Kwanini Dini za asili hazipewi nafasi?

Loyalist

JF-Expert Member
Aug 28, 2020
411
884
Habari zenu wakuu?

Kuna jambo limekuwa linanitatiza kwa muda mrefu sana, hasa inapokuja kwenye suala la mikutano au hafla za kiserikali, taasisi au hata siasa!

Nchi yetu inafahamika kwa kufuata Sera ya secularism, yaani nchi isiyofuata dini rasmi, nchi ambayo kila mwananchi ana imani yake binafsi, hakuna dini Moja rasmini ya kitaifa!

Lakini jambo linaloniumiza kichwa sana ni kwamba kwanini kwenye hafla, mikutano au mikusanyiko ya kitaifa, kisiasa au mingineyo viongozi wa dini zetu za asili hawapewi nafasi ya kufanya Maombi kama dini nyingine hususani uislam, ukristo au hata uhindu?

Nashindwa kuelewa sababu hasa ya kuibagua imani hii, japo ni dini zetu za asili kabla hata ya kuja imani hizi tulizoletewa na wakoloni (waarabu na wazungu) lakini cha kushangaza ni vigumu sana kukuta viongozi wa dini zetu za asili wakipewa nafasi ya kufanya Maombi kama wenzao wa dini ya Kikristo na Kiislam?

Tatizo ni nini?! Bado tunakasumba za kuthamini sana vitu vya kikoloni kuliko vyetu kama Tulivyo aminishwa na wakoloni kwamba ni dini za kishenzi au ni dini hizo kukosa wawakilishi wao rasmi ni?

Maana hata kwenye mikutano ya kisiasa inayoendelea hivi sasa hapa nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani 28 October 2020 sijawahi kuona chama chochote kikianza kwa kuwapa nafasi viongozi wa dini za asili, zaidi ya viongozi wa dini za kiislam, kikristo na kihindu kidogo!

NB: Mimi sio mfuasi wala muumini wa dini za asili.

Lakini kama tunajinasibihisha kuwa nchi yetu haina dini je, hatuoni kwamba tunafanya ubaguzi kwa kuwatenga na kutowapa nafasi viongozi wa dini za asili?

Tena tunaonekana kama bado tunakasumba za kupuuza vitu vyetu wenyewe na kuthamini zaidi vitu vilivyoletwa na wageni?
 
Mzungu ukristo
Muarabu uislamu
Mu asia buddha
Kuna jews ajili ya mataifa flan flan

Muafrica ni kama hastahili kuwa na dini yaani africa ni soko huria kutangaza dini zao.Sijui imekuaje kuaje mpk imani zetu zimekuwa ushetani na nguvu za giza. Ina maana sisi wazee wetu hawana jema,mizimu yetu tu ndo mashetani?mbona wahindi wanaabudu hadi ng’ombe!nyoka!watu!

Nadhani kuwa watu flani flani walijua dini zetu zinanguvu sasa wakataka kuzibadili lkn swali ni je tunawabadilishia tunawapa dini gani?????Pili,hawa wapuuzi walijua wakitufanya tuchukie utamaduni wetu na imani zetu halfu tukapenda za kwao ni rahisi sana kututawala.

Dini zinakuja ili tutawalike kirahisi na kimsingi Dini zote zinafundisha basics priniciple ambazo ni imani,msamaha,maombi,ibada,matendo mema yaani kifupi mpagani akifanya hayo ana nguvu sawa na mshika dini...

usizini inayozungumzia kwenye biblia ndo ile ile ya kwenye quaran sema tu lugha tofauti uwasilishaji tofauti.Ukweli huu unahitaji uwe na akili huru sana..

Leo hii hata kunywa dawa ya asili unaonekana mshirikina!!!unaonekana mshamba!
 
Mzungu ukristo
Muarabu uislamu
Mu asia buddha
Kuna jews ajili ya mataifa flan flan

Muafrica ni kama hastahili kuwa na dini yaani africa ni soko huria kutangaza dini zao.Sijui imekuaje kuaje mpk imani zetu zimekuwa ushetani na nguvu za giza. Ina maana sisi wazee wetu hawana jema,mizimu yetu tu ndo mashetani?mbona wahindi wanaabudu hadi ng’ombe!nyoka!watu!

Nadhani kuwa watu flani flani walijua dini zetu zinanguvu sasa wakataka kuzibadili lkn swali ni je tunawabadilishia tunawapa dini gani?????Pili,hawa wapuuzi walijua wakitufanya tuchukie utamaduni wetu na imani zetu halfu tukapenda za kwao ni rahisi sana kututawala.

Dini zinakuja ili tutawalike kirahisi na kimsingi Dini zote zinafundisha basics priniciple ambazo ni imani,msamaha,maombi,ibada,matendo mema yaani kifupi mpagani akifanya hayo ana nguvu sawa na mshika dini...

usizini inayozungumzia kwenye biblia ndo ile ile ya kwenye quaran sema tu lugha tofauti uwasilishaji tofauti.Ukweli huu unahitaji uwe na akili huru sana..

Leo hii hata kunywa dawa ya asili unaonekana mshirikina!!!unaonekana mshamba!
Kweli mkuu,,, nakumbuka hata kupiga nyungu (kujifukiza wakati wa covid - 19) watu walidai kuwa ni ushirikina?! Wakati ulaya na marekani kuna rooms za mvuke !

Na cha kushangaza zaidi, hizi dini zetu kubwa ukristo na uislam wanasisitiza sana kwenda kuhiji au kuzuru kwenye makaburi ya mitume na masharifu kule Israel na saudia wakidai utapata thawabu kiasi kwamba watu maskini wanadunduliza fedha hadi mamilioni ili tu kwenda kudhuru makaburi hayo,

wakati huohuo wanatukataza hata kwenda kuyafanyia usafi na kuyajengea makaburi ya babu zetu na ndugu zetu ili kudumisha kumbukumbu zao zisipotee, kwa madai kwamba hiyo ni haramu na ni ibada ya mizimu! Hata kama lengo lako ni kwenda tu kuyafanyia usafi na si vinginevyo!

Sasa najiuliza hivi inakuwaje kwenda kutembelea makaburi ya babu zetu na ndugu zetu kule kijijini na kuyafanyia usafi ni haramu na ushetani na ni ibada ya mizimu lakini kukusanya mamilioni ya fedha kwenda kutembelea au kuzuru makaburi ya hao wa Israel au saudia ni thawabu (wanaita kuhijji na sio ibada ya mizimu) na sio ushetani kama kwenda kutembelea nakusafisha haya makaburi ya ndugu zetu?!
 
Mzungu ukristo
Muarabu uislamu
Mu asia buddha
Kuna jews ajili ya mataifa flan flan

Muafrica ni kama hastahili kuwa na dini yaani africa ni soko huria kutangaza dini zao.Sijui imekuaje kuaje mpk imani zetu zimekuwa ushetani na nguvu za giza. Ina maana sisi wazee wetu hawana jema,mizimu yetu tu ndo mashetani?mbona wahindi wanaabudu hadi ng’ombe!nyoka!watu!

Nadhani kuwa watu flani flani walijua dini zetu zinanguvu sasa wakataka kuzibadili lkn swali ni je tunawabadilishia tunawapa dini gani?????Pili,hawa wapuuzi walijua wakitufanya tuchukie utamaduni wetu na imani zetu halfu tukapenda za kwao ni rahisi sana kututawala.

Dini zinakuja ili tutawalike kirahisi na kimsingi Dini zote zinafundisha basics priniciple ambazo ni imani,msamaha,maombi,ibada,matendo mema yaani kifupi mpagani akifanya hayo ana nguvu sawa na mshika dini...

usizini inayozungumzia kwenye biblia ndo ile ile ya kwenye quaran sema tu lugha tofauti uwasilishaji tofauti.Ukweli huu unahitaji uwe na akili huru sana..

Leo hii hata kunywa dawa ya asili unaonekana mshirikina!!!unaonekana mshamba!
Hakika umenena mkuu
 
Acha uhuni mkuu, tunataka dini inayomwabudu Mungu aliyejuu aliyeviumba viumbe vyote vilivyomo na visivyo onekana. Mungu aliyeumba mito, jua, nyota, mbingu, dunia.
Hizo dini zingine zinawaabudu watu, zinawaabudu mizimu ya mababu ambao wote hao waliumbwa na Mungu aliyeziumba mbingu na nchi
Mkuu sio uhuni, ni kwamba Tanzania ni secular country! Hatuna dini rasmini ya taifa mkuu,

Kila imani /dini ina haki ya kutambulika, kuheshimika na kupewa nafasi mkuu!

Dini mbili kuu ukristo na uislam (ambazo zililetwa na wakoloni) zimekuwa zikipewa nafasi sana hapa nchini (na sipingi hilo hata kidogo) uhindi na mabohora pia, lakini hatuoni dini zetu za asili zikipewa nafasi pia?!

Haki iko wapi katika nchi ambayo inafuata mfumo wa secularism?!
 
swali lako nimekujibu tayari lakini, hizo dini za asili ni za kichawi chawi tu.
Mkuu Sijui kama umenielewa vizuri ndugu yangu?!

Wacha nirudie tena ni hivi:

Tanzania haina dini rasmini kila dini ina haki sawa mbele ya katiba na taifa, ukristo au uislam sio bora kuliko dini za asili kwa mujibu wa katiba!

Kwahiyo kwa Tanzania hakuna dini bora kuliko nyingine mkuu, wala usidhani kuwa dini yako (au dini Fulani) ni bora au sahihi kuliko nyingine KWA MUJIBU WA KATIBA YETU hivyo sio haki kuiita au kuikosoa dini /imani nyingine kuwa ni ya kishetani au vinginevyo (kwa mujibu wa katiba zote ni sawa)

Hata uhindu pia uhabudu nyoka, ng'ombe n.k. lakini kuna mikutano viongozi wa kihindu wanapewa nafasi, na hata hao wanao amini dini za asili wanaweza kuona imani yako wewe ni ushetani pia kama wewe unavyoziona imani zao kwa mujibu wa imani yako! Au wakasema imani yako ni kasumba tu zilizopandikizwa na wakoloni ili watutawale kirahisi.

Ndio maana katiba yetu inatambua na kuheshimu dini /imani zote hata kama unaabudu jiwe ni shauri yako!

Kwahiyo hakuna imani /dini bora kuliko nyingine kwa mujibu ya katiba yetu (ila kuna dini /imani zenye wafuasi wengi) na dini zote zina haki sawa mbele ya katiba yetu ambayo ndio sheria mama na muongozo wa utawala!
 
Nimeshawahi kuleta mada inafanana hivi kuwa hapa nchini kuna watanzania wenzetu ambao wana asili ya Asia.Wana dini yao inaitwa Hindu pia wapo Sikh na pia Buddha.Kwanini wako nyuma ya pazia kwenye kuliombea taifa au hafla za kitaifa nao hawajitokezi ilhali ni watanzania wenzetu?

JIBU NI RAHISI MTOA MADA NAOMBA NILIANDIKE INFERIORITY COMPLEX KWA DINI ZA ASILI NA DINI AMBAZO SIO ZA IBRAHIM(ukristo na uislam)
Ni nyerere tu alivyofariki mkuu wa dini ya Hindi Nyerere alipokuwa anaombewa naye alijitokeza akamuombea.

Naomba nimnukuu askofu Desmond Tutu ''Wakoloni walivyokuja tulikuwa na dini zetu wakatuletea biblia.Wakatuambia tufunge macho tuombe.Tulipofunga macho na kuomba baada ya kufungua tu tukakuta wamechukua ardhi yetu na sisi tumebaki na biblia''-------mwisho wa kunukuu
 
Nimeshawahi kuleta mada inafanana hivi kuwa hapa nchini kuna watanzania wenzetu ambao wana asili ya Asia.Wana dini yao inaitwa Hindu pia wapo Sikh na pia Buddha.Kwanini wako nyuma ya pazia kwenye kuliombea taifa au hafla za kitaifa nao hawajitokezi ilhali ni watanzania wenzetu?
JIBU NI RAHISI MTOA MADA NAOMBA NILIANDIKE INFERIORITY COMPLEX
Ni nyerere tu alivyofariki mkuu wa dini ya Hindi Nyerere alipokuwa anaombewa naye alijitokeza akamuombea.
Kwakiasi Fulani naweza kukubaliana na wewe mkuu, japo sio moja kwa moja boss wangu,

Nikweli inawezekana hii dhana ya inferiority complex yaani kujiona wao wanyonge, wako chini sana, hawastahili kuhudhuria au kujumuika na viongozi wenzao wa dini kubwa katika masuala ya kuliombea taifa ,

Lakini pia mkuu, kuna hili suala la mialiko, dini hizi kubwa hupewa kipaumbele sana na viongozi wetu wa serikali, hasa pengine kwasababu na wao ni waumini (au wafuasi) wa dini hizo, hii inaweza sana kuziweka mbele dini /imani hizi kubwa, ni rahisi kumuona kiongozi wa serikali kwenda kwa askofu/padre/Mchungaji/kasisi/ au mufti/sheikh/ustaadhi /maalim kutaka ushauri/Maombi /dua n.k au kuwaalika viongozi hao wadini ikulu au kukutana nao sehemu Fulani/ kuwajengea nyumbani za ibada na hata kuwapigia simu kuwapa mialiko Fulani Fulani

Lakini sio rahisi kuona mambo kama hayo kwa viongozi wa dini za asili, pengine viongozi wetu nao wana inferior complex ya kujidharau au kudharau imani zetu za asili, au pengine kuona jamii yetu inazichukulia imani zetu za asili kama ushetani au ushenzi au ushirikina hivyo viongozi kuonekana kwenda huko ni kujidhalilisha na kujipunguzia hadhi /heshima yake katika jamii inayomzunguka!

Au pengine viongozi wetu wanafanya hivi kutafuta wapiga kura wao kisiasa, maana dini kubwa mbili (ukristo na uislam) zina waumini wengi sana (wapiga kura) na zina ushawishi mkubwa kwenye jamii kulinganisha na dini za asili?! Pia ziko well organised kulinganisha na dini za asili ambazo ni makundi madogo madogo yasiyo na umoja kama madhehebu ya ukristo na uislam?!

Sasa mkuu nashindwa kuelewa hasa hii inferiority complex iko kwa viongozi wa dini za asili au viongozi wa serikali?!
 
Ukitaka kuelewa haya mabo rudi nyuma rudi nyuma anzia mwanzo nasema rudi nyumaa ukidandia kwa juu hutaweza kuelewa.
 
Acha uhuni mkuu, tunataka dini inayomwabudu Mungu aliyejuu aliyeviumba viumbe vyote vilivyomo na visivyo onekana. Mungu aliyeumba mito, jua, nyota, mbingu, dunia.
Hizo dini zingine zinawaabudu watu, zinawaabudu mizimu ya mababu ambao wote hao waliumbwa na Mungu aliyeziumba mbingu na nchi


Cha kushangaza zaidi, utakuta eti na wewe Ni kichwa Cha familia fulani
 
Mzungu ukristo
Muarabu uislamu
Mu asia buddha
Kuna jews ajili ya mataifa flan flan

Muafrica ni kama hastahili kuwa na dini yaani africa ni soko huria kutangaza dini zao.Sijui imekuaje kuaje mpk imani zetu zimekuwa ushetani na nguvu za giza. Ina maana sisi wazee wetu hawana jema,mizimu yetu tu ndo mashetani?mbona wahindi wanaabudu hadi ng’ombe!nyoka!watu!

Nadhani kuwa watu flani flani walijua dini zetu zinanguvu sasa wakataka kuzibadili lkn swali ni je tunawabadilishia tunawapa dini gani?????Pili,hawa wapuuzi walijua wakitufanya tuchukie utamaduni wetu na imani zetu halfu tukapenda za kwao ni rahisi sana kututawala.

Dini zinakuja ili tutawalike kirahisi na kimsingi Dini zote zinafundisha basics priniciple ambazo ni imani,msamaha,maombi,ibada,matendo mema yaani kifupi mpagani akifanya hayo ana nguvu sawa na mshika dini...

usizini inayozungumzia kwenye biblia ndo ile ile ya kwenye quaran sema tu lugha tofauti uwasilishaji tofauti.Ukweli huu unahitaji uwe na akili huru sana..

Leo hii hata kunywa dawa ya asili unaonekana mshirikina!!!unaonekana mshamba!
exactly
 
Acha uhuni mkuu, tunataka dini inayomwabudu Mungu aliyejuu aliyeviumba viumbe vyote vilivyomo na visivyo onekana. Mungu aliyeumba mito, jua, nyota, mbingu, dunia.
Hizo dini zingine zinawaabudu watu, zinawaabudu mizimu ya mababu ambao wote hao waliumbwa na Mungu aliyeziumba mbingu na nchi
Mnaabudu mizimu ya kiyahudi, kina marehemu Yesu na wengine
 
Kwa jina la Yesu, nakufungua katika vifungo vya kuto jitambua na kutomtambua Mungu wa kweli. Ndugu zako walikufunga ili usiweze kutafakari lakini Leo anakwenda kubadirisha ufahamu wako kwa jina la Yesu nafungua ufahamu wako ili umjue Yesu Kristo Mungu alive hai. Katika jina la Yesu Kristo Mungu aliyehai amen.
Hana lolote. Mtu alishakufa miaka mingi nyuma huko kwao akusikie wewe mmatumbi
 
Back
Top Bottom