Ingekuwa vyema kama ungezitaja hizo dini za afrika ambazo tulikuwa nazo kabla ya hizo za kuja.
Mkuu, dini za asili au za jadi hazinaga majina kama brand za kibiashara, maana hizi za kikoloni za kuletwa na meli na majahazi zina majina mengi,
Kila kabila au jamii inaijua dini yake au imani yake, iliyokuwa inaifuata kabla ya kufika kwa wageni wa mwanzo, waarabu, wazungu na wahindi hata Wachina (Buddha, Tao nk).
Ukisema utaje majina sidhani kama tutaelewana au hata thread itatosha hii, majina ya dini za asili yako mengi kulingana na lugha ya kabila husika, mfano wazaramo, wachagga, wasambaa, wazigua, wangazija, wasukuma, wahaya,wamakonde, wamwela, wangoni, wayao, wagogo, wanyamwezi,waha,wangindo, wanyakyusa, n.k. kila kabila lilikuwa na imani yake au dini yake waliyokuwa wanaitumia kufanya ibada na Maombi kwenye matukio mbalimbali mfano:
majanga ya asili kama ukame (wanapoomba mvua), kubariki watoto wanapozaliwa, jando na unyago, ndoa, mavuno, ugonjwa hata vita!