Teknolojia ni Alfa na Omega kwa mustakabali wa maendeleo ya Tanzania

Kyuku Lilu

Member
Mar 22, 2018
16
28
Salaam Wana JF!

Niende kwenye mada yangu kama hedingi hapo juu.

Kwanza naomba tusameheane kwa uandishi wangu, pili, hii mada ni kwa wale GT tu, kwa maana wenye kutazama mbaali, pia hii mada sii ya kisiasae, ingawa huwezi kujitenga na siasa. Mwisho, endapo utachangia hapa, nakuomba uwe siriazi. Kwa wale wote wenye mawazo ya kitoto, naombaywapishe mbali.

"Technolojia" ________ Sote twafahamu maana kamili ya neno hili.

Ili tuweze kuvuka hapa tulipo, tunaihitaji sana kuipata hii technolojia, ni ujuzi fulani wa kutengeneza kitu chochote kwa kuleta badiliko chanya ama hasi kwa mtu binafsi ama nchi

Kwetu TANZANIA, tunaihitaji kuchagua kitu gani tunaihitaji ili kujikwamua hapa tulipo

Kwa wale wenzangu wa kabla ya uhuru ('50s ______70s) , mtakumbuka kabla ya "Uhuru" tulikuwa na nini na baada ya UHURU awamu ya JKN tulifanikiwa kuwa na viwanda mbali mbali mali yetu kabisaa, tulivyoviendesha sisi wenyewe kwa kiasi kikubwa sana. Hapa nikiwa na maana ya viwanda mama, mfano: kiwanda cha UFI cha majembe ya mkono na plau, zana karibu zote za kilimo, viwanda vya RADIO, viwana tairi za gari, baiskeli, nguo, usindikaji nyama, madawa, usafishaji na ukataji madini vito, sabuni, siagi, mafuta na vingine vingi tu.
JE, kwa nini viwanda hivi vilifeli?

(1) Ni kwa sababu utawala uliokuwepo na hata huu uliopo kamwe haujawahi kuwa na lengo la kuipa kipaombele No.1 iwe ni tekinolojia, haukuwa na dira hiyo na hadi hawa waluopo hawana wazo hili. Kwani ili tutoke hapa tunaihitaji kufanya haya na lazime iwe hivi

(2) TUWE NA SERIKALI
(3) TUWE NA MAHAKAMA
(4) TUWE NA BUNGE (wanasisa)

SERIKALI - Hii ni lazima tuwe na taasisi IMARA na zenye nguvu ili kuweka mipango imara ya kimaendeleo bila kuyumbishwa na vyama vya siasa au vingozi wa vyama vya siasa.

MAHAKAMA - Iwe na nguvu kubwa ikishirikiana na SERIKALI ili kulinda mipango mkakati ya kimaendeleo iliyopanga na taasisi IMARA, viongozi wote hawa wasitokane na teuzi za kisiasa.

BUNGE/WANASIASA/DOMODOMO Hawa wapewe nini cha kukinadi (sera) toka SERIKALI I NA MAHAKAMA kwa ajili ya kuwaletea Maendeleo WANANCHI bila kujali ni chama gani kinaongoza, chama kitanadi mipango ya SERIKALI na MAHAKAMA.

Hivyo basi endapo tungekuwa hivyo tangu uhuru, tungekuwa na uwrzo wa kusonga mbele kimaendeleo bila kuyumbishwa na vyama ama chochote kama ilivyo kwa nchi kama China, Iran, N Korea, Pakistan, India, n.k.

Je, hapa tulipo tunaihitaji sana tufanye nini ili kuifikia hatua hii?
Je, tumechelewa sana?
Je, kuna haja ya kufanya mageuzi ya viongozi wetu?
Je, hawa viongozi wa sasa, kweli wana nia njema na Taifa letu TANZANIA?
Je, vijana wa kizazi hiki cha sasa ni nini matumaini Yao? Ama kwao yote sawa, iwe MVUA ama JUA yote kheri!
Kwangu mimi na wengine wa 50s/60s tunaiona hii dosari, je vijana waliona hii dosari? Wanawaza nini?
Naona leo niishie hapa, nitaiendeleza kwa undani zaidi hasa kwa wale wenye kuhitaji nasi tuwe moja ya taifa linalojivunia kumiliki tekinolojia take/yetu kwa maendeleo mbali mbali.
 
Vitu tulivyokua tunazalisha vilikua vizuri sana na vyenye ubora. Kule mwatex sijui pepo gani liliingia kule,zao la pamba linajikongoja. Tumechelewa sana saiv ni kizazi cha kujali sana faida kuliko ubora wa malighafi etc

#Hopenimeelewamada
 
Back
Top Bottom