Kwako Waziri wa Elimu; Crash program shule za msingi zinatuharibia watoto

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,241
4,466
Hivi karibuni kumejengeka tabia ya shule nyingi za msingi, hasa za binafsi kuanzisha masomo ya ziada yanayoitwa CRASH PROGRAM.

Programu hii huhusisha masomo ya ziada kwa wanafunzi wa shule za msingi wa darasa la nne na la saba (hata la sita) kwa ajili ya kuwaandaa wanafunzi kwa ajili ya mitihani ya madarasa husika.

Katika mipango hii watoto kuwawahishwa darasani asubuhi na mapema (kwa day scholars na boarders) na kuwaachia usiku, huku shule nyingine zikikaa na wanafunzi darasani hadi saa mbili usiku.

Muda wote huo wanafunzi hubaki darasani ili wajifunze vitu vinavyoitwa vya ziada ati kwa nia ya kumaliza mitaala.

Hii ikimaanisha kuwa wanafunzi wa madarasa haya, wakisoma kwa utaratibu wa kawaida, hawawezi maliza mitaala yao.

Kwa watoto wa darasa la nne, ambao wengi wana miaka kati ya 8 hadi 10, kuwakalisha zaidi ya masaa tisa darasani kunaweza leta athari za kudumu.

Kipindi hiki watoto wanapaswa wapate elimu, lakini muhimu pia wanahitaji muda wa kutosha wa kupumzika na kufanya mambo mengine ya kijamii yatakayo kuza ujuzi muhimu, kuongeza uwezo wa kufikiri, kujenga hamu ya kujua jinsi mambo yanavyofanya kazi na jinsi yanavyotengenezwa n.k.

Bahati mbaya sana shule zinawaandaa watoto wafaulu mtihani kwa kuwakalisha madarani kwa masaa zaidi ya 9 kitu ambacho hata ubongo wao unazidiwa.

Hivi kuna umuhimu gani wa mtoto wa darasa la nne kukaa crash program? Kitu gani cha msingi anafundishwa ambacho hakiwezi tolewa katika masaa ya kawaida ya shule? Huyo mtoto atapumzika saa ngapi?

Tuna mifano yoyote ya watoto waliopita katika mfumo huo ambao walifanya vizuri zaidi walipoingia kwenye soko la ajira?

Hizi crash program zimekuwa ni chanzo cha mapato kwa walimu na shule, maana mambo waliyopaswa kuwafundisha watoto wa shule ya msingi ndani ya muda uliopangwa na serikali, hufanyika nje ya muda.

Mimi naamini elimu ya watoto inapaswa kuwasaidia watoto kuwakuza haiba, vipaji na uwezo wao. Isiwe elimu ya kuwalazimisha wafaulu kwa viwango fulani.

Inapaswa kuwafundisha kuelewa haki zao wenyewe, na kuheshimu haki, tamaduni na tofauti za watu wengine.

Hii kitu ikatazwe mashuleni. Watoto wapate muda wa kupumzika na kucheza.
 
  • Thanks
Reactions: BRN
Ni ujinga ambao hata shule za English Medium ambazo zamani tuliziona za maana wanafanya sasa hivi.

Yani shuke ina walimu wazuri, kila mtoto anamiliki kitabu chake, wanafunzi 30 tu mkondo mmoja, ada unalipa zaidi ya milioni, chakula wanakula shuleni eti bado nao wanaanzisha huu upuuzi wa Crsh program!

Inaudhi sana. Wizara ya Afya Tanzania hili linaafya gani kwa makuzi ya mtoto?....Wiraza ya Elimu hasa sehemu ya Uthibiti Ubora, Ualimu ElimuMsingi na TAMISEMI haya hamyaoni? ...mnasubiri hadi Mh. Rais azungumze ndipo mu act?
 
Kwanza hiyo haiitwi Crush Programme. Crush Programme ni kitu tofauti kabisa. Wao wanafanya Remedial Classes (Mafunzo Rekebishi) na Serikali inayakubali baada ya kukataa tuitions. Binafsi nimeridhia mwanangu wa darasa la saba afanye haya mafunzo mwasababu kwanza hayana malipo na yanamkeep bize binti yangu badala ya kuangalia series. Kama wa kwako ni kilaza na hata huko kwenye mafunzo rekebishi unaona anapoteza, mzuie asisome.
 
Hivi karibuni kumejengeka tabia ya shule nyingi za msingi, hasa za binafsi kuanzisha masomo ya ziada yanayoitwa CRASH PROGRAM.

Programu hii huhusisha masomo ya ziada kwa wanafunzi wa shule za msingi wa darasa la nne na la saba (hata la sita) kwa ajili ya kuwaandaa wanafunzi kwa ajili ya mitihani ya madarasa husika.

Katika mipango hii watoto kuwawahishwa darasani asubuhi na mapema (kwa day scholars na boarders) na kuwaachia usiku, huku shule nyingine zikikaa na wanafunzi darasani hadi saa mbili usiku.

Muda wote huo wanafunzi hubaki darasani ili wajifunze vitu vinavyoitwa vya ziada ati kwa nia ya kumaliza mitaala.

Hii ikimaanisha kuwa wanafunzi wa madarasa haya, wakisoma kwa utaratibu wa kawaida, hawawezi maliza mitaala yao.

Kwa watoto wa darasa la nne, ambao wengi wana miaka kati ya 8 hadi 10, kuwakalisha zaidi ya masaa tisa darasani kunaweza leta athari za kudumu.

Kipindi hiki watoto wanapaswa wapate elimu, lakini muhimu pia wanahitaji muda wa kutosha wa kupumzika na kufanya mambo mengine ya kijamii yatakayo kuza ujuzi muhimu, kuongeza uwezo wa kufikiri, kujenga hamu ya kujua jinsi mambo yanavyofanya kazi na jinsi yanavyotengenezwa n.k.

Bahati mbaya sana shule zinawaandaa watoto wafaulu mtihani kwa kuwakalisha madarani kwa masaa zaidi ya 9 kitu ambacho hata ubongo wao unazidiwa.

Hivi kuna umuhimu gani wa mtoto wa darasa la nne kukaa crash program? Kitu gani cha msingi anafundishwa ambacho hakiwezi tolewa katika masaa ya kawaida ya shule? Huyo mtoto atapumzika saa ngapi?

Tuna mifano yoyote ya watoto waliopita katika mfumo huo ambao walifanya vizuri zaidi walipoingia kwenye soko la ajira?

Hizi crash program zimekuwa ni chanzo cha mapato kwa walimu na shule, maana mambo waliyopaswa kuwafundisha watoto wa shule ya msingi ndani ya muda uliopangwa na serikali, hufanyika nje ya muda.

Mimi naamini elimu ya watoto inapaswa kuwasaidia watoto kuwakuza haiba, vipaji na uwezo wao. Isiwe elimu ya kuwalazimisha wafaulu kwa viwango fulani.

Inapaswa kuwafundisha kuelewa haki zao wenyewe, na kuheshimu haki, tamaduni na tofauti za watu wengine.

Hii kitu ikatazwe mashuleni. Watoto wapate muda wa kupumzika na kucheza.
Umelazimishwa kupeleka watoto wako shule hizo, ficha ujinga wako kidogo. Fyuuu
 
Jinsi unavyojifunza vitu. ndivyo akili inavyokoma na kufanya kazi vizuri. , pia naamini. kwenye kujifunza kwao kote , mtoto lazima atapata masaa yake nane ya kupumzika, kwahiyo punguza hofu. watapumzika wakimaliza.
 
Hivi karibuni kumejengeka tabia ya shule nyingi za msingi, hasa za binafsi kuanzisha masomo ya ziada yanayoitwa CRASH PROGRAM.

Programu hii huhusisha masomo ya ziada kwa wanafunzi wa shule za msingi wa darasa la nne na la saba (hata la sita) kwa ajili ya kuwaandaa wanafunzi kwa ajili ya mitihani ya madarasa husika.

Katika mipango hii watoto kuwawahishwa darasani asubuhi na mapema (kwa day scholars na boarders) na kuwaachia usiku, huku shule nyingine zikikaa na wanafunzi darasani hadi saa mbili usiku.

Muda wote huo wanafunzi hubaki darasani ili wajifunze vitu vinavyoitwa vya ziada ati kwa nia ya kumaliza mitaala.

Hii ikimaanisha kuwa wanafunzi wa madarasa haya, wakisoma kwa utaratibu wa kawaida, hawawezi maliza mitaala yao.

Kwa watoto wa darasa la nne, ambao wengi wana miaka kati ya 8 hadi 10, kuwakalisha zaidi ya masaa tisa darasani kunaweza leta athari za kudumu.

Kipindi hiki watoto wanapaswa wapate elimu, lakini muhimu pia wanahitaji muda wa kutosha wa kupumzika na kufanya mambo mengine ya kijamii yatakayo kuza ujuzi muhimu, kuongeza uwezo wa kufikiri, kujenga hamu ya kujua jinsi mambo yanavyofanya kazi na jinsi yanavyotengenezwa n.k.

Bahati mbaya sana shule zinawaandaa watoto wafaulu mtihani kwa kuwakalisha madarani kwa masaa zaidi ya 9 kitu ambacho hata ubongo wao unazidiwa.

Hivi kuna umuhimu gani wa mtoto wa darasa la nne kukaa crash program? Kitu gani cha msingi anafundishwa ambacho hakiwezi tolewa katika masaa ya kawaida ya shule? Huyo mtoto atapumzika saa ngapi?

Tuna mifano yoyote ya watoto waliopita katika mfumo huo ambao walifanya vizuri zaidi walipoingia kwenye soko la ajira?

Hizi crash program zimekuwa ni chanzo cha mapato kwa walimu na shule, maana mambo waliyopaswa kuwafundisha watoto wa shule ya msingi ndani ya muda uliopangwa na serikali, hufanyika nje ya muda.

Mimi naamini elimu ya watoto inapaswa kuwasaidia watoto kuwakuza haiba, vipaji na uwezo wao. Isiwe elimu ya kuwalazimisha wafaulu kwa viwango fulani.

Inapaswa kuwafundisha kuelewa haki zao wenyewe, na kuheshimu haki, tamaduni na tofauti za watu wengine.

Hii kitu ikatazwe mashuleni. Watoto wapate muda wa kupumzika na kucheza.
Umeongea point mmmno... mmmno....
binafsi huwa najiuliza wizara ya elimu na tamisemi hawana wataalamu wakuyaona haya na kurekebisha haraka???
Tunawatu maofisini very very bogus and stupid kwakweli!
Hasa hizi english medium zinaharibu sana watoto na taifa hili kwa kuzalisha vijana wenye vyeti vizuuuri lakini very poor mind set and innovations...
Licheti linama 'A' kibao lakini kijana hajui basic issues za maisha na mvivu wakazi... hawezi kufuga? Hawezi kilimo hata bustani, usafi na ubunifu poor,hawezi kukabili changamoto zakitaa wanakimbilia pombe(kuji-zungusha wanakunywaga wine wanajidai watasha),
Wanachojua nikuongea kingreza chakooni na kuchomekea.
YOU POOR ENGLISH MEDIUM SCHOOLS (MANY) wapumzisheni watoto wetu, wafundisheni maigizo,michezo,ngomazetu, innovations muwatransform Kuwa reliable citizen badala yakuwakaririsha masomo kiiiilamuda ili shulezenu zionekane zinafaulisha saana mitihani!!! Stop that nonsense...
Dont look for money and eminence..look for standards and quality education....
 
Haya ni madhara ya kushindanisha mashule.
Shule zinakuwa under pressure ya kupata A’s tu.
Wanakaririshwa tu maswali na “mbinu” za kujibu mitihani.
 
Back
Top Bottom