Kiswahili chenyewe ni shida..REJEA matokeo ya shule za msingi darasa la nne na la saba ambako wanafunzi hufundishwa kwa kiswahili. Naona kuna shida ya kuwasilisha maarifa kwa lugha husika. Tuna mikakati ya kusambaza kiswahili kwenye mataifa mengine wakati sisi hatutaki lugha za kigeni😶😶.Jiulize kwa nini hakuna tution ya lugha ya kihindi....
 
Kwa mtazamo huo wengine watataka kutumia lugha zetu za kibantu ambazo ziko kwenye damu😂😂 (kisukuma,kimakonde,kinyakyusa,kimatemwe.. n.k)💪🇹🇿👍
Kiswahili chenyewe ni shida..REJEA matokeo ya shule za msingi darasa la nne na la saba ambako wanafunzi hufundishwa kwa kiswahili. Naona kuna shida ya kuwasilisha maarifa kwa lugha husika. Tuna mikakati ya kusambaza kiswahili kwenye mataifa mengine wakati sisi hatutaki lugha za kigeni😶😶.Jiulize kwa nini hakuna tution ya lugha ya kihindi....
Ningependa tuzungumzie zaidi Kiswahili na Kiingereza kwa kuzingatia zaidi takwimu za matokeo ya kidato cha nne 2022.
 
Ningependa tuzungumzie zaidi Kiswahili na Kiingereza kwa kuzingatia zaidi takwimu za matokeo ya kidato cha nne 2022.
Zianzishwe sekondari za "Swahili medium" zipambane na hizi za "English medium" tuone mziki wake.
Shida iko kwenye jinsi ya kutoa maarifa.
Wale wa private schools mbona hawana shida hiyo ...mfano S0295 PRECIOUS BLOOD SECONDARY SCHOOL,wanafunzi wote 94 wamepata division ONE...👇👇👇

Watanzania wengi wamesoma nchi za nje kwa kutumia lugha za huko na kufaulu vizuri.
 
Zianzishwe sekondari za "Swahili medium" zipambane na hizi za "English medium" tuone mziki wake.
Shida iko kwenye jinsi ya kutoa maarifa.
Wale wa private schools mbona hawana shida hiyo ...mfano S0295 PRECIOUS BLOOD SECONDARY SCHOOL,wanafunzi wote 94 wamepata division ONE...👇👇👇

Watanzania wengi wamesoma nchi za nje kwa kutumia lugha za huko na kufaulu vizuri.
Sawa
 
View attachment 2500540

Maswali kwa Wizara ya Elimu Tanzania na kwa wadau wote humu Jamiiforums:

Kwa kuzingatia takwimu za matokeo ya kidato cha nne 2022.

1. Kwa nini wizara haija amuru matumizi ya lugha ya kiswahili katika kufundisha na kuondoa matumizi ya lugha ya kiingereza katika ngazi zote za kielimu hapa nchini?

2. Je serikali ina fahamu madhara ya kufundisha kupitia lugha isiyo na matumizi makubwa na kuacha lugha yenye utumizi mkubwa katika taifa?

3. Kwa nini kuna matumizi ya lugha ya kiingereza katika kufundishia huku mazingira ya kazi yaki hitaji zaidi matumizi ya lugha ya kiswahili?

4. Kwa nini kiingereza kisibaki kama yalivyo masomo mengine kama Kichina, kifaransa, bailojia, fizikia, kemia n.k
NCHI YA AJABU SANA DUNIA YOTE LUGHA KUU NI KIINGEREZA nyie mnakomaa na KISWAHILI
juzi Wanafunzi wa LAW SCHOOL wamefeli vibaya Tume imeundwa imekuja na majibu kuwa LUGHA ya Kiingereza ni TATIZO KUBWA leo mnataka KISWAHILI haikosi mnataka KUTUNGA MASHAIRI ?
 
NCHI YA AJABU SANA DUNIA YOTE LUGHA KUU NI KIINGEREZA nyie mnakomaa na KISWAHILI
juzi Wanafunzi wa LAW SCHOOL wamefeli vibaya Tume imeundwa imekuja na majibu kuwa LUGHA ya Kiingereza ni TATIZO KUBWA leo mnataka KISWAHILI haikosi mnataka KUTUNGA MASHAIRI ?
Wewe mwenyewe umekiri hapa kuwa lugha ya kiingereza ni tatizo, kwa nini sasa kina endelea kutumika kama ni tatizo ?

Dunia gani lugha kuu ya kufundishia kwa mataifa yote ni kiingereza ? Au Japan, France, Germany, China, Russia, Vietnam, Malaysia, Korea wao hawapo dunia hii ?
 
Back
Top Bottom