Kwa watumiaji wa Google Pixel

Kwa watumiaji wa Google Pixel

Biashara nyingine hii hapa wadau
Google Pixel 3 128GB Storage
Clean used US Stock
325,000 - simu na charger
0764081567
Dar es salaam

PXL_20221206_154633644~2.jpg

PXL_20221206_154702139.jpg
 


Mi nilianza 3 na 3a sahivi nipo 4, mwakani January napiga 5 December 6 Pro.

Sema Google kwenye hardware wanafail. 3 battery ilivimba, 3a sio waterproof iliingia maji yaan mvua kdg sana, 4 ipo poa sema battery dogo sana bora uende 4a.
How much is 4a?
 
Nilitoka Pixel 3a nikaenda 11 ndio nimekuja 4.

3a nilinunua 350 enzi zile (mwezi wa 11 au 12 mwaka jana) iphone 11 nikanunua Mil 1.2 (Mwezi wa 2 au 3) na Pixel 4 nimenunua 520 Mwezi wa 8.

Kusema kweli thamani ya Mil 1 na zaidi sikuiona. Especially kwa mimi ambae kifaa pekee cha Apple ni iPhone.

Ila kama una airpods, Apple watch, Mac, Apple TV etc ndio iPhone itafaa.

Pia kwenye picha, kusema kweli iPhone 11 bado sana kwa Pixel 4. Na screen ya iPhone 11 sio nzuri ata compare na iPhone X. Kuna watu uwa wanasema iPhone 11 ni upgrade ya iPhone XR na sio XS.

Sema iPhone kingine jiwe, ukiiangusha ina possibility kubwa ya kusurvive ila huyu Pixel naogopa nahisi akienda chini, msiba.
Chama la iPhone ni lingine kabisa mkuu ila camera kali inaanzia 12 Pro max hii ni moto kwenye selfie
Nipo kwenye 13 Pro max ni moto sana kwenye video na kibiashara
video it's the best sana

Naenda iPhone 14 Pro max soon ni mnyama kwa vyote front camera na back


Pia Google nimeona mnaisifia sana night shot mbona kwa iPhone ni jambo la kawaida sana hilo
 
Pixel inayokaa na chaji ni 5A tu,
Kunakipindi nilikuomba ushauri wa sim yenye camera kali ukanishauri nichukue Redmi note 10 duh! Nilivyoenda dukani nikaikuta bei imechangamka sana mpaka nikajichanganya nikachukua Redmi 10 . Nilivyo chukuaga Google pixel nikajiuliza huyu Chief-Mkwawa kwanini hakunishauri kuhusu Google pixel?
 
Back
Top Bottom