BABA SANIAH
JF-Expert Member
- Oct 20, 2013
- 4,777
- 6,267
wanasema utarudi kwa uliyezaa naye... ila wanaume ni wabinafsi sana
Kuliko wewe miss chaga
wanasema utarudi kwa uliyezaa naye... ila wanaume ni wabinafsi sana
ewaa!! Huo ndio mtihan tunaopata hata sisi.
Nafikiria mengi kuwa nikioa mwanamke mwenye mtoto atapata tabu tu, najua mm peke yake ndio ntakuwa msaada kwake wala sio wifi zake wala mama mkwe wake,.
Huyo mwanamke lazma atachukiwa na ndg zangu wote, kunaleo na kesho labda mm nmesafiri ile safar ya kudumu basi mkew wangu atakuwa kinyago mbele za mawifi zake atakuwa mtu mwenye kutukana na kutengwa. Sasa kwann tufikie huko? Soln ni kuoa asiye na mtoto
Mie mwanaume nilienae, amempokea mwanangu tangu yuko tumboni na mpaka leo hii ana 7 years niko nae mpaka mwanangu anajua kuwa yule baba yake....
Ila ngoma iko upande mwingine....mawifi waliweka ngumu, lakini mwisho wa siku, ilibidi wakubali matokeo maana wakinikuta nami kisiki cha mpingo.
Ila masai dada, MAWIFI na MAMA WAKWE NDO TATIZO.
ukifa mkeo asiolewe????
aisee...inategemea anaweza kuhusika labda ndio maana sitaki hio habari....lakini mwanamke ndio ataamua anikubali na mtoto au la...ila mimi mwanamke mwenye mtoto...ni no no no!
Wanaume wabinafsi
Hapana mkuu nimependa tu alivyojibu...hahahahahaaaa mkwara wakati mwingine unafaida.kuna kitu unakitafuta lakn bila shaka utakipata. Endelea kuchombeza wake za watu
Dah sio wote aise ila kwa upande wangu sija bahatika kukutana na mwanamke mwenye watoto wa nje na ikitokea bas nita wa care kama wanangu wa kuwazaa coz mi mwenyew nimelelewa na baba wa kufikia na nimepewa elimu,malezi sawa bila kuonyesha ubaguzi kwa watoto wote japo alisha fariki lakini nilimueshimu kama baba na baba alie nizaa simjui mpaka leo. So mtu kama mimi sioni kama watoto wa mwanamke ni kipingamizi cha yeye kuishi na mimi na hata kama ana watoto wa 3 nitamshauri awa lete tuishi pamoja coz na wenyewe ni members wa familia.
Mama yangu baada ya baba kufariki aliolewa tena na huyu baba wa sasa...na ndiye alietulea na kutusomesha mpaka chuo huyu Mzee.
So to me mwanamke mwenye mtoto nnayeweza kumuoa ni mjane tuu na sio uruke ruke huko wakumimbalize utarajie kuolewa na mm,never.
kabisaa madam
wengi humghasi sana mume
kama mume atawasikiliza hamna ndoa hapo
japo pia wanaume wengi wenyewe hawataki
AISEEE MPENDE MUMEO KULIKO CHOCHOTE
Iga mfano wa baba yako wewe
.....na ndio wanaoongoza kwa kuchagua wachumba ambao hawajazaa wakati huku nyuma ana msururu wa Azam team.
Yaani Mgirik kanivunja nguvu kabisa.
Najua wanaume watavutia upande wao.
Ila kiukweli tatizo kubwa lipo kwa mama zao.
Mgirik kasema kule juu, endapo utang'ang'ania kuoa mke mwenye mtoto, na nduguze hawamtaki.....akisafiri je, na kama unavyojua gubu la mawifi....ndio maana eti anaoa mke kigori.
.....Mimi nakataa....ukimpenda mwanamke, hata mama yako aongee mpaka apasuke mdomo, kama mmependana, watagonga mwamba tu
Ni poa kuishi na watoto wa kufikia ila wanawake wa cku izi hawanamisimamo ktk maaamuz yao, akija baba mtoto kampigia magoti basi michanuo kama kawaaa...
Hivi unadhani ni kitu rahisi kufanya hayo maisha huku wazazi hawajaridhia????
Mie mwanaume nilienae, amempokea mwanangu tangu yuko tumboni na mpaka leo hii ana 7 years niko nae mpaka mwanangu anajua kuwa yule baba yake....
Ila ngoma iko upande mwingine....mawifi waliweka ngumu, lakini mwisho wa siku, ilibidi wakubali matokeo maana wakinikuta nami kisiki cha mpingo.
Ila masai dada, MAWIFI na MAMA WAKWE NDO TATIZO.
Ndio maana nimesema mwanamke mwenye mtoto nnaeweza oa ni yule ambae alikua ameolewa na mumewe bahati mbaya akafariki...(huyu baba alimuoa mama baada ya baba yangu mzazi kufariki,na hiyu baba pia mkewe alikua ashafariki zamani,so walioana waliopoteza wenza)