deepsea
JF-Expert Member
- Aug 10, 2013
- 3,287
- 946
Tanzania mahali pazuri mno pa kuishi hata kama huna ujuzi wala elimu yoyote almradi tu uwe na shekeli kidogo, unahitaji chochote utapata iwe kibali cha kuishi na kufanya kazi nchini, hati ya kusafiria vyeti vya shule, chuo nk! lakini fungakazi ya yote ni leseni za udereva, karibia kika mgeni anamiliki leseni na ukienda kwenye database ya POLISI na TRA utakuta wametimiza vigezo vyote, ila katika uhalisia si kweli. vijana wengi wa bodaboda wanazo leseni lakini hata mlango wa chuo cha udereva haujui. uzalendo umetutoka kabisa kila mtu anaangalia anapata bei gani kwenye nini! na kwa njia hii tunaimaliza nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe
najipanga nikanunue udead afu baada ya 2015 uwaziri nikajichotee na mimi mijihela