Kwa nini wanaume hamtukubali na watoto

Kwa nini wanaume hamtukubali na watoto

Kila atakapoenda kuwekeza lazima aache watoto.
Matokeo yake akitaka kuoa, mama mzazi atataka mke asiyekuwa na mtoto, matokeo yake nakuja kulea mimi watoto

ni majanga hawa viumbe WABINAFSI
 
Ni ngumu mno

Ujue taasisi ya ndoa hata ktk vitabu vya dini inaanza na Baraka za wazazi...
Sasa kabisa nianze kuwa kichwa ngumu kwa mama kisa mwanamke ambae alishindwa jiheshimu hadi akadungwa mimba????huo upuuzi sijaufanya bado....
Yaani na ninavochukia watoto nje ya ndoa ndo kabisa.
 
Unapozungumzia kuishi na mtu unazungumzia ku-share majukumu. Kumbuka mtafutaji mkubwa(kwa familia nyingi) ni baba. nadhani Khantwe kajibu vizuri sana

sawa nimekuelewa
Kwa hiyo waliozalishwa haijalishi katika situation gani
hawastaili kuolewa tena??
 
Last edited by a moderator:
Ujue taasisi ya ndoa hata ktk vitabu vya dini inaanza na Baraka za wazazi...
Sasa kabisa nianze kuwa kichwa ngumu kwa mama kisa mwanamke ambae alishindwa jiheshimu hadi akadungwa mimba????huo upuuzi sijaufanya bado....
Yaani na ninavochukia watoto nje ya ndoa ndo kabisa.

Ni limbukeni wa mapenzi ndie atakubali kugombana na wazazi wake kisa mwanamke
 
Kwahiyo mimi nikikuhitaji unioe wakati nina mtoto na baba yake anaishi tu mjini hapa imekula kwangu.
Duhhhh!!!!!....kweli kazi.
Ila kupenda ni kitu kingine Innocizy, waweza kuta penzi na upendo unaoupata toka kwa kigori ni mabaya afadhali hata ungeoa mwenye mtoto am aye ana kidhi vigezo

Ni kweli kabisa....who knows
 
Last edited by a moderator:
Mtoto sio wangu,mpelekee mwenyewe,siwezi kutunza familia ya mtu labda awe amekufa
 
Jamii itasema vibaya kwa mwanaume kuoa mwanamke ambaye tayar ana mtoto/watoto......Ngoma dro kama wote mtakua mna watoto nje
 
Hawanalolote ni wabinafsi tu ila wao kuzaa nje na kuleta watoto ndani wanaona sawa tu
 
Ni swala la ajabu sana ambalo pengine ukilifukiria unaeza ukasikitika

ni kawaida sana wanaume kutuambiwa wana watoto hata watatu na wenyewe kuona kawaida sana bila hata kutushawishi kwamba utaishi na mwanangu

yaani wao uchukulia kawaida sana sisi kuishi na watoto wao bila kuuliza chochote na wao huona sinkikwazo chochote na pindi utakapokionesha basi unaonekana Mkatili unaonekana wewe sio mke mwema(JAPO KUNA WANAWAKE HUKATAA ) ila sio wengi

SASA IJE SISI NDO TUNA WATOTO
wanaume wengi hukataa kuoa mwanamke mwenye mtoto KWA MSISITIZO na hata kama akikubali husema basi mtoto wako akae kwa bibi au baba ake sijui atawajibika
na mambo mengi hapo katikati

SASA SWALI NI JE KWANINI NYIE MNAONA SISI KUKAA NA WATOTO WENU NI RAHISI LAKINI NYINYI KUKAA NA WETU NI ISSUE tena kubwa sana????


Kwa sababu Wanaume wa Tanzania woote ni wanaume suruali tu labda na mkanda basi, zaidi hapo hamna kitu, na hiyo ni mpaka raisi wa nchi!
 
hilo ndio la msingi. Wanawake nyinyi ara nyingi ndio mnakuwa chanzo

Chanzo ni jamii husika....wanaume na wanawake na mazoea ya jamii husika...
Ukisema wanawake peke yake unakua unakosea,ni uonevu.
 
Roho ya kibinafsi tu, kama ishu ni kuogopa kukumbushia kwani mwanaume hawezi kukumbushia....
 
Back
Top Bottom