Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Kwanini Lowassa anakwepa kuzungumzia ufisadi?

Ameamua kujipanga kukemea hadharani wale wote wanaojihusisha na rushwa na ufisad. Amedai kuwa wanalitia aibu taifa letu.
Hiyo nimeipata kutoka kwa wapambe wa Lowassa a.k.a team Lowassa kuwa mzee wao kaamua kuja na style hiyo ya kukemea rushwa na ufisadi pengine labda inaweza kumtoa kimasomaso kwenye kinyang'anyiro cha urais 2015 October.

Mbona hatujamwona bungeni akijenga hoja hiyo wakati wa escrow! Amekumbuka shuka kumekucha.
 
Haa ha ha...nadhani kwenye hiyo press conference yake ataongozana na rafiki zake Chenge na Rostam Aziz wakikemea juu ya ufisadi na ukiukaji wa maadili ya viongozi ulioenea nchini.

Bila kumsahau bibi bomba wa kihaya mamaa wa mboga ya milioni 10 prof. Tibaijk
 
Ha ha ha ha ha ha, Lawasa yupi wa kukemea rushwa? Hana sababu ya kufanya hivyo
 
Ameamua kujipanga kukemea hadharani wale wote wanaojihusisha na rushwa na ufisad. Amedai kuwa wanalitia aibu taifa letu.
Hiyo nimeipata kutoka kwa wapambe wa Lowassa a.k.a team Lowassa kuwa mzee wao kaamua kuja na style hiyo ya kukemea rushwa na ufisadi pengine labda inaweza kumtoa kimasomaso kwenye kinyang'anyiro cha urais 2015 October.

Nitapenda kuiona video ya maneno hayo kama ni kweli.
 
Ni Lowasa yupi?.Huyuhuyu mwenye Mvii?.kama niyeye ntamuona nisawa na mchawi anayekuja kulia msibani akijua niyeye aliyesababisha.Tuwekeeni video tumsikilize labda mumemnukuu vibaya
 
Aliyeleta uzi huu hafikilii masilahi mapana kwa nchi hii.Mimi siisomi naenda naenda nyumbani kwetu RICHMOND,aah samahani MONDULI
 
Mla rushwa hawezi kuwakemea wala rushwa wenzake kwanza Lowasa hana uwezo wa kukemea rushwa kwa sababu ndo Sera ya ccm
 
Wanasema VITA HAINA MACHO,inawezekana hata KATIBU WANGU WA CHAMA siku moja akaacha kusomba maji kwenye bustani za mbogamboga na kunyanyua tofari za maabara akaenda kusaidiana na Askari wa Wanyama poli kuokoa tembo wetu wanaoteketezwa polini na majangili.YA MUNGU MENGI BINADAMU HUWA HATUJUI
 
Aliyeleta uzi huu hafikilii masilahi mapana kwa nchi hii.Mimi siisomi naenda naenda nyumbani kwetu RICHMOND,aah samahani MONDULI
 
Back
Top Bottom