Kwanini kunguru akifa hatoki funza?

Kwanini kunguru akifa hatoki funza?

Ukishika wire halafu umekanyaga chini basi utakula shoti ila kama umeshika wire juu kwa juu hutapigwa shoti kwa kuwa hujacomplete circuit haya ni kwa mujibu wa mwl wangu wa physics a level (nisahihishe)
Amekudanganya huyo.. Nenda kashike waya wa gridi ya taifa bila kugusa chini uone kama hujageuka majivu
 
Mkuu chaUkucha

Sio kweli Kunguru hapigwi shoti ya umeme coz ya sumu iliyopo ndani ya damu yake,

Unajua hakuna shoti kama hakuna "potential difference" katika terminals za kifaa chochote kile,

Kunguru anapokanyaga waya mmoja kunakua hakuna "Partial discharde ( p.d ) lakini kama akitanua miguu yake na kukanyaga waya mbili atapigwa na shoti na kugeuka majivu in a seconds!

Chukulia mfano wa binaadamu,yeye anatengeneza partial discharge (p.d) kati ya waya na "earth"
Yani binaadamu anapokuwa kasimama ardhini, lakini kama akining'inia kwenye waya kwa mkono mmoja au hata kwa mikono yake yote miwili ikiwa karibukaribu hakuna madhara mradi hagusi chochote kinachogusana na ardhi. Lakini kama akitanua mikono yake itakua anatengeneza partial discharge na lazima apigwe na shoti,

Kitu kingine,Kunguru miguu yake ina magamba ambayo ni "Insulation" hii humsaidia asipigwe na shoti hata akigusa miguu yote hatapata shoti,ila hiyo insulation yake ni kwa umeme mdogo tu kama vile 1V to 450V kwa umeme mkubwa hiyo insulation yake miguuni haitomsaidia kitu.
Na sababu nyingine, nyaya za umeme zina maganda juu, kwa hiyo akitua sehemu yenye ganda hawezi kunaswa na shoti ya umeme
 
Kuna MTU uku kwetu mitaa ya yombo kilakala alikula kungulu aliumwa mpaka akafaliki
 
Kwasababu Kunguru mwenyewe ni funza mwenye mabawa,funza anakula mizoga na kunguru hivyo hivyo
Hahahaa! Mkuu hii elimu ulifundishwa na nani? Na ilikua wapi?

Kunguru atakuaje yeye ni Funza?!Funza ni hatua mojawapo ya ukuaji wa viumbe hasa wadudu ambao wanapitia hatua za Metamorphosis,

kwa mfano kuna jamii fulani ya Nzi weupe,hawa Nzi wana umbo kubwa kiasi,hawa Nzi hua wanataga mayai,na baada ya dakika kadhaa hugeuka kua Funza,Jaribu kusoma Theories of evolution has a spantaneous generation utaelewa zaidi.
 
Ndege wote miguu yao imefunikwa na magamba yasiyopitisha umeme ndio maana hawawezi kudhurika na umeme
 
alitumwa na nuhu akacheki kama maji yameisha hakurudi tena kwa nuhu akanogewa na mapochopocho aloyakuta yanaeleaelea
Si kweli kwamba alinogewa na mapochopocho ndiyo maana hakurudi,ila sababu ni kuwa alipata pa kutua na hilo ndiyo lillomjulisha nuhu kuwa maji yamekauka!!!
 
Mkuu Kunguru haozi bali hukauka tu,suala la kwanini haozi nimelitolea maelezo huko juu,ni kweli atakauka ila "atapotea" kwa nature,hata chuma ukikiweka ardhini for so long,mwisho wake kitabadilika na kua udongo tu na kupotea,hiyo haina maana eti chuma kimeshambuliwa na bacteria!
mkuu kwani kinacho decompose chuma nnn kama si baadhi ya viumbe visivyoonekana? the same applied to Kunguru nao wanaoza kwa sababu kwenye eco-sestem kuna decomposers hukoo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom