Loyalist
JF-Expert Member
- Aug 28, 2020
- 411
- 894
- Thread starter
- #101
Mkuu hauko mbali sana na maana halisi inayozingatiwa hapa, tatizo ni mtazamo tu mkuu,Mkuu dini na imani hayo ni maneno mawili tofauti,lazima ujue neno imani linasimama vp lenyewe na neno dini linasimama vp. Mtu akikuuliza "wewe ni imani gani?" haina maana moja kwa moja anaulizia dini,unaweza usiwe na dini ila ukawa unaamini Mungu tu au chochote ila hauamini dini.
Sasa hayo waliyokuwa wanayafanya wazee wetu kama hayo ya matambiko sijui kuomba mizimu yalikuwa ni sehemu ya masuala yenye kuhusu jamii kuendana mila zao.
Sasa wewe umechukua hayo masuala tu na kuyaita dini wakati nachojua dini ni zaidi ya ibada(kuabudu).
Uislamu sio tu kuswali swala tano au ukristo kwenda kanisani kufanya ibada.
Umewahi kusikia kuhusu neno DINI ZA ASILI...???!!!!
ulidhani ni dini gani?! Uislam na ukristo au?!
Serikali yenyewe inatambua kuwepo kwa dini za asili, narudia tena dini za asili, ndio ni dini za asili,
Usidhani kwamba waafrika hawakuwa na dini zao wenyewe kabla ya kuja kwa wakoloni au wageni Wa mwanzo nope! Zilikuwepo mkuu, dini sio lazima kuwe na msikiti au kanisa, au kuvaa kanzu au msalaba! Au kuwe na kitabu cha Quran au Biblia, au nguzo tano au riturjia!
Taratibu zozote za ibada ni dini kamili, hata wazee wetu wakipokuwa wanaabudu chini ya miti, mapangoni, misituni na kutoa matambiko na kafara hizo ni dini kamili mkuu,,,