Kwa waliozaa kabla ya ndoa

Kwa waliozaa kabla ya ndoa

Nimeiona ila nikakudondokea wewe....
Husninyo siku hizi hanisalimii vizuri aisee....lol!!

Ndoa yenye mtoto aliyezaliwa kabla ni changamoto sana na watu wasipokuwa waangalifu wanabwaga manyanga!

Kuna jamaa yangu alilazimika kuzuiwa kwenda kwa mzazi mwenzake na kumleta mtoto nyumbani kwa sababu walikuwa wanatumia hiyo nafasi kumsalimia mtoto na mama wa mtoto....(wazazi wengine wanakuwa mabazazi)!!

Hii ni changamoto kwa kweli
 
Mimi ni mwanaume nilibahatika kupata mtoto wa kiume nje ya ndoa.
Sasa miaka 10 baadae nimeoa na nimemchukua huyu mtoto wangu naishi naye.

Sasa mke wangu ameniwekea masharti ambayo nafikiri ni magumu kutekelezeka. Naamini kuwa mwanamke niliye zaa naye ana haki ya kumuoma mtoto wake kila anapohitaji kufanya hivyo.

Sasa mke wangu hataki huyu mama mtoto afike nyumbani kumuona. Hataki mtoto aende kwa mama yake. Anataka mama mtoto akitaka mtoto tumtume housegirl ampeleke mtoto hoteli foleni halafu wakimaliza kuongea arudi naye.

Hali hii imeniingiza kwenye migogoro maana mama mtoto anaona namnyanyasa na upande mwingine mke wangu anaona pia namnyanyasa.

Hebu niambieni what is the beat way ku deal na hii situation?

Wewe ni mzungu ? Kama mwafrika piga ngumi za kutosha huyo mkeo, masharti unapanga wewe hapangi mke mbona wanaume wa kihaya ni vibonde hivi
 
Hii itawezakana endapo huyo mama wa mtoto hayuko kwenye ndoa. Endapo yuko kwenye ndoa hali inaweza kuwa tofauti.

Mshikaji wangu alimchukua mtoto baada ya ugomvi na mkewe, ila baadaye walishindwa na kumrudisha mtoto kwa mama. Huyo mama naye aliolewa na ikabidi mtoto abaki na bibi.

Kwa ufupi ni maisha ambayo yana changamoto nyingi sana. Hakuna njia rahisi au ya mkato.
Aisee babu mimi nashindwa kabisa kumuelewa mwanamke ambae anakubali ndoa inayomfanya mtoto wake aonekane mchungu. Sijui kama ni utoto ama lack of experience ila nashidwa kabisa. Hao ndo wale wanaosaidia waume zao kuwakandamiza watoto wao wenyewe ili mradi tu ndoa izidi kuwepo.
 
Over my deadbody mama yangu hawezi kulea mtoto wangu jukumu lake alishamaliza.

Kama mtoto yuko under age abaki na mama yake na hata akiwa over age ruksa pia historia inaonesha kwenye situationa kama hii tena mtoto wenyewe utakuta ni mmoja aachwe amfariji mama yake, Baba unaclear bill tu. Umeoa mwanamke mwingine zaeni wa kwenu kama unadhani mpaka kuitwa Baba au mama au fulani ni mchezo.
Sindo hapo sasa. Unakuta mwanamke mwenyewe anaeng'ang'ania mtoto achukuliwe hafanyi kwa mapenzi yake kwa mtoto ila kwa insecurities zake binafsi. Mtoto anaishia kuishi maisha ya shida wakati haikuwa lazima.

Wazee wapumzike. Walozaa walee wenyewe.
 
Kweli kila mtu ana akili na roho ya kipekee.

Kwahiyo wewe kwa akili yako una uhakika kwamba huyo mkeo ndo atakuwa na positive effect+influence na mtoto kuliko mama yake mzazi. Nyie ndo huangalia watoto wakinyanyaswa kwenye himaya zenu day in day out kisa ulimbukeni wa mapenzi.

Mke ninaye ishi naye nyumba moja hawezi kumtesa mwanangu huku mimi nikiwepo.

Nimeshuhudia mengi ndugu yangu kuhusu hili Swala Kwahiyo mpaka nimesema hivyo basi ujue ni kwamba nimeyaona na kuyaishi. Mwanamke uliyezaa naye kwa asilimia kubwa sana akiona umeshaoa atamtumia mtoto kuvunja ndoa yako. Hujawahi sikia kesi ya mama wa mtoto kumtuma mwanaye akaweke sumu? Au mtoto akienda kukutana na mama yake anarudi kabadilika anakuwa na kiburi kwelikweli? Hizi kesi zipo Kwahiyo Si kila mama wa mtoto ni mwema na Si kila mama wa kambo ni mbaya. Ila kwa asilimia kubwa mama wa mtoto akishajua umeoa lazima alete vituko,Kwahiyo kuna mawili hapo either mtoto akae na mama yake Au mama yake asionane naye unless kama mama yake ni mstaarabu.

Kwahiyo usinihukumu bila kujua Sababu zangu za kufanya hivyo. I know it all na kwa niliyopita na kuyaona there is no way nikawa blinded na mke wangu juu ya malezi ya mtoto wangu.
 
Unajuwa hizi kesi hazifanani kama mwanamke uliyezaa naye hajaolewa na mwanaume mwingine na angalau anayamudu maisha yake mpe mtoto akae naye wewe utatoa matunzo, ni uselfish uliopitiliza mtoto kukosa mapenzi ya wazazi wake, inabidi ni lazima mmoja wenu akae na mtoto, binafsi siwezi kukubali mama yangu kulea watoto wangu, alishanizaa nimekuwa kazi yake imekwisha kama ng wajukuu watamtembelea weekend na kuspend naye likizo inatosha na yeye wale good time na mume wake siku zao zilizobaki.

Mkuu sijasema mtoto aishi na babu na bibi yake. Nilichosema ni kwamba huyo mama wa mtoto akitaka kumuona mtoto wakaonane nyumbani kwa wazazi wa baba. Wakishaonana na kuspend time then mtoto anarudi kwa baba yake. Kwa babu yake panakuwa ni meeting point.
 
Mke ninaye ishi naye nyumba moja hawezi kumtesa mwanangu huku mimi nikiwepo.

Nimeshuhudia mengi ndugu yangu kuhusu hili Swala Kwahiyo mpaka nimesema hivyo basi ujue ni kwamba nimeyaona na kuyaishi. Mwanamke uliyezaa naye kwa asilimia kubwa sana akiona umeshaoa atamtumia mtoto kuvunja ndoa yako.

Kwahiyo usinihukumu bila kujua Sababu zangu za kufanya hivyo. I know it all na kwa niliyopita na kuyaona there is no way nikawa blinded na mke wangu juu ya malezi ya mtoto.
Hilo la kuhakikisha mtoto hanyanyaswi ni jema, ni vizuri una uhakikisha hilo. Lakini bado hutumii busara wala haki kusema mtoto asiende kwa mama yake kamwe. Kama ulijua ulozaa nae sio mwema kwanini ulizaa nae on the first place. Ungesubiri ukazaa na ambae ni mke wako ili kusiwe na mtafaruku wa aina yoyote ile.
 
Sometimes inabidi wachangiaji tuwe extrimist tuu no way out!

Baba ndio kichwa cha nyumba hakuna mwingine wa kumpangia ratiba wala cha kufanya

Ukiwa umezaa kabla ya ndoa iwe bahati mbaya au makusudi kaa tayari kwa mitatizo kama hii

Huwezi kupanda mchongoma ukavuna bolibo

Am out!
 
Mkuu sijasema mtoto aishi na babu na bibi yake. Nilichosema ni kwamba huyo mama wa mtoto akitaka kumuona mtoto wakaonane nyumbani kwa wazazi wa baba. Wakishaonana na kuspend time then mtoto anarudi kwa baba yake. Kwa babu yake panakuwa ni meeting point.


Kama mmekubaliana na kuridhia huo utaratibu basi ni sawa. Ila kama anavyosema Lizzy, wakati mwingine mmoja wenu anaweza kuwa anatumia mabavu na hilo siyo sawa.

Hata hivyo, lazima kuwepo na jitihada kubwa kulinda ndoa, na pia kuangalia ustawi wa mtoto!
 
Last edited by a moderator:
Kama ulijua ulozaa nae sio mwema kwanini ulizaa nae on the first place. Ungesubiri ukazaa na ambae ni mke wako ili kusiwe na mtafaruku wa aina yoyote ile.

Inaonyesha unaongelea kwa hisia zaidi kuliko uhalisia.

Hakuna ambaye anapenda kuzaa nje ya ndoa,hilo ulifahamu kwanza. Bali ni circumstance zinatokea watu mnashindwana. Hamna mtu ambaye anaweza kuzaa na mtu ambaye Si mwema.

Pia elewa kuwa mnapokuwa kwenye mahusiano kila mtu anakuwa mwema ila makucha ya mtu huonekana pale ambapo mnaanza kutofautiana. Na wanawake wengi walio na watoto nje ya ndoa hapo ndipo wanakoseaga, wanakuwa frustrated sana na swala la ndoa kiasi kwamba anaanza kufanya mambo ya ajabu kwa mzazi mwenzie(Si wanawake wote),hapo ndipo unaanza kujua Her true color. Kuna wakati mtu unafikiria pengine umuoe kwa ajili ya mtoto lkn ukifikiria kero na vituko alivyofanya unaona kabisa huwezi vumilia Sababu unakuwa umesha mjua ni mtu wa aina gani. Hakuna aliye mkamilifu lakini kuna vitu mtu akifanya huwezi kufikiria Mara mbili kumuoa au kukuoa

Hata wewe leo hii kama upo na mtu wako utakuwa mwema lkn mambo yakisha enda kombo ndio ubaya wako utakapo julikana. Hivyo hiyo kauli yako hapo juu si sahihi.
 
Kama mmekubaliana na kuridhia huo utaratibu basi ni sawa. Ila kama anavyosema Lizzy, wakati mwingine mmoja wenu anaweza kuwa anatumia mabavu na hilo siyo sawa.

Hata hivyo, lazima kuwepo na jitihada kubwa kulinda ndoa, na pia kuangalia ustawi wa mtoto!

Mama ana Haki ya kumuona mtoto wake,tena binafsi ningependa mtoto aishi na mama yeke kuliko Kuishi na mimi. Lakini kuna wanawake wengine wanafanya makusudi kulazimisha mtoto aishi kwa baba ili apate fursa ya kuvuruga ndoa yako. Yani usije kuomba kukutana na mwanamke wa aina hiyo,huyu mkuu Lizzy anaongea tu kirahisi,unafikia kipindi inabidi kufanya maamuzi magumu ambayo mtu wa kawaida atakuona una Roho mbaya Lakini kiuhalisia ni kwasababu una jitahidi kuhakikisha things don't fall apart lkn Mzazi Mwenzio Yupo busy kukupa stress kwa kumtumia mtoto
 
Last edited by a moderator:
xfactor pamoja na yote hayo bado humtendei haki mzazi mwenzio. Besides, unadhani kwa kumkataza mtoto kwenda kwake ndo hatajaribu kukuharibia ndoa yako kama lengo lake ni hilo?! Be fair, kama unavyopenda wewe kukaa na mwanao ndo na yeye anapenda vile vile, mpe uhuru nae. Pia usidhani mtoto atakuja kukushukuru kwa hilo. Maana hapo ulipo unafikiria "ndoa yangu, ndoa yangu" na wala sio mtoto. Don't be like that aisee. Binafsi nisingefurahia kama mtu nlonae angekuwa kama wewe iwapo angekuwa amezaa kabla ya kukutana na mimi. Besides, Sio kila ubaya unaokusudiwa humfika mtu, mengine hupita tu kwahiyo usiishi kwa hofu ya kufanyiwa ubaya kupitia mtoto. Pia kumbuka kwamba huyo mtoto anakua na atakuja kufanya maamuzi yake mwenyewe linapokuja swala la kuonana/kuwa na mama yake mzazi. How will you control him/her then?! Kama ujinga si atajazwa tu?!

Muhimu ni wewe kutumia nafasi yako kama baba,mume na mzazi mwenza vizuri. Usikandamize sana upande mmoja ukapendelea kwingine na mwisho ukaishia kuharibu badala ya kujenga kama ulivyokusudia.
 
Last edited by a moderator:
Siyo lazima kuchangia kila thread, grow up.

na wewe ulichochangia nini hapa? Acha kujifanya mjuvi na mwenye busara wakati ni mburula tu!
Kila mtu ana uhuru wa kuchangia aonavyo inafaa usilazimishe kila mtu afikiri utakavyo wewe!
 
Mama ana Haki ya kumuona mtoto wake,tena binafsi ningependa mtoto aishi na mama yeke kuliko Kuishi na mimi. Lakini kuna wanawake wengine wanafanya makusudi kulazimisha mtoto aishi kwa baba ili apate fursa ya kuvuruga ndoa yako. Yani usije kuomba kukutana na mwanamke wa aina hiyo,huyu mkuu Lizzy anaongea tu kirahisi,unafikia kipindi inabidi kufanya maamuzi magumu ambayo mtu wa kawaida atakuona una Roho mbaya Lakini kiuhalisia ni kwasababu una jitahidi kuhakikisha things don't fall apart lkn Mzazi Mwenzio Yupo busy kukupa stress kwa kumtumia mtoto

Nakuelewa sana mkuu. Siku zote nadharia ni tofauti na hali halisi...

Practical experience ndiye mwalimu wa kweli.

Sina tatizo endapo maamuzi yako/yenu yameridhiwa na wadau wote (Mke, mama wa mtoto na wewe mwenyewe)! Au hata kama hakuna maridhiano, basi mmekubaliana kwamba ndiyo njia bora kwa sasa!
 
Mimi ni mwanaume nilibahatika kupata mtoto wa kiume nje ya ndoa.
Sasa miaka 10 baadae nimeoa na nimemchukua huyu mtoto wangu naishi naye.

Sasa mke wangu ameniwekea masharti ambayo nafikiri ni magumu kutekelezeka. Naamini kuwa mwanamke niliye zaa naye ana haki ya kumuoma mtoto wake kila anapohitaji kufanya hivyo.

Sasa mke wangu hataki huyu mama mtoto afike nyumbani kumuona. Hataki mtoto aende kwa mama yake. Anataka mama mtoto akitaka mtoto tumtume housegirl ampeleke mtoto hoteli foleni halafu wakimaliza kuongea arudi naye.

Hali hii imeniingiza kwenye migogoro maana mama mtoto anaona namnyanyasa na upande mwingine mke wangu anaona pia namnyanyasa.

Hebu niambieni what is the beat way ku deal na hii situation?

Huyo mkeo ana common sense kweli?
 
Lakini kuna wanawake wengine wanafanya makusudi kulazimisha mtoto aishi kwa baba ili apate fursa ya kuvuruga ndoa yako. Yani usije kuomba kukutana na mwanamke wa aina hiyo,huyu mkuu
Well ukisema hivyo napata point yako na taratibu naanza kukuelewa.

Kama kalazimisha mwenyewe tena kwa nia mbaya then nakosa jinsi ya kumtetea. Good luck xfactor ila hakikisha kwamba hulindi ndoa yako ukasahau kumlinda mtoto.
 
Last edited by a moderator:
xfactor pamoja na yote hayo bado humtendei haki mzazi mwenzio. Besides, unadhani kwa kumkataza mtoto kwenda kwake ndo hatajaribu kukuharibia ndoa yako kama lengo lake ni hilo?! Be fair, kama unavyopenda wewe kukaa na mwanao ndo na yeye anapenda vile vile, mpe uhuru nae. Pia usidhani mtoto atakuja kukushukuru kwa hilo. Maana hapo ulipo unafikiria "ndoa yangu, ndoa yangu" na wala sio mtoto. Don't be like that aisee. Binafsi nisingefurahia kama mtu nlonae angekuwa kama wewe iwapo angekuwa amezaa kabla ya kukutana na mimi. Besides, Sio kila ubaya unaokusudiwa humfika mtu, mengine hupita tu kwahiyo usiishi kwa hofu ya kufanyiwa ubaya kupitia mtoto. Pia kumbuka kwamba huyo mtoto anakua na atakuja kufanya maamuzi yake mwenyewe linapokuja swala la kuonana/kuwa na mama yake mzazi. How will you control him/her then?! Kama ujinga si atajazwa tu?!

Muhimu ni wewe kutumia nafasi yako kama baba,mume na mzazi mwenza vizuri. Usikandamize sana upande mmoja ukapendelea kwingine na mwisho ukaishia kuharibu badala ya kujenga kama ulivyokusudia.

Upo sahihi Lakini tatizo ni kwamba mtazamo wako umekaa katika hisia kwamba Mume anawaza ndoa yake. Hata kama hujaona kwa hali ya kawaida baby mamas huwa ni wasumbufu,mbaya zaidi ana mtumia mtoto kutimiza matakwa yake

Naomba uelewe kuwa mimi sipingi mtoto kuonana na mama yake,na kama nilivyosema hapo juu kuwa I prefer mtoto aishi na mama yake kuliko kuishi na mimi. Lakini tabia na mwenendo wa mama yake ndio Sababu ya mimi kuwa na msimamo huo wa bora kuzuia mtoto asionane na mama yeka. Mtoto kama Atakuja kinilaumu akisha kuwa mkubwa I will take the blame lakini stress za mama wa mtoto wako zisikie tu kwa wengine ndugu yangu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom