Kwa nini wanaume hamtukubali na watoto

Kwa nini wanaume hamtukubali na watoto

Yaani Mgirik kanivunja nguvu kabisa.
Najua wanaume watavutia upande wao.
Ila kiukweli tatizo kubwa lipo kwa mama zao.
Mgirik kasema kule juu, endapo utang'ang'ania kuoa mke mwenye mtoto, na nduguze hawamtaki.....akisafiri je, na kama unavyojua gubu la mawifi....ndio maana eti anaoa mke kigori.
.....Mimi nakataa....ukimpenda mwanamke, hata mama yako aongee mpaka apasuke mdomo, kama mmependana, watagonga mwamba tu

yawezekana unajua ila hujaelewa na unasikia lakn hujaona.
Hakuna kitu kigumu kama kutengwa na familiya yako. Usiangalie leo bali angalia hata kesho,,. Ipo siku mm ntakosa kuelewana na mke wangu huyo ndipo hapo gunia la misumali linaponiangukia.
 
Last edited by a moderator:
Hivi unadhani ni kitu rahisi kufanya hayo maisha huku wazazi hawajaridhia????

Sio kila ushauri wa mzazi unapaswa uutii.....wazazi wengine kavu tu.
Inabidi utumie ujasiri wa hali ya juu kuukubali, la sivyo, unajipindua tu mkuu.
 
This is not about the money my dear its about the love

mbona unakuta hata mama huyo ana kazi na hamtegemei mwanaume kihivyo??

Hata kama mama ana kazi jukumu la kutunza familia linaeleweka ni la mwanaume....
 
Dah sio wote aise ila kwa upande wangu sija bahatika kukutana na mwanamke mwenye watoto wa nje na ikitokea bas nita wa care kama wanangu wa kuwazaa coz mi mwenyew nimelelewa na baba wa kufikia na nimepewa elimu,malezi sawa bila kuonyesha ubaguzi kwa watoto wote japo alisha fariki lakini nilimueshimu kama baba na baba alie nizaa simjui mpaka leo. So mtu kama mimi sioni kama watoto wa mwanamke ni kipingamizi cha yeye kuishi na mi
mi na hata kama ana watoto wa 3 nitamshauri awa lete tuishi pamoja coz na wenyewe ni members wa familia.


Hongera sana kwa kulitambua hili,shits do happen kwenye maisha
 
  • Thanks
Reactions: 7ve
yawezekana unajua ila hujaelewa na unasikia lakn hujaona.
Hakuna kitu kigumu kama kutengwa na familiya yako. Usiangalie leo bali angalia hata kesho,,. Ipo siku mm ntakosa kuelewana na mke wangu huyo ndipo hapo gunia la misumali linaponiangukia.

Mkuu mahali ambapo naweza tofautiana na wazazi ni kwingine ila sio ktk mchakato wa kuingia ktk taasisi ya ndoa...
 
Hebu nitumie number yako nikutumie pesa ya sikukuu....umejibu PERFECT.
Khantwe nadhani leo uko kwenye ubora wako.

Woow....nimeshakutumia PM. Nlikuwa nafikiria mwaka mpya huu ntatoka vipi
 
Last edited by a moderator:
Sio kila ushauri wa mzazi unapaswa uutii.....wazazi wengine kavu tu.
Inabidi utumie ujasiri wa hali ya juu kuukubali, la sivyo, unajipindua tu mkuu.

Na ndio maana rate ya divorce now ni kubwa than ever,
Rate ya kesi za mahusiano zilizoko mahakamani ni kubwa kuliko zamani.
Rate ya vifo vya sababu ya mapenzi ni kubwa kuliko zamani.
Rate ya mabifu mengi sio pesa Bali mapenzi


Sababu ni nn??ujuaji...... We think we know better than them parents.
 
chanzo kwamba tunawabaka au?

chanzo ugomvi dhid ya wanawake wenye watoto kuolewa.

1. Huwez kukubali kaka yako aoe mke mwenye mtoto wakat yeye hajawahi kuoa wala kuwa na mtoto
2. Ndio chanzo cha ugomvi na wake zetu. Huwez kuishi na wifi yako kwa mda wa mwaka mmoja bila kugombana.
3. Mmejaa nyodo, kejeli na dharau kwa mawifi zenu hasa kama kaka yako ni tajiri na hasa kama hawajatafuta wote.
4. Kivumbi na jasho ni pale wifi yako hajashika mimba mnaanza mitusi kibao.
Yaan nyinyi wanawake sijui mna roho gan
 
yawezekana unajua ila hujaelewa na unasikia lakn hujaona.
Hakuna kitu kigumu kama kutengwa na familiya yako. Usiangalie leo bali angalia hata kesho,,. Ipo siku mm ntakosa kuelewana na mke wangu huyo ndipo hapo gunia la misumali linaponiangukia.

Msitubebeshe mizigo jamani.
Wangapi wametengwa mpaka wewe uogope?
Vaa mabomu ujilipue
 
Yaani Mgirik kanivunja nguvu kabisa.
Najua wanaume watavutia upande wao.
Ila kiukweli tatizo kubwa lipo kwa mama zao.
Mgirik kasema kule juu, endapo utang'ang'ania kuoa mke mwenye mtoto, na nduguze hawamtaki.....akisafiri je, na kama unavyojua gubu la mawifi....ndio maana eti anaoa mke kigori.
.....Mimi nakataa....ukimpenda mwanamke, hata mama yako aongee mpaka apasuke mdomo, kama mmependana, watagonga mwamba tu

ki ukweli wanaume wawe na misimamo
maana hata kama kaoa mwanamke asie na mtoto
Mafiwi watasema mbona
HANA MATTAKO MAKUBWA
MBONA HANA NYWELE NYINGI

and the like ifikie hatua mwanaume asimame kama mwanaume
kwani anamuolea nani??
kila mtu akitoa kigezo chake patakalika??wifi aseme anataka nyonyo,mama aseme anataka fig no 9

waat
 
Last edited by a moderator:
chanzo ugomvi dhid ya wanawake wenye watoto kuolewa.

1. Huwez kukubali kaka yako aoe mke mwenye mtoto wakat yeye hajawahi kuoa wala kuwa na mtoto
2. Ndio chanzo cha ugomvi na wake zetu. Huwez kuishi na wifi yako kwa mda wa mwaka mmoja bila kugombana.
3. Mmejaa nyodo, kejeli na dharau kwa mawifi zenu hasa kama kaka yako ni tajiri na hasa kama hawajatafuta wote.
4. Kivumbi na jasho ni pale wifi yako hajashika mimba mnaanza mitusi kibao.
Yaan nyinyi wanawake sijui mna roho gan

haya mambo karne hii bado yapo .. basi kazi kweli kweli
 
sawa nimekuelewa
Kwa hiyo waliozalishwa haijalishi katika situation gani
hawastaili kuolewa tena??

Hapana...inategemea interest ya huyo mwanaume anayeolewa nae na utaratibu walivyoupanga....si wanaume wote wanakataa kuoa single mothers wapo wengi tu wanaoa na tunaona singo mothers wanaolewa deile
 
Nimemjibu kuwa kiukweli sitakubali.
Kaka yangu hata hajala mshahara wake vizuri, halafu analetewa mtoto....nikiwa kama wifi, SITAKI IFRS

Madame, umewakilisha kundi kubwa la wanawake!! Hiyo ndiyo hali halisi, wanaume mara nyingi huwa hatuna hayo matatizo ya kiviiile!! Hata angalia mahusiano ya Zari mwenye watoto watatu na Diamond wanaopinga sana yale mahusiano ni wanawake!!

Wanawake mpo nyuma maasi mengi ya wanaume ila hamjioni tu!!
 
Duu!!! Wanaume ni wabinafi sana kwani Mimi nalea watoto 3 wa mwenzangu na wanatabia za ajabu mfano wananiibia nguo, ela na kuwapelekea mama Zhao then kibaya zaidi huyo mwanaume anawasiliana na mke aliyezaa naye. Nikimuuliza ananijibu eti wanawasiliana kwa ajili ya watoto. Imenichosha sana na wanapigiana simu wakati wa usiku tukiwa tumelala.
 
Mi mwenyewe siwezi kukubali kulea mtoto wa mtu
 
Mkuu mahali ambapo naweza tofautiana na wazazi ni kwingine ila sio ktk mchakato wa kuingia ktk taasisi ya ndoa...

ww waache tu wanajifanya hawajui wakat ukweli wa mambo wanaujua vzr kabisa.
 
Back
Top Bottom