Wakuu nimemaliza kuangalia kitu kimoja kikali sana! "The Social Media Butterfly"! Nimekipenda sana, kwa ufupi ni Story ya Mrembo Jasmine na Blazaman Andreas!
Jasmine 22,/Mrefu, mtamu, nywele ndefu na amechora tatoo ya UA hapa uani kwake kiunoni! Anaachwa na ndege na anakutana na Kijana barubaru Andreas ambaye anafanya kazi ya muda Uwanja wa ndege kama security officer.
Ghafla mahaba yanageuka kuwa mahabati. Jasmine mlimmwende, mamaa ya social media, kila kitu lazima aposti, ana followers kama wote, anajikuta kakolea kwa Mlinzi, dogo anaishi kwenye apartment matata.
Kwa kufupisha, Andreas hapendezewi na tabia ya kuwa online kwa Jasmine na kila mtu kupost comment kwa page yake, yaani kama vile WIVU flani hivi amazing.
Ugomvi unaanza, wanaanza kuchunguzana kwenye simu soma chats za huyu, soma chats za yule kisirisiri. Jasmine siku moja alipochoka kutuhumiwa akaamua na yeye aingie kwenye page ya Mshakaji, akakuta kumbe jamaa dah! Hajawahi hata kusema kuwa yuko kwa relationship.
Jasmine akampigia Dada yake kumweleza but kabla hajamaliza jamaa akawa anafka na hapo ndio ilikua mwisho wa Jasmine kuwasiliana na Dada yake Melanie!
Kumbe jamaa alimuua na kumchoma moto ili isigundulike Bahati mbaya kilichosaidia ni alama ile ya tatoo aliyojichora Jasmine miaka mitatu nyumba! Police wa Virginia wakapost taarifa hizo huku wakionyesha alama hio, classmate wa Jasmine akaiona akampigia Melanie na kumjulisha, ukumbuke muda huo wameshatafuta kwenye ile apartment bila kufanikiwa but laptop nakibanio cha nywele na viwalo vyake vilikuepo hali ambayo iliashiria kitu kibaya kutokea maana kwa mujibu wa Dada yake Jasmine asingeweza kwenda popote bila hivyo vitu viwili. Ndio ikawa confirmed kuwa mwanamke huyo ni Jasmine. Jasmine ametutoka.
Katikati ya confusion Melanie akakumbuka kuwa gari ya Andreas ilikua zimefungwa tracking device hivyo akawajulisha Police ambao alikua nao mida hio! Gari ikaonekana iko mitaa ya Virginia, police wakawasiliana ili kuikamata gari hio, iliposimamishwa kweli Driver alikua Andreas, baada ya kuona ni askari akakimbia but baadae alishuka kwenye gari akiwa na silaha kisha kufanya maamuzi ya kujipiga risasi kidevuni.
Hivyo basi haikujulikana issue ilikua ni wivu tu au? Na je alimuua peke yake au alishirikiana na MTU?
Funzo, kama mchumba hapendi uwe mtu wa social media please acha!