Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Lowasa ni fisadi hawezi kupambana na yeye mwenyewe.Anakuja kutununua kwa pesa alizotuibia
 
Watanzania wenzetu sijui nani katuloga. Mbona tunasahau mapema sana kiasi hiki. Hivi leo tumesahau kuwa chanzo kikuu cha ufisadi hapa nchini ni mfumo uliopo serikalini?

Swali dogo naomba kuuliza:

Ni waziri mkuu gani mwenye rekodi ya kipekee ya kuwa mkali zaidi tena kwa vitendo kwa watendaji wa serikali? Sio Lowassa huyu huyu aliekaa madarakani kama mtendaji mkuu wa serikali kwa muda mchache zaidi, na ndie huyu aliweka rekodi ya kuwa mkali zaidi kwa watendaji wa serikali wanaopenda kufanya kazi kwa mazoea?

Ni waziri mkuu yupi aliekuwa na uwezo wa kumwajibisha mkuu wa wilaya on the spot? Halafu leo mnasema Lowassa hajawahi kupambana na ufisadi!

ninaungana nawe kabisa kwenye hoja yako ya utangulizi niliyo highlight in RED. Wewe mwenyewe una tatizo hilo hilo la kusahau mapema......maana jibu la swali lako juu ya Waziri Mkuu gani mwenye rekodi ya kipekee ya kuwa mkali zaidi, tena kwa vitendo kwa watendaji wa Serikali- Jibu sahii ni EDWARD SOKOINE

jambo la pili, muhimu kuclarify.....UFISADI na UZEMBE japo vyote vinaathiri maendeleo ya nchi, ni vitu viwili tofauti. Mifano uliyotoa kwenye uzi wako ni rekodi ya Mhe Lowassa kushughulikia UZEMBE, na sio kushughulikia UFISADI.

Ni kweli kabisa kwamba mifumo Serikalini inaweka mazingira ya kulea rushwa.....kwa mfano.....Maslahi duni Serikalini, hupelekea baadhi ya wauguzi au mapolisi kuchukua rushwa....na hizi ndio rushwa zinazowakera na kuwaumisa wananchi kila siku mijini na vijijini- ningetegemea kuona mifano ya Mhe Lowassa alivyotetea kuboresha maslahi ya watumishi wa umma.

mfano mwingine wa mfumo wa Serikali unaochochea rushwa upo kwenye sheria zilizopo....mfano Sheria ya Manunuzi ya Umma......Mhe Lowassa na Wagombea wengine wote wanaojipambanua na rushwa, wamechukua hatua gani (wakiwa kama Wabunge) kupendekeza mabadilisho ya sheria hiyo na nyinginezo kuziba mianya ya rushwa?

Tatizo lingine lililopo ni rushwa kubwa (Grand Corruption)- ununuzi wa Rada, Deep Green, EPA, Land grabbing ni mifano michache- ni vema rekodi za wanaojipambanua na rushwa zikapimwa kwa hatua/misimamo walioyochukua kushughulikia na madhira haya.

Nimalizie kwa kueleza maoni yangu na swali kwa Mhe Lowassa. Sina shaka yoyote na uwezo wa Mhe Lowassa kuongoza nchi; Sina shaka yoyote juu ya dhamira ya Mhe Lowassa kuona nchi hii inasonga mbele kwa kasi zaidi.

Swali langu ni je atawezaje kuwakwepa baadhi ya watu wanaomzunguka ambao hawana uwezo na dhamira njema kama yake- baadhi yao rekodi zao za utendaji na uadilifu ni za kutiliwa shaka?

Kwenye kundi lake kuna walioshiriki kikamilifu kwenye GRAND CORRUPTION, kuna watu wenye rekodi za kukwepa kodi na kuinyima serikali mapato zinafahamika wazi. Je watu hawa wana share njozi yake ya matumaini kwa watanzania wote au wataendelea na njozi yao ya matumaini kwao peke yao?

Anawatosaje watu hawa? Haya maswali watanzania wengi wangependa kujua!
 
ninaungana nawe kabisa kwenye hoja yako ya utangulizi niliyo highlight in RED. Wewe mwenyewe una tatizo hilo hilo la kusahau mapema......maana jibu la swali lako juu ya Waziri Mkuu gani mwenye rekodi ya kipekee ya kuwa mkali zaidi, tena kwa vitendo kwa watendaji wa Serikali- Jibu sahii ni EDWARD SOKOINE

jambo la pili, muhimu kuclarify.....UFISADI na UZEMBE japo vyote vinaathiri maendeleo ya nchi, ni vitu viwili tofauti. Mifano uliyotoa kwenye uzi wako ni rekodi ya Mhe Lowassa kushughulikia UZEMBE, na sio kushughulikia UFISADI.

Ni kweli kabisa kwamba mifumo Serikalini inaweka mazingira ya kulea rushwa.....kwa mfano.....Maslahi duni Serikalini, hupelekea baadhi ya wauguzi au mapolisi kuchukua rushwa....na hizi ndio rushwa zinazowakera na kuwaumisa wananchi kila siku mijini na vijijini- ningetegemea kuona mifano ya Mhe Lowassa alivyotetea kuboresha maslahi ya watumishi wa umma.

mfano mwingine wa mfumo wa Serikali unaochochea rushwa upo kwenye sheria zilizopo....mfano Sheria ya Manunuzi ya Umma......Mhe Lowassa na Wagombea wengine wote wanaojipambanua na rushwa, wamechukua hatua gani (wakiwa kama Wabunge) kupendekeza mabadilisho ya sheria hiyo na nyinginezo kuziba mianya ya rushwa?

Tatizo lingine lililopo ni rushwa kubwa (Grand Corruption)- ununuzi wa Rada, Deep Green, EPA, Land grabbing ni mifano michache- ni vema rekodi za wanaojipambanua na rushwa zikapimwa kwa hatua/misimamo walioyochukua kushughulikia na madhira haya.

Nimalizie kwa kueleza maoni yangu na swali kwa Mhe Lowassa. Sina shaka yoyote na uwezo wa Mhe Lowassa kuongoza nchi; Sina shaka yoyote juu ya dhamira ya Mhe Lowassa kuona nchi hii inasonga mbele kwa kasi zaidi.

Swali langu ni je atawezaje kuwakwepa baadhi ya watu wanaomzunguka ambao hawana uwezo na dhamira njema kama yake- baadhi yao rekodi zao za utendaji na uadilifu ni za kutiliwa shaka?

Kwenye kundi lake kuna walioshiriki kikamilifu kwenye GRAND CORRUPTION, kuna watu wenye rekodi za kukwepa kodi na kuinyima serikali mapato zinafahamika wazi. Je watu hawa wana share njozi yake ya matumaini kwa watanzania wote au wataendelea na njozi yao ya matumaini kwao peke yao?

Anawatosaje watu hawa? Haya maswali watanzania wengi wangependa kujua!

Swali dogo jibu refuuuuuuuuuuuuuuuuuu kama unataka kulia! Unalia nini sasa!
 
Kama mtakumbuka,mwaka 2012 chama cha mapinduzi kilifanya uchaguzi wake mkuu.Katika uchaguzi huo,kuna tukio lilitokea ambapo Husein bashe alimtuhumu benard membe kuwa alikuwa akiratibu mkakati wa kutengua mfumo wa kofia mbili kwa ngazi ya mwenyekiti wa taifa wa ccm...RAIS awe mwingine na mwenyekiti wa chama awe mwingine.Sakata hili liliishia katika kamati ya maadili.Lakini bashe alijiapiza kuwa membe hatashinda katika nafasi ya ujumbe wa NEC,Membe alishinda!.Lakini,Siku ya tarehe 02/06/2015,mwitongo butiama,,Makongoro nyerere alipokuwa anatangaza nia,Aliweka wazi mchana kweupee kuhusiana na akina nani walikuwa wanaratibu mkakati huo.Makongoro alisema "HAWA VIBAKA WALINIFUATA ILI NIWASAIDIE KATIKA MPANGO WAO WA KUTENGANISHA KOFIA MBILI.NAMI NILIWAULIZA,KWA NINI MNATAKA KUTENGANISHA KOFIA HIZI?,NAO WAKAJIBU..HUYU KIKWETE ANATUBANIA SANA MAMBO YETU...AKAWAULIZA...MAMBO YENU YANA MASLAHI YA TAIFA?..WAKAINAMISHA VICHWA VYAO CHINI".Mwisho makongoro akasema..."waliokuwa wanaratibu mkakati huu ni mapacha watatu.....yaani lowasa,chenge na rostam..the king maker!.Ukiangaliangalia genge hili kwa haraka,Utafikiri kuwa ni watu wenye uchungu na nchi hii kweli kweli.Ukifanya tafakuri kwa kina utagundua kuwa genge hili ni "VIBAKA WANAOVAA SUTI..Lakini tabia zao haina tofauti na vibaka wanaokwapua simu.Mwaka 2005 lowasa ndiye alikuwa mwenyekiti wa wanamtandao...hilo amelisema siku anatangaza nia.Ni yeye ndiye aliratibu mkakati mchafu wa kumchafua dr salm na kumwita ni mwarabu,mara alishiriki kumuua karume,mara ni hizbul,mara ndugu zake wako oman nk.Mwalimu nyerere aliwahi kusema "dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana.ukisha tenda dhambi ya ubaguzi huwezi kuiacha,na dhambi hii ni sawa na kula nyama ya mtu,huwezi kuiacha kamwe...utaendelea nayo tu".Dhambi ya ubaguzi aliyiasisi lowasa na kuisimamia utekelezaji wake ndiyo itakayomtafuna mpaka anakwenda kaburini.Hebu fikiria,DR SALM Aliitwa mwarabu,mbona wapambe wanaomzunguka kuna msomali bashe,Rostam ni mhindi,mbona lowasa hawabagui?...Kwa namna hiyohiyo ambapo lowasa aliratibu dhambi ya kumbagua dr salim ndivyo watanzania tutakavyo mbagua yeye,,,,Lowasa huyu huyu ndiye alimgeka samwel sitta kuhusu sitta kuwa waziri mkuu.Leo hii anatarajia nini kutoka kwa watanzania?...huruma?..kura?..urais?...HAPATI HATA KIMOJA...Fedha zake za kifisadi zitaliwa na hakuna atakachopata.Ndani ya ccm akiteuliwa,Ukawa wataenda ikulu bila kampeni....nja nyeupe kwa ukawa mpaka madodoni.Nani asiyejua sakata la lowasa na batilda burian?,Nani asiyejua sakata la lowasa na betty mkwasa?..Nani asiyejua jinsi lowasa alivyomfanya antony dialo?.Nani asiyejua biashara ya lowasa na hamis mgeja?,Nani asiyejua jinsi fedha za kagoda walivyogawana na rostam?..Nani asiyejua uhusiano uliyopo kati ya lowasa,chenge na karamagi?.....Wapambe wa lowasa mjiandae kupakuliwa full ushahidi kama mtabisha,,,,,LOWASA HAFAI HATA KIDOGO KUWA MKUU WA FAMILIA,URAIS ATAUWEZA?..POLENI SANA ILA NDO UKWELI....
 
Naunga mkono hoja. Hii team= Lowasa, Karamagi, Chenge na Rostam= wako pamoja hata leo na nimtandano hatari mnokwa taifa letu. Washugulikiwe haraka iwezekanavyo.
 
Nanze mada yangu kwa kuuliza maswali la kipuuzi hivi.
1. Ni kweli lowasa amenuia kuingia ikulu?......
2.Ni kweli watanzania wanapenda lowasa awe rais wao?....
3.Je,lowasa atambua kuwa watanzania wana mtaka awe rais?...
4Je,wapambe wa lowasa,wafadhili wake pamoja marafiki wake wanatambu hilo?.
5.Je,lowasa amejiandaa vizuri kukabidhiwa nchi?....
6.Je,lowasa anatambua kuwa yeye ndiye mtia nia mwenye sifa kuzidi watia nia wengine?....
7.Je,lowasa anatambua kuwa endapo watanzania wataamua kumchagua mgombea mwingine,lowasa atafanya nini?...

Maswali yote hayo,jibu ni moja tu.Jibu hilo ni kuwa,' HANA SIFA.
Edwaed ngoyai lowasa hajanuia kuingia ikulu baada ya uchaguzi huu,kwa sababu,Kwa sababu kama angelikuwa na nia thabiti ya kuingia ikulu basi,lowsa angeanza kujisafisha machoni pa watanzania hasa kuhusiana na tuhuma mbalimbali zinazo mwandama...rushwa,ufisadi na mashaka ya mali alizonazo.Kuhusu watanzania kumtaka awe rais wao,lowasa na wapambe wake bado hajatambua kuwa,watanzania hamtaki rais ambaye anakabiliwa na tuhuma za ufisadi,rushwa na staha hafifu ,kitu ambacho lowasa na wafuasi wake halitambui hata kidogo.

kuhusu utayari wa kukabidhiwa nchi,lowasa hajajiandaa kukabithiwa ikulu,Kwani angelikuwa tayari,lowasa asingepingana na sera/ilani ya ccm kuhusiana na elimu kwanza badala ya kilimo kwanza.Hii inaonyesha kuwa,lowasa haiheshimu ccm na dira ya maendeleo ya ccm,Na kwamba,endapo ccm itamsimamisha lowasa na kushinda katika uchaguzi hou,Basa,lowasa ataacha kufuata na kutekeleza ilani na maagizo ya ccm,badala yake ataendesha nchi kwa ilani yake anayoijua yeye.
Ni kweli kabisa kuwa lowasa ndiye mtia nia ambaye ana sifa kuliko watia nia wengine....richmond ni sifa yake...alphatel. ni sifa yake...kuratibu kumchafua dr salim 2005 ni sifa yake....Uhusiano!/ na batilda burian ni sifa yake...bety mkwasa...sifa yake...kagoda ni shombo yake....makundi ya urais yanayo tukana pale wanapoombwa majibu kuhusiana na mgombe wao ni sifa yake...kutoa hongo ili adhaminiwe na chama ni sifa yake..kujisahau na kuongelea habari fulani kwa majibu tofauti ni sifa yake.Watanzania wenzangu,Naomba tuinuke na kwa sauti moja kuanzia sasa popote ulipo..TUMKATAE LOWASA KUWA RAIS WETU,................
 
Kweli ukuwadi ni jambo baya sana! Yaani umelishwa sumu mpaka umejisahau!

Watanzania sio makuwadi wala wajinga kama wewe! wala hatuna akili za kushikiwa kama wewe!

Kabla ya kuanza kubwabwaja na kutema pumba na hoja zako dhaifu! kwanza ungejiuliza maswali yafuatayo;

(1).Kuhusu rushwa na ufisadi ni mahakama gani iliwahi kumkuta EL na hatia?! wewe unao ushaidi wa tuhuma hizo au unaleta ushabiki maandazi?!

(2).Kutokufuata ilani ya ccm; Hivi Membe aliposema atabadili sheria na kumfunga mtoa rushwa tu badala ya mtoaji na mpokeaji alifuata ilani ya chama?! Usiwe kilaza mpaka unajisahau! watanzania wa-leo sio wale wa mwaka 1961..!

Majungu, chuki na wivu ni sumu ya maelendeleo ya nchi, tutoe hoja facts na sio tetesi za mitaani na kwenye kahawa! kuhusu afya EL yuko fit kama anavyoonekana! angekuwa mgonjwa angeweza kuzunguka nchi nzima kutafuta wadhamini?! Na wakusema afya ya mtu ni yeye mwenyewe au daktar wake! wewe daktar wake?!

Acha Kutumiwa kama toilet paper tumia ufaham wako mzuri aliokupa muumba!
 
Nanze mada yangu kwa kuuliza maswali la kipuuzi hivi.
1. Ni kweli lowasa amenuia kuingia ikulu?......
2.Ni kweli watanzania wanapenda lowasa awe rais wao?....
3.Je,lowasa atambua kuwa watanzania wana mtaka awe rais?...
4Je,wapambe wa lowasa,wafadhili wake pamoja marafiki wake wanatambu hilo?.
5.Je,lowasa amejiandaa vizuri kukabidhiwa nchi?....
6.Je,lowasa anatambua kuwa yeye ndiye mtia nia mwenye sifa kuzidi watia nia wengine?....
7.Je,lowasa anatambua kuwa endapo watanzania wataamua kumchagua mgombea mwingine,lowasa atafanya nini?...

Maswali yote hayo,jibu ni moja tu.Jibu hilo ni kuwa,' HANA SIFA.
Edwaed ngoyai lowasa hajanuia kuingia ikulu baada ya uchaguzi huu,kwa sababu,Kwa sababu kama angelikuwa na nia thabiti ya kuingia ikulu basi,lowsa angeanza kujisafisha machoni pa watanzania hasa kuhusiana na tuhuma mbalimbali zinazo mwandama...rushwa,ufisadi na mashaka ya mali alizonazo.Kuhusu watanzania kumtaka awe rais wao,lowasa na wapambe wake bado hajatambua kuwa,watanzania hamtaki rais ambaye anakabiliwa na tuhuma za ufisadi,rushwa na staha hafifu ,kitu ambacho lowasa na wafuasi wake halitambui hata kidogo.

kuhusu utayari wa kukabidhiwa nchi,lowasa hajajiandaa kukabithiwa ikulu,Kwani angelikuwa tayari,lowasa asingepingana na sera/ilani ya ccm kuhusiana na elimu kwanza badala ya kilimo kwanza.Hii inaonyesha kuwa,lowasa haiheshimu ccm na dira ya maendeleo ya ccm,Na kwamba,endapo ccm itamsimamisha lowasa na kushinda katika uchaguzi hou,Basa,lowasa ataacha kufuata na kutekeleza ilani na maagizo ya ccm,badala yake ataendesha nchi kwa ilani yake anayoijua yeye.
Ni kweli kabisa kuwa lowasa ndiye mtia nia ambaye ana sifa kuliko watia nia wengine....richmond ni sifa yake...alphatel. ni sifa yake...kuratibu kumchafua dr salim 2005 ni sifa yake....Uhusiano!/ na batilda burian ni sifa yake...bety mkwasa...sifa yake...kagoda ni shombo yake....makundi ya urais yanayo tukana pale wanapoombwa majibu kuhusiana na mgombe wao ni sifa yake...kutoa hongo ili adhaminiwe na chama ni sifa yake..kujisahau na kuongelea habari fulani kwa majibu tofauti ni sifa yake.Watanzania wenzangu,Naomba tuinuke na kwa sauti moja kuanzia sasa popote ulipo..TUMKATAE LOWASA KUWA RAIS WETU,................

Nyamalingo nafikiri umeyaandika haya baada ya mke wako kukuambia ulale sebuleni kwa sababu mwanaume umekosa sifa ya kulala chumba kimoja na Mimi.
 
Kweli ukuwadi ni jambo baya sana! Yaani umelishwa sumu mpaka umejisahau!

Watanzania sio makuwadi wala wajinga kama wewe! wala hatuna akili za kushikiwa kama wewe!

Kabla ya kuanza kubwabwaja na kutema pumba na hoja zako dhaifu! kwanza ungejiuliza maswali yafuatayo;

(1).Kuhusu rushwa na ufisadi ni mahakama gani iliwahi kumkuta EL na hatia?! wewe unao ushaidi wa tuhuma hizo au unaleta ushabiki maandazi?!

(2).Kutokufuata ilani ya ccm; Hivi Membe aliposema atabadili sheria na kumfunga mtoa rushwa tu badala ya mtoaji na mpokeaji alifuata ilani ya chama?! Usiwe kilaza mpaka unajisahau! watanzania wa-leo sio wale wa mwaka 1961..!

Majungu, chuki na wivu ni sumu ya maelendeleo ya nchi, tutoe hoja facts na sio tetesi za mitaani na kwenye kahawa! kuhusu afya EL yuko fit kama anavyoonekana! angekuwa mgonjwa angeweza kuzunguka nchi nzima kutafuta wadhamini?! Na wakusema afya ya mtu ni yeye mwenyewe au daktar wake! wewe daktar wake?!

Acha Kutumiwa kama toilet paper tumia ufaham wako mzuri aliokupa muumba!

Kamati Teule ya Bunge ilimkuta na hatia mwaka 2008, hali iliyomlazimu ndugu Edward Lowassa ajiuzulu Uwaziri Mkuu mwaka huo huo. Kama isingekuwa kashfa na UFISADI wa Richmond, leo hii tunavyoongea Lowassa angekuwa waziri mkuu. Kwa hiyo, hii haihitaji mahakama. Tuhuma tu zinatosha kumuengua mtu kwenye kinyang'anyiro cha kugombea ukuu wa Rais. Cha msingi nyinyi jibuni hoja kwa hoja na sio kuleta porojo hapa. Jamaa kauliza maswali mhimu, myajibu na sio kumshambulia. Watu waungwana huwa wanajibu maswali kwa hoja na majibu sahihi sio kuropoka

Kuna kipindi cha 2007 alitajwa pia kuwa mmoja wa MAFISADI kwenye list of shame pale Mwembeyanga mwaka 2007 na Dr.Slaa wakati ule. Mpk ninavyoongea leo hii Lowassa hakuwahi kupeleka kesi mahakamani ili kupinga na kuwashitaki waliomtaja kuwa ni FISADI. Kwa hiyo, ninyi mnaotoa hoja ya mahakama kama kigezo mhimu cha kumsafisha mtu, toeni na hoja hiyo. Bunge ni mhimili unaojitegemea, ulimkuta Lowassa na hatia akajiuzulu nafasi yake, na wala mamlaka ya Bunge hayawezi kuhojiwa na chombo chochote cha dola, si mhimili wa utendaji/utawala wala mahakama. Tafakari
 
Kweli lowasa ndie rais dalil kama hz zinanionyesha kabisa jamaa anafaa kuwa rais twende na mwendo wa matumain
 
Kama kigezo ni kujiuzuru uwaziri kwa tuhuma tu! hata Mwinyi aliwahi kujiuzuru uwaziri na baadae akaja kuwa Raisi!

Na kama hoja ni kashfa' hata membe hafai kuwa raisi maana ana kashfa ya fedha za ghaddaf..!

watanzania hatutaki kuchaguliwa raisi kama watoto wadogo! hatutaki raisi wa kuchora kwenye karatasi..!
Tunataka raisi mtendaji na mwenye maamuzi magumu na sahihi..! Tulipofika pametosha!
 
Kama kigezo ni kujiuzuru uwaziri kwa tuhuma tu! hata Mwinyi aliwahi kujiuzuru uwaziri na baadae akaja kuwa Raisi!

Na kama hoja ni kashfa' hata membe hafai kuwa raisi maana ana kashfa ya fedha za ghaddaf..!

Kwa kawaida hutakiwi kuhalalisha kosa kwa kutumia kosa jingine. Membe kama ni mchafu au FISADI huwezi kumtumia kuhalalisha UFISADI wa Lowassa. Kimsingi kwa kigezo hicho ina maana wote ni MAFISADI na hawafai kuwa Marais wetu. Pia, hoja ya kujiuzulu kwa Ally Hassan Mwinyi akiwa Waziri ya mambo ya ndani, hakuna uhusiano wowote na kujiuzulu kwa Lowassa. Mazingira ya kujiuzulu watu hawa wawili yanatofautiana sana, na muktadha wa kujuzulu kwao ni tofauti. Lakini hoja mhimu, wakati Mwinyi akijiuzulu kutokana na maswala ya kufa kwa wafungwa gerezani, Edward Lowassa alijiuzulu kutokana na kashfa kubwa sana ya UFISADI wa Richmond iliyotuingiza hasara kubwa Watanzania.

Aidha, Lowassa alijiuzulu kutokana na shinikizo baada ya kukutwa na hatia na kamati teule ya Bunge. Japo yeye alisingizia tatizo ni Uwaziri Mkuu. Kujiuzulu kwa Ally Hassan Mwinyi kunafanana sana jinsi walivyojiuzulu wale Mawaziri 4 katika Operation Tokomeza, akiwemo waziri wa mambo ya ndani Dr.Emmanuel Nchimbi. Ukiwafananisha hawo na Mwinyi tutakuelewa, lakini sio kujiuzulu kwa Edward Lowassa.
 
Inasemekana LOWASSA anamuogopa sana MAKONGOLO NYERERE, coz nyerere anam-face direct kwa kutumia udhaifu wa neno fisadi ambao Lowassa hawezi kumjibu kwa njia yoyote akaonekana msafi, bila kulitamka neno hilo ambalo ni mwiko kwake kulitamka.
 
Back
Top Bottom