Swali ni kwamba una uhakika na ushahidi kwamba Lema, Sugu na Boni walisema hayo?
Tunachotaka ni proof siyo kwenda na habari za kusikia.
Seriously? Unataka sasa mpaka usikie recording ya Lema, Sugu na Boni ndio uamini? Au unataka minutes za kikao husika? Wewe hauoni kukaa kimya kwao kunatia wasiwasi? Na sio wao tu, hakuna hata kiongozi mmoja aliyekuwepo anayekanusha tukio hilo.
Mnyika kasema yeye ndiye anatunza pesa na zipo salama. Iwe kweli au uongo tumesikia kutoka kinywa chake
Habibu Mchange akisema Lema, Boni na Sugu walisema, huo si ukweli achilia mbali credibility yake.
Shutuma sio pesa zilizokuwa kwenye akaunti za Chadema zimeliwa. Shutuma ni kuwa Heche amekuwa hafikishi pesa anazopewa kwa ajili ya Chadema. Shutuma ni kuwa anaziingiza kwenye akaunti yake binafsi. Katika hali hiyo Mnyika anahusika vipi? Au KM anasimamia pia akaunti binafsi ya Heche?
Kinacho shangaza ni kuwa ili kujibu tuhuma hizi ametokeza mfanya biashara mmoja na kusema kuwa ana uhusiano wa kibiashara na Heche na pesa anazompa sio kwa ajili ya matumizi ya Chadema. Amesema pia kuwa huwa anachangia pia CCM. Hili nalo lina shida ethically kwa Heche kama hakuwaambia wenzake kuhusu mahusiano na huyo mfanyabiashara. Aidha, linatia wasiwasi kuwa huyo mfanyabiashara atakuwa na leverage juu yake pale chama chake kitakapo shika dola.
Hata kama walisema, je, walitoa ushahidi? na nani wa kutuhumiwa Katibu mkuu au Heche?
Kwanini wanasema HECHE na si Makamu Mwenyekiti.
Toa mfano wa hicho unachoita kuwa ni ushahidi.
Kwa nini Mnyika ahusishwe wakati katika maelezo yao Katibu Mkuu hakuhusika?
Inawezekana wanasema Heche kwa sababu tuhuma ni kuwa alizihujumu kama Heche na sio kama Mwenyekiti. Wanadai michango hiyo iliingizwa kwenye akaunti ya Heche na sio ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema.
Ushihidi wa MBOWE upo. Walimtoa magereza wakamkimbiza Ikulu. Kutokea hapo Mbowe akabadilika. Walikaa na Mbowe mwaka wakizungumza mwisho wa siku zero
I am sorry, but this is pure nonsence. Hakuna ushahidi kuwa Mbowe alipelekwa Ikulu. Mbowe ana usafiri wake na anasema kuwa alialikwa na Rais kwenda Ikulu hivyo akaenda. Hajawahi kuficha kuwa alienda. Amesema pia kuwa aliwapa viongozi wenzake taarifa ya mazungumzo hayo. Hakuna kiongozi aliyesema kuwa hakupata taarifa.
Mbowe hajawahi kuficha kuwa anapendelea zaidi dialogue kuliko confrontation. Hata wakati wa JPM alienda Mwanza kuomba wazungumze. Hapo kosa liko wapi? Mandela aliongea na De Klerk. Martin Luther King Junior aliongea na Lyndon Johnson. Hamas wameongea na Israel wakati watu wao wanafanyiwa unyama. Iran inaongea na USA. Zelensky anataka mazungumzo na Putin. Wote hawa ni wasaliti?
Mmoja wa waliofaidika na hayo mazungumzo ni Lissu. Aidha, mamia ya wafuasi wa Chadema waliondolewa magerezani na kesi zao kufutwa kutokana na hayo mazungumzo. Zuio la mikutano ya hadhara liliondolewa na Chadema walitumia fursa hiyo kikamilifu kwa kufanya mikutano ya hadhara mingi ambayo baadhi ilihutubiwa na Lissu na wenzie.
Mbowe aliendelea kuita maandamano hata pale ambapo hao mashujaa wenu walijificha. Na CCM waliposema kuwa anawachuuza watoto wa wengine, aliongozana na binti yake. Nakumbuka picha ya Hilda akiwa amejificha ili askari wasimuone.
Lissu aliposhambuliwa Mbeya, Mbowe alikimbilia kwenda kusimama nae ingawa alijua thika kuwa angeweza kukamatwa. Na kweli alikamatwa. Mbowe alichangia zaidi ya milioni 200 ili kuwezesha Mkutano Mkuu wa Chama. Lissu alisema yeye sio tajiri hivyo hawezi kuchangia.
Pamoja na kambi ya Lissu kudai kuwa hujuma zitafanyika katika uchaguzi huo, uchaguzi uliendeshwa kwa uwazi ambao ni nadra katika chaguzi tulizo zoea. Na Mbowe aliposhindwa alikubali na kumpongeza Lissu. Katika yote haya huo ushahidi wa kununuliwa na Samia uko wapi? Ni fitna tu.
Mbowe alisema kwa ushahidi kwamba kuna wenzetu walishiriki kuharibu maridhiano! Ushahidi kwamba yeye na CCM walikuwa na mitazamo sawa.
Kwani ni uongo? Kuna ubaya gani katika kutaka mazungumzo na mpinzani wako? Sio upande wa Chadema peke yake ndio kulikuwa na wasiotaka maridhiano, Kinana nae alisema wazi kuwa CCM nako kuna waliokuwa wanapinga mazungumxo hayo. Aidha, hakuna mtu anayeingia katika mazungumzo anaingia ili yashindwe. Lakini akiona mwenzie hana nia njema, anajitoa. Na ndivyo alivyofanya Mbowe. Ni ishara ya maturity.
Mkandara, MBOWE alifanya madudu sana! hilo linahitaji ushahidi kweli.
Hakuna kiongozi asiyefanya madudu. Ni sehemu ya uongozi. Kiongozi anapimwa kwa ujumla wa matendo yake. Ku cherry pick makosa sio kumtendea haki.
Ndiye wanamtaka au photocopy yake
CCM hawajawahi kumtaka Mbowe. Machawa wa CCM walimpigia kampeni za wazi ili Chadema wahisi amenunuliwa na hivyo waamue kumpigia kura mshindani wake. CCM walimtaka Lissu kwa sababu walijua atawapa fursa ya kukibana Chadema na kukitoa kwenye uchaguzi. Na kweli walifanikiwa. Na walijua kuwa pamoja na kelele zao kambi ya Lissu hawana ujasiri wa Mbowe. Mbowe aliita maandamano dhidi ya utawala pamoja na dola kuyakataza. Alifanya mikutano, pamoja na watu wake kuzuiwa na wakati mwingine. Mbowe na wenzake walifanya creative civic disobedience. Wakina Husna walikataa kushusha bendera ya chama chao Chato. Wakina Mwakipesile na wenzake walijigala gala nje ya ubalozi wa Marekani. Mwakipesile alikaa ndani lakini alikataa kuwataja wenzake. Wakina Ruge, Halima na wengine wengi walikaa sana rumande. Sugu alifungwa. Mbowe na wenzake nao walifungwa. Heche alipotoka alisema Mbowe alikataa kutoka jela mpaka wenzake wote wametoka. Tuambie Chadema ya Lissu imeandaa maandamano mangapi?
Yote hayo mnataka kutuaminisha kuwa CCM walimtaka Mbowe kuliko hao wa sasa ambao wanangoja wapewe kibali ili waandamane na kufanya mikutano ya hadhara! CCM wana mmwagia masifa Mbowe ili asikubalike ndani ya Chadema.
Na kwa kiasi fulani wamefanikiwa maana kuna blind hatred dhidi ya Mbowe kiasi ya watu kukataa kuona ushahidi ulio machoni mwao. CCM wanatazama 2030, na watahakikisha kuwa ifikapo hapo Chadema inakuwa kibogoyo. Unfortunately, watu kama nyie mna wa facilitate kufikia kwenye adhma hiyo.
Ni kweli, na bahati nzuri sisi wengine tulikemea hilo kwa msingi ule ule kwamba EL alikuwa fisadi kwa ushahidi
Hapo ndipo Mbowe alionyesha pragmatism. EL alichangia Chadema kupata wageni wengi. Kura alizopata ziliwapa wabunge wa viti maalum wengi na ruzuku ambayo iliwawezesha kukijenga chama chao. Ile ruzuku na uwepo wa wabunge wao ndio ulionyesha watanzania kuwa kuna alternative to CCM. Ujasiri wao chini ya Mbowe wa kukataa kunyamazishwa ndio umefikisha Chadema hapa ilipo. Viongozi wengi wa Chadema wanakiri kuwa Mbowe ana mchango mkubwa katika uwepo wao kwenye siasa.
Chadema ya Mbowe ilikuwa na wigo kubwa la viongozi mahiri na jasiri kiasi kuwa hata alipokuwa ndani chama chake kiliendelea kuisumbua CCM. Bawacha, Bavicha na Bazecha wote walishiriki kikamilifu na walipewa nafasi za kung'ara chini ya Mbowe. Yote haya yaliwezeshwa kwa kiasi kikubwa na master stroke ya kumtumia Lowassa. Hivi ukimuondoa Heche ni kiongozi gani wa sasa wa Chadema anaweza kuumudu u makamu Mwenyekiti? Sugu? Boni Yai?
Ninachoshangaa ni kuwa hamuonyeshi outrage kwa chama kumkumbatia kiongozi wao ambae aliandika kitabu kukihusisha kilichokuwa chama chake na utekaji na utesaji wa wanachama wake.
Hamuonyeshi outrage kwa kumpokea kiongozi ambae alihamia upande wa pili na kukichafua sana chama chake akiwa amevaa kijani na amebeba picha ya Mwenyekiti wa CCM.
Huu ni unafik mtupu.
Amandla....