Unajua nini maana ya ASILI mkuu?!Kama wewe si mfuasi wa hiyo unaita dini ya asili, huoni hadi wewe umeipuuza na kuitenga?
kuwaomba mizimu ? unamuomba mfu nn?Sijasema 'kuabudu' chief,nlisema 'kuomba'.
somo gan ilo tena?wape somo hawa
This is pointKweli mkuu,,, nakumbuka hata kupiga nyungu (kujifukiza wakati wa covid - 19) watu walidai kuwa ni ushirikina?! Wakati ulaya na marekani kuna rooms za mvuke !
Na cha kushangaza zaidi, hizi dini zetu kubwa ukristo na uislam wanasisitiza sana kwenda kuhiji au kuzuru kwenye makaburi ya mitume na masharifu kule Israel na saudia wakidai utapata thawabu kiasi kwamba watu maskini wanadunduliza fedha hadi mamilioni ili tu kwenda kudhuru makaburi hayo,
wakati huohuo wanatukataza hata kwenda kuyafanyia usafi na kuyajengea makaburi ya babu zetu na ndugu zetu ili kudumisha kumbukumbu zao zisipotee, kwa madai kwamba hiyo ni haramu na ni ibada ya mizimu! Hata kama lengo lako ni kwenda tu kuyafanyia usafi na si vinginevyo!
Sasa najiuliza hivi inakuwaje kwenda kutembelea makaburi ya babu zetu na ndugu zetu kule kijijini na kuyafanyia usafi ni haramu na ushetani na ni ibada ya mizimu lakini kukusanya mamilioni ya fedha kwenda kutembelea au kuzuru makaburi ya hao wa Israel au saudia ni thawabu (wanaita kuhijji na sio ibada ya mizimu) na sio ushetani kama kwenda kutembelea nakusafisha haya makaburi ya ndugu zetu?!
Sawa kabisa mkuu, swali zuri kabisa, ungeuliza hivyo mwanzo ningekujibu directly! Ila hitimisho lako kwamba " huoni na wewe kuiita dini ya asili umeipuuza dini hiyo?! Ndio nikakujibu kuiita asili sio kuipuuza Bali ni kuiheshimu maana asili sio tusi Bali ni sifa!Mkuu Loyalist, heshima mbele!
Hata mimi sijachanganya asili na kienyeji, hakuna sehemu nimeandika namna hiyo.
Swali langu liko pale pale, kwa tafsiri yako kuwa asili ni heshima.... pengine ulitaka kumaanisha nini uliposema "wewe pia si mfuasi wa dini za asili"?
Unachanganya imani,dini na mila/tamaduni.Mkuu, dini za asili au za jadi hazinaga majina kama brand za kibiashara, maana hizi za kikoloni za kuletwa na meli na majahazi zina majina mengi,
Kila kabila au jamii inaijua dini yake au imani yake, iliyokuwa inaifuata kabla ya kufika kwa wageni wa mwanzo, waarabu, wazungu na wahindi hata Wachina (Buddha, Tao nk).
Ukisema utaje majina sidhani kama tutaelewana au hata thread itatosha hii, majina ya dini za asili yako mengi kulingana na lugha ya kabila husika, mfano wazaramo, wachagga, wasambaa, wazigua, wangazija, wasukuma, wahaya,wamakonde, wamwela, wangoni, wayao, wagogo, wanyamwezi,waha,wangindo, wanyakyusa, n.k. kila kabila lilikuwa na imani yake au dini yake waliyokuwa wanaitumia kufanya ibada na Maombi kwenye matukio mbalimbali mfano:
majanga ya asili kama ukame (wanapoomba mvua), kubariki watoto wanapozaliwa, jando na unyago, ndoa, mavuno, ugonjwa hata vita!
ni dini mbili zinazo kizi vigezo hivyo dini ya kikiristo na Kiislamu. Kwani hujui mkuu.
Dini ya uislam na ukristu ndio uchawi ndio maana kutwa kupambana na mapepo na mjiniSwali lako nimekujibu tayari lakini, hizo dini za asili ni za kichawi chawi tu.
Wahindi sio ndugu zetu hebu toa ushamba wa wazungu waarabu na wazungu kichwani mwskoNimeshawahi kuleta mada inafanana hivi kuwa hapa nchini kuna watanzania wenzetu ambao wana asili ya Asia.Wana dini yao inaitwa Hindu pia wapo Sikh na pia Buddha.Kwanini wako nyuma ya pazia kwenye kuliombea taifa au hafla za kitaifa nao hawajitokezi ilhali ni watanzania wenzetu?
JIBU NI RAHISI MTOA MADA NAOMBA NILIANDIKE INFERIORITY COMPLEX KWA DINI ZA ASILI NA DINI AMBAZO SIO ZA IBRAHIM(ukristo na uislam)
Ni nyerere tu alivyofariki mkuu wa dini ya Hindi Nyerere alipokuwa anaombewa naye alijitokeza akamuombea.
Naomba nimnukuu askofu Desmond Tutu ''Wakoloni walivyokuja tulikuwa na dini zetu wakatuletea biblia.Wakatuambia tufunge macho tuombe.Tulipofunga macho na kuomba baada ya kufungua tu tukakuta wamechukua ardhi yetu na sisi tumebaki na biblia''-------mwisho wa kunukuu
Nani ulimuona yupo uchiAcheni masuala ya kuturudisha kwenye matambiko usiku wa manane watu wakiwa uchi na sadaka za damu ifikie wakati waafrica tusiwe tena bara la giza
Zilimtesa NaniKiongozi eti kuzidharau dini zetu za kiasili ni kasumba''HAPANA SIWEZI NARUDIA TENA HAPANA''sitaki uniaminishe katika miungu Hivi unajua hizi madhabahu za ukoo jinsi zinavetesa watu wewe watu wanawekewa vikwazo wanashindwa kuishi katika ndoto zao kwa ajili ya maagano ya giza walioingia mababu zao miaka na miaka roho za magonjwa,ufukara,utasa/ugumba kwanini tuishi nje ya misingi ya baraka MUNGU alizotuwekea...Kilichotokea pale msalabani ni pigo kubwa kwa shetani(NA YOTE IMEKWISHA)Yani tumekombolewa rejea "Eeeh BABA WASAMEHE KWAKUWA HAWAJUI WALITENDALO" lakini sio kwamba shetani kafungwa minyororo la hasha hapana ndio maana ana hasira zaidi so usishangae mabaya yanayotekea.Nimechoka kidogo tupo pamoja
Unaweza kunambia Albadili maana yake ni nini ?wasoma albadili nyie
Unachanganya imani,dini na mila/tamaduni.
Hayo mambo unayosema kwenye hayo makabila yetu sio dini ni tamaduni au mila zenye kuambatana na imani mbalimbali.
hizo dini zingine ondoa mkuu, abudu dini zinazo mwabudu yule aliye umba dunia na vitu vyote huyo ndio wa kumwabudu
Wewe unabeba kama yalivyo ndipo unapokosea...Kiongozi eti kuzidharau dini zetu za kiasili ni kasumba''HAPANA SIWEZI NARUDIA TENA HAPANA''sitaki uniaminishe katika miungu Hivi unajua hizi madhabahu za ukoo jinsi zinavetesa watu wewe watu wanawekewa vikwazo wanashindwa kuishi katika ndoto zao kwa ajili ya maagano ya giza walioingia mababu zao miaka na miaka roho za magonjwa,ufukara,utasa/ugumba kwanini tuishi nje ya misingi ya baraka MUNGU alizotuwekea...Kilichotokea pale msalabani ni pigo kubwa kwa shetani(NA YOTE IMEKWISHA)Yani tumekombolewa rejea "Eeeh BABA WASAMEHE KWAKUWA HAWAJUI WALITENDALO" lakini sio kwamba shetani kafungwa minyororo la hasha hapana ndio maana ana hasira zaidi so usishangae mabaya yanayotekea.Nimechoka kidogo tupo pamoja
najua basi 😅😅. in content sijui ila ni kama kumtumia mtu laana flainUnaweza kunambia Albadili maana yake ni nini ?
Uzi mzuri huuHabari zenu wakuu?
Kuna jambo limekuwa linanitatiza kwa muda mrefu sana, hasa inapokuja kwenye suala la mikutano au hafla za kiserikali, taasisi au hata siasa!
Nchi yetu inafahamika kwa kufuata Sera ya secularism, yaani nchi isiyofuata dini rasmi, nchi ambayo kila mwananchi ana imani yake binafsi, hakuna dini Moja rasmini ya kitaifa!
Lakini jambo linaloniumiza kichwa sana ni kwamba kwanini kwenye hafla, mikutano au mikusanyiko ya kitaifa, kisiasa au mingineyo viongozi wa dini zetu za asili hawapewi nafasi ya kufanya Maombi kama dini nyingine hususani uislam, ukristo au hata uhindu?
Nashindwa kuelewa sababu hasa ya kuibagua imani hii, japo ni dini zetu za asili kabla hata ya kuja imani hizi tulizoletewa na wakoloni (waarabu na wazungu) lakini cha kushangaza ni vigumu sana kukuta viongozi wa dini zetu za asili wakipewa nafasi ya kufanya Maombi kama wenzao wa dini ya Kikristo na Kiislam?
Tatizo ni nini?! Bado tunakasumba za kuthamini sana vitu vya kikoloni kuliko vyetu kama Tulivyo aminishwa na wakoloni kwamba ni dini za kishenzi au ni dini hizo kukosa wawakilishi wao rasmi ni?
Maana hata kwenye mikutano ya kisiasa inayoendelea hivi sasa hapa nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani 28 October 2020 sijawahi kuona chama chochote kikianza kwa kuwapa nafasi viongozi wa dini za asili, zaidi ya viongozi wa dini za kiislam, kikristo na kihindu kidogo!
NB: Mimi sio mfuasi wala muumini wa dini za asili.
Lakini kama tunajinasibihisha kuwa nchi yetu haina dini je, hatuoni kwamba tunafanya ubaguzi kwa kuwatenga na kutowapa nafasi viongozi wa dini za asili?
Tena tunaonekana kama bado tunakasumba za kupuuza vitu vyetu wenyewe na kuthamini zaidi vitu vilivyoletwa na wageni?