Kwa sababu hao wanaotaka kulipwa sana wanazalisha kidogo !!!
Kwa sababu hao wanaotaka kulipwa sana wanazalisha kidogo !!!
1. Mishahara BoT, Wakurungenzi, Wizarani, Waalimu Elimu ya Juu (public), watafiti, madaktari nk yaani hawa wote wana mishahara mizuri tu sana! Yaani mishahara isiyopungua 1.5 -2 m kwa mwezi- inategemea umefanya kazi mda kiasi gani! Pia wengine wana marupurupu makubwa kuliko mishahara!
Pengine tujilaumu sisi wenyewe!
Isitoshe, kuangalia mishahara tu bila kuangalia bei za vitu na mfumuko wa bei ni kuangalia nusu ya jambo hili tu.
Waalimu wa Hungary wanaweza kulipwa nusu ya wakurugenzi wa Tanzania, lakini kama bei ya vitu Hungary ni robo ya level ya bei ya vitu Tanzania, ukiangalia purchasing power parity utaona walimu wa hungary wanalipwa zaidi in real terms kwa sababu wanaweza kununua vitu vingi zaidi.
Kwamba bei ya vitu Hungary ni robo ya level ya bei ya vitu Tanzania? Sina uhakika. Ila kulicho wazi ni kwamba stlye ya maisha na majukumu yanatofautiana. Kwa mfano mfanyakazi ya TZ most likely ana extended family, ana jukumu la kumlipa mfanyakazi wa ndani, mlinzi, etc. tofauti na mfanyakazi wa ki-Hungary - hii inaleta income strain.
Serikali ya Tanzania ni kubwa kuliko makusanyo ya kodi inayopatikana. Just imagine, Marekani li nchi likubwa ajabu, ina mawaziri 6 tuu, Tanzania kinchi kidogo, mawaziri na manaibu almost 60!.
Kutokana na ugumu wa maisha, waBongo hatuna utamaduni wa kulipa kodi. Tunajitahidi sana kuiba na kukwepa kodi huku tukijenga majumba kwa fedha za mfukoni bila mikopo!
1. Cost of Living Tz ni kidogo sana ktk EA kama unapata mshahara wa $ 2000 kwa mwezi! Pia inategemea unaishi wapi Tz ! Kumbuka kuwa mwal. primary anapata $ 150 na ni nchi hiyo hiyo!
2. Sina uzoefu na cost of living Romania: ila kumbuka wako ktk Romania na ktk EU $ 500 au hata $1000 ni pesa kidogo sana ukilinganisha na Standard of Living enoe la EU!
Mishahara ni midogo kwasababu nyingi - ikiwa ni pamoja na ukweli kuwa serikali inaajiri watu wengi zaidi ya wanaohitajika na kwa msingi huo kazi zinazofanyika ni kidogo ukilinganisha na kinachopatikana. Input kidogo =output kidogo.Wage bill kubwa utai justify vipi? Linganisha na taasis nyingine kama sekta binafsi au mashirika ya kimataifa.Huko unakuta badala ya kuwa na dereva, mhudumu, mfagizi, sekretari na mesenja kama ilivyo serikalini (watu watano) kazi zote hizi zinafanywa na mtu mmoja.Fikiria mshahara uliokuwa ulipwa mathalani watu watano, analipwa mtu mmoja. Kingine ni kuwa serikalini kuna uvujaji sana wa fedha - matumizi mabaya/makubwa kwa wachache wakati wengi hawapati hata mshahara wa kutosha kujikimu.