Kwa waliozaa kabla ya ndoa

Kwa waliozaa kabla ya ndoa

Mimi natoa pesa za matumizi hukohuko. Sijui mama yake nae akiamua kuolewaaaa na kutaka iwe zamu yangu kumlea??? Daaah!! Yaani sitaki hata kufikiria hio situation..
 
Hakuna mwanamke anayeza kuishi na mtoto ambaye cyo wake huyo mtoto kama hatateswa basi huyo mama wa kambo hatamlea vzr maana hatajali maendeleo ya mtoto ktk kukuwa vema
 
Hili swala ni gumu na kuna baadhi ya wazazi wanafanya maamuzi mengine bila kufikiria.kuna Mdogo wangu alioa akiwa amezaa nje tiari,na mke aliyemuoa pia alikuwa na mtoto,mtoto wa Mdogo wangu anakaa na mama yake nje ya mkoa ila mtoto wa mkewe wanakaa nae ishu ilikuja kuwa ngumu pale ambapo mke wa Mdogo wangu alipokuja kumtukana mtoto kisa anaongea na babake Kwenye cm baba mtu alimind mno na kumuuliza mkewe sababu ya kufanya hivyo ilhali nae ana mtoto na wanakaa nae na anaongea na babake japo hana uhakika,mke alikataa kwamba mwanangu haongei na babake ambae yuko mkoani,hii ilimfanya Jamaa awe na asira na ameapa kumvizia mtoto huyo na akikuta anaongea na babake ndo itakuwa mwisho wa hiyo ndoa na atamfukuza mkewe Kwa kuwa alimfanya mjinga kumtukana mwanae ili hali mtoto wake anaongea na babake.maamuzi mengine inatakiwa kufikiria kabla ya kuamua
 
Binafsi sion ugumu hapo...mkeo ukiyenaye yupo sahihi...huyu wa nje ni mzazi mwenzako,usitake kujenga mazingira yakuharibu ndoa yako kwa swala lakizembe...ikishindikana mpe huyo mzazi mwenzako amlee,ukiona hawezi mlea basi fuata anachosema mkeo,kuwa upande wa mkeo halafu fikiria ingekuwa ni yeye jamaa wake wa zamani anakuja mtembelea ingekuwaje??
 
Ni rahisi kuhisi hivyo kwakuwa si mhusika wa tukio zima. Ukweli wa jambo hilo ndio huo vinginevyo siwezi jua kilichojificha ndani ya moyo wa mtu alienitendea hilo. Naamini MUNGU Mwenyezi anazo sababu.
Mkuu matola kama unataka kulithibitisha hili kwa faida ya jamii niko tayari njoo p.m nikupe contacts za wahusika wote wa tukio zima then uwahoji upate fact.

Na kuthibitisha pia may be GOD has purpose for this, hakimu aliehukumu kesi yangu baada ya kupata majanga yake kazini alinitafuta kuniomba msamaha akikiri kutokunitendea haki na anahisi yanayomkuta ni kama laana kutoka kwa MUNGU,mimi sijui kama madai ya hakimu huyo ni kweli au hisia zake tu, lakini hayo ndiyo yaliyonikuta kwa mwanaume yule.
Nampenda na kumshukuru MUNGU kwani hajaniacha peke yangu na haki yangu italipwa tu.
 
@MBEBA MAONO KAJA kwa nini wanakutendea yote hayo

Pole sana

Mungu wa Mbinguni atakufariji

Damu haipotei

Kila jambo linalotokea ni mpango wa Mungu

Huyo ni mwanao aliyekaa tumboni mwako 9 months.....ni wa kwako

Jipe moyo

There is one day utakuwa pamoja na mwanao

Story yako imenigusa sana

Pole

naamimi MUNGU anayo sababu ya jambo hili ingawa bado sijaijua.
 
Mpeleke mtoto boarding school visiting day Mama yake ataenda huko.

Ila una mtihani mgumu sana kimaisha wengi hapa hawaelewi ni wepesi tu kukushauri waonavyo.

Mtoto anahitaji kumjenga kisaikolojia kwa nini hauishi na Mama yake. Pole sana.

ushauri wako nadhani ndio bora kabisa kimtazamo wangu.
 
Best way to solve the issue. Mpeleke mtoto boarding school. Then likizo aende kwa mama yake wiki 2 na kwako wiki 2. Changamoto hapo ni utaratibu wa kumfuata huyo mtoto nyumbani kwa mama yake. Nafikiri hapo ni elimu kwa mke wako.
 
Mimi ni mwanaume nilibahatika kupata mtoto wa kiume nje ya ndoa.
Sasa miaka 10 baadae nimeoa na nimemchukua huyu mtoto wangu naishi naye.

Sasa mke wangu ameniwekea masharti ambayo nafikiri ni magumu kutekelezeka. Naamini kuwa mwanamke niliye zaa naye ana haki ya kumuoma mtoto wake kila anapohitaji kufanya hivyo.

Sasa mke wangu hataki huyu mama mtoto afike nyumbani kumuona. Hataki mtoto aende kwa mama yake. Anataka mama mtoto akitaka mtoto tumtume housegirl ampeleke mtoto hoteli foleni halafu wakimaliza kuongea arudi naye.

Hali hii imeniingiza kwenye migogoro maana mama mtoto anaona namnyanyasa na upande mwingine mke wangu anaona pia namnyanyasa.

Hebu niambieni what is the beat way ku deal na hii situation?

Sio vyema kwa mama mtoto wake kuja nyumbani kwako uishipo na mkeo.

Mkeo atakuwa hataki mtoto aende kwa mama ake either kuna kitu anaficha anaogopa kitajulikana , kuna malezi mema aliompa mtoto na najua kwamba akienda huko atabadilika. Maana kila mtu ana namna yake ya kulea au anawivu tuu.

Ila on the other side mkeo hayupo sahihi kwani mta mpastress mtoto . Na mama ake maana anae anahaki ya kuwa na mwanae.
 
Ukweli swala hili hutegemea ntu na ntu!
Kama umeamua kuishi na huyu, niwazi kitendo cha yule mzazi mwenzio kuja kuja hapo kwenu,
kutamfanya mkeo ahisi pengine mnaendeleza mahusiano hata kama sivyo.
Usiruhusu hali hio kwa maslahi ya ndoa yako.
Kaa ukijua Wanawake wana mambo ndugu!
Ukiruhusu hali hio hapo kwenu,
Kaa ukijua hata kama Mkeo alikua na upendo kwa mtoto wenu, upendo utapungua.
Maadam imeshindikana kuishi na mama yake.
Hakikisha mtoto anapata elimu kadiri ya uwezo wako.
Mengine haya ni sheeeeeedah!
 
kuwe na utaratibu maalum wa kuumuona mtoto, mwingine anajifanya anataka kuona mtoto kumbe ndio anajileta leta kijanja. ila kama mazingira yanaruhusu bora mtoto alelewe na mama yake mzazi tu.
Mkuu ni rahisi kuzungumza hivi Kama hayajakukuta! Muhimu ni mtoto kuwa na access ya kuwaona wazazi wote wawili Ktk mazingira ya upendo. Mke hahusiani kabisa na maamuzi ya jinsi ya mume wake kumwona mtoto. Ni maamuzi ya wawili hao waliomleta huyo mtoto duniani. Kwa nini mtoto akose haki yake ya msingi eti kwa sababu mke hapendezwi na jambo Fulani. Wanandoa wamekosa kuaminiana ndio shida inapoanza. Kama ni swala la mtoto na wazazi wa mtoto huyo hawana magomvi au hali ya kudhuriana basi ni haki ya mama kuja kumchukua mtoto nyumbani kwa baba yake hana lazima ya kuingia ndani ya nyumba vilevile kwa baba kumpeleka mtoto kwa mama yake. Kwa nini housegirl afanye jukumu lisilomhusu? Mke alipoolewa hakujua Kama kuna mtoto kama alilitambua basi akubaliane na mazingira yaliyopo ya mumewe kuwa na haki ya kumpenda na kumwona mtoto wake katika uaminifu kwamba yeye ni baba na mume wa mtu period. Mke naye atumie busara ya duniani mengi Kama amezaa basi ajue hii Hali inaweza kumkuta hata yeye na watoto wake. Tenda mema utalipwa mema
 
kweli mnashauri tu uyo mkeo anasababu mtt akienda kwa mama yake anarudi kitu cha ajabu!anarudi na misemo yakijinga na ugomvi haushi ndani!fikiria tu kama mkeo ndo angekua na mtoto?ungeruhusu bwana kuja?akipazoea atakuja hata ukiwa haupo ukisikia utaelewa?akifika mtoto anaumwa akataka kwenda hospitali na mkeo na mtoto utaelewa?
 
suala la kwanini hauishi nq mama yake halimuhusu tena akaepembeni kabisa mimi nilikuja gundua mtt anawaambia watt wangu kua mama yake nimzuri kuliko mimi embu niambieni
 
Achana nao wote...alafu ishi na mwanao tu..wasikuumize kichwa hao viumbe...
 
Wanaume tumeumbwa tumiliki vitu,mali ,na watoto na mama zao.mengine yote potezeni mda kujadili
 
wewe inaelekea hujaolewa jinsi unavyoreason. unadhani wewe ungekuwa na mtoto wa nje mmeo angeruhusu uliezaa nae aje aje kwako eti kumuona mtoto? na angekataa ungemlaumu kama unavyomsema mwanamke mwenzio eti ana visa visivyo na logic?!

nahisi uko kwenye nafasi kama ya huyo dada mwenye mtoto ndo maana unaongea kwa kuwa upande wake. khaaa!

katibasitti wewe ndio mke wa iMind nini?! Maana unaonyesha una hasira kweli kweli.

Anyway, punguza gadhabu ili ukisoma uelewe. Binafsi sijali kama mwenye mtoto ataruhusiwa kwenda kwa hao wanandoa au la. Nnachotetea mimi ni mtoto kuruhusiwa kwenda kwa mama yake na mama kuruhusiwa kuwa na mwanae, simple and clear.
 
Last edited by a moderator:
Umpe nafasi mama wa mtoto kukaa na mwanaye wakati mwingine hasa wa rikizo itapunguza uhitaji wa kuja kumtembelea mara kwa mara,ila mkeo naye asiwe insecure kiasi icho,after all those years bado anaona mzazi mwenzio ni tishio!!Lazima at one point ninyi kama wazazi mtaonana tu,ingawa siafiki swala la mzazi mwenza kuja hapo kwako.

Fuata ushauri huu
 
Back
Top Bottom