Niliwahi kuishi na bro wangu pale Arusha miaka ya 2006, yeye kabla ya kufunga ndoa na mkewe tayari alikwishazaa nje watoto wa3, wakike yupo kateshi, wakike yupo mbulu na wakiume yupo kisongo ila hakuwa amemwambia mkewe.
Alipoamua kufunga ndoa mke wake wa sasa aliyezaa naye watoto wawili aliamua kutest zali la kumweleza mkewe na kwenda kumchukua yule mtoto wa kiume pale kisongo akiwa darasa la nne na kuja kuishi naye ngusero akisoma s/m sokoni one.
Maskini mtoto alinyanyaswa na kuteswa na yule shemeji mpaka huruma, akampa marufuku mama yake kuja kumwona pale nyumbani, shuleni wala kanisani au hata kuongea kwa simu.
Mtoto akawa anajaribu kutoroka kwenda kwa mama yake anakaa huko wk 2 basi akirudi pale home atasemwa na kusingiziwa kuwa katoka kuchukua madawa ya uchawi ya kumuua yule shemeji ili mama yake arudie ndoa na yule mtoto atanyolewa nywele zote za kichwani, kwapani mpaka matako.ni ili atolewe huo uchawi.
Hayo yalikuwa yanafanywa na shem bila bro kujua na kale katoto kalikuwa hakasemi ila alipokuja kugundua akaamua kumhamisha shule na kumpeleka kwa bibi yake huko songea ndo ikawa pona ya yule mtoto.
Baadhi ya wanawake ni makatili sana kwa watoto ambao sio wao na akipata mwanya wa kumfanya atakacho anamfanya kweli huyo mtoto.